Monday, February 25, 2019

MLO WANGU WA JIONI YA LEO UTAKUWA HUU NA CHA KUTEREMSHIA NI MAJI...

Karibuni tujumuike ndugu/rafiki zangu ni samaki kwa viazi....Nimekumbuka sana kule nilikozaliwa Nyasa ila kule kwetu kungekuwa na ugali wa muhogo weeeee

Wednesday, February 13, 2019

UJUMBE WA LEO- TOFAUTI BAINA YA SHULE NA MAISHA.....

Shuleni unajifunza somo/masomo na baadaye unapata mtihani. LAKINI- Katika maisha , kuna mitihani ambayo tunajifunza masomo.
PANAPO MAJALIWA , Kapulya wenu!

Tuesday, February 12, 2019

KUMBUKUMBU: NI SHAIRI LA SIKU NYINGI SANA NILIIMBA NIKIWA DARASA LA NNE



Nililiimba kipindi niko shule ya msingi ,nakumbuka ni darasa la nne na mpaka leo takribani miaka 30 zaidi bado nalikumbuka. Bila shaka shairi hili litakukumbusha yaliyo mema ya kipindi cha nyuma. Na cha kufurahisa zaidi kitabu hiki ambacho hili shairi lipo ninacho:-)

Monday, February 11, 2019

HIZI ZITAKUWA PICHA ZA MWZI HUU WA PILI

Nimeamka asubuhi ya leo na nikawa na hamu ya kula yai  kwa kawaida huwa napenda kula yai moja tu lakini lakini leo macho yangu yakakutana na maajabu haya katika yao moja nikaona ni mawili. Cha ajabu yao halikuwa kubwa kuliko kawaida....nimeyale yote :-)  Mara nikakumbuka kuna mtu alinitumia picha ....
...picha maajabu yaliyotokea mgomba mmoja umezaa mikungu minne ya ndizi. Hakika hii ni kali ya mwezi ..

Monday, February 4, 2019

TUANZE MWEZI HUU WA PILI KWA PICHA HII:-UMOJA NI NGUVU

 Kuna wengi watakumbuka hii kazi ya kutwanga  sio hapo zamani tu hadi sasa hasa vijijini bado wana enzi utamaduni huu. Lakini jamii ya sasa sijui kama kuna anayejua kinu   na mwichi ni nini...najivunia kuwa mmoja ninayeuenzi utamaduni huu pia hata kizazi changu. NAWATAKIENI MWEZI MPYA HUU UWE MWEMA.