Showing posts with label taswira. Show all posts
Showing posts with label taswira. Show all posts

Thursday, February 19, 2015

TASWIRA:- SEHEMU FULANI AFRIKA

Alhamis njema kwa wote...pabapo majaliwa tutaobana kesho ijumaa!!

Friday, November 18, 2011

TUANZE MAPUNZIKO AU MWISHO WA JUMA NA HII TASWIRA MWANANA KATIKA UFUKWE WA MBAMBA BAY!!!

Picha na maelezo toka blogu ya Profesa J. Mbele.
Mbamba Bay ni mji mdogo, kando kando ya Ziwa Nyasa, upande wa Tanzania. Ingawa umaarufu wa mji huu tangu zamani ni bandari, hapo ni mahali pazuri kwa mapumziko.Picha hii ilipigwa mwanzoni mwa Agosti, mwaka huu.Unaweza kusogea hapo ufukweni, ukawa unapunga upepo na kuangalia shughuli za wavuvi, wauzaji wa samaki, akina mama wakifua nguo, na watoto wakicheza majini. Kama unajua kuogelea, mahali hapo utafafurahia. Ukija siku ambapo meli inakuja, utajionea ujio wa meli na kuondoka kwake.


IJUMAA NJEMA KWA WOTE....

Tuesday, January 25, 2011

UNAKUMBUKA MICHEZO KAMA HII?

Nimekumbuka michezo kama hii nilipokuwa mdogo, maana katika familia yetu watoto wa kiume ni wengi zaidi kwa hiyo tulikuwa hawanibagui katika michezo....haya wewe je uliwahi kusafiri na gari kama hili????:-) brrrrrrrrrrrrrrr kanyonyonyooooooo twendeeee....

Thursday, June 24, 2010

Salaam kutoka Seminary ya Likonde!!

Jengo la Seminary kuu ya Likonde


Nimtume nani unatume mimi nitume bwana.
Leo nimetembelea Likonde Seminary na nimeona iwe picha ya wiki hii. Najua wengi mtakuwa na kumbukumbu nyingi kuhusu Likonde. Tukutane tena wakati mwingine.


Tuesday, June 22, 2010

Je? barabara hii itakufikisha wapi??

Barabara hii imenikumbusha mengi sana wakati wa utoto /zamani mtu umechoka una mzigo kichwani na barabara unaiona ndefuuuuuu. Haya karibu ni wapi hapa?