Showing posts with label nyimbo za utotoni. Show all posts
Showing posts with label nyimbo za utotoni. Show all posts

Friday, March 10, 2017

PALE WATU WAZIMA WANAPOKUMBUKA NYIMBO ZA UTOTONI ..NIMEPENDA SANA HII


Ndugu zanguni wapendwa hizi nyimbo ni hazina yabidi tuzihifadhi na pia tuwafundishe wanetu. Yaani laeo nimekumbuka sana enzi za utoto wangu...kama sio chekechea basi shule ya msingi na kama sio huko basi usiku wa mbalawezi.. IJUMAA NJEMA NA PIA MWISHO MWISHO WA JUMA UWE MWEMA SANA KWA WOTE MLIOPITA HAPA.....NI KAPULYA WENU:-)

Thursday, November 4, 2010

WIMBO HUU NI KWAKO DA´MIJA!!!!

Da´Mija

Najua utajiuliza kwa nini da´Mija aimbiwe wimbo lakini yeye nadhani anajua:-
Haya Mija tuimbe pamoja:-)
Shilingi ya Nyerere katikati kuna mwenge x2
Aah doilidoli aah doli Somora eeeh x2-
------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Haya hapa nimekumbuka nyimbo nyingine za utotoni:-
Twendeni tukawinde vipepeo x2
Aiya mama vipepeo vipepeo x2
Askari eeh vitani eeh x2
Kiongozi :- Wanabeba
Wote:- Wanabeba bunduki, bisi kibuyu cha maji vitani eeh x2

Kiongozi: Tumefika
Wengine: Bado. Mkifika mnakoenda mnaitikia tumefika

Kiongozi :-Nyama x2
Wengine:- wanaitikia nyama
Kiongozi anasema:- ya mbuzi,
wengine mnaitikia:- Nyama .....unaendelea hivyo kutaja wanyama woteeee. Wimbo huu ni mzuri naupenda kwani sio wimbo tu, pia unafundisha watoto kujua majina ya wanyama kwa urahisi.
Jamani mwenzenu nimekumbuka kweli zamani/utoto. Nawaombeni wote endelezeni hizi nyimbo kwa vizazi vyetu. Binafsi nawaimbia wanangu hasa wimbo huu TUMEFIKA, BADO ni pale watoto wanaonapo uvivu kufanya kitu fulani kwa mfano kwenda kulala au kupiga mswaki, basi tunaimba huu wimbo tunajipanga mstari huku tumeshikana mikono mabegeni na vichwa tumeinamisha chini isipokuwa yule wa kwanza atakuwa kiongozi na safari inaanza ........ujanja eeh!! Kama kuna anayejua nyimbo nyingine za utotoni karibu kutushirikisha na pia unaweza kugonga hapa kwa kupata nyimbo nyingine hasa za mchakammchaka wakati ule mwaka 1947:-)