Showing posts with label yesu. Show all posts
Showing posts with label yesu. Show all posts

Sunday, December 22, 2013

NI DOMINIKA YA NNE YA MAJILIO MWAKA A..PIA BADO SIKU CHACHE NA NDIPO ITAKUWA KUZALIWA KWAKE YESU MKOMBOZI WETU

"Bikira atachukua mimba, atamzaa mtoto wa kuime, naye ataitwa Emanuali" Maana yake "Mungu yupo pamoja nasi."
NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI HII KABLA KUZALIWA KWAKE BWANA WETU YESU KRISTO IWE NJEMA KWA WOTE. KAMA ILIVYOANDIKWA MUNGU YUPO PAMOJA NASI. WOTE MNAPENDWA....KAPULYA

Sunday, March 18, 2012

NI JUMAPILI YA NNE YA KWARESMA SASA: WOTE MUWE NA JUMAPILI NJEMA NA BARAKA ZA MWENYEZI MUNGU ZIWE KATIKA NYUMBA ZENU!!


Ni kipindi ambacho watu wahitaji kusameana na kuwa pamoja ...muwe na amani wote na baraka za mwenyezi Mungu ziwe kwenu. JUMAPILI NJEMA!!!

Sunday, April 24, 2011

KHERI KWA SIKUKUU YA PASAKA KWA WOTE!!


BWANA AMEFUFUKA NA WOTE TUFURAHI LEO....KHERI SANA KWA PASAKA!!!

Sunday, April 3, 2011

HEBU SIKILIZA HAPA JINSI WALIVYOJUA KUIGIZA...KAAZI KWELIKWELI


Muda mrefu nimekuwa mkimya bila kusikiliza miziki kwa ajiliya machungu yaliyonipata katika upekuzi wangu nimekutana nao hau kwa kweli wamenifanya nitabasamu kiduchu.. sijui nanyi wenzangu mtajiunga nami???

Sunday, June 6, 2010

JUMAPILI NJEMA KWA WOTE NA UJUMBE NI HUU UPITIOA KWA WIMBO HUU WA ZAKAYO!!!



Wimbo huu nadhani unaimbwa kwa kimasai nimeusikiliza mara nyingi na nikaona ni vema kulinukuu hili neno:-
Mtakatifu Luka 19: 1-10
”Naye alipoingia Yeriko alipita katikati yake. Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watoza ushuru, naye ni tajiri. Huyu alikuwa akitafuta kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, asiweze kwa sababu ya umati wa watu, maana ni mfupi wa kimo. Akatangulia mbio, akapanda juu ya mbuyu apate kumwona , kwa kuwa atakuja kuipitia njia ile. Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu akamwambia, Zakayo, shuka upesi, kwa kuwa leo imenipasa kushinda nyumbani mwako. Akafanya hharaka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha. Hata watu walipoona, walinungúnika wote, wakisema, Ameingia kukaa kwa mtu mwenye dhambi. Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang´nya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne. Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu. Kwa kuwa mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.”
TUMSIFU YESU KRISTO MILELE AMINA. JUMAPILI NJEMA WANDUGU!!!

Thursday, December 24, 2009

SALAMU ZA NOELI KUTOKA SWEDEN KWA WOTE ULIMWENGUNI!!!!

Kwa kawaida au niseme Noeli kwa sehemu nyingi ni kesho au kwa mimi lakini hapa Sweden Noeli ni leo 24/12. Kwa hiyo sisi au mimi na familia yangu tunapenda kuwatakieni wote
CHRISTMAS NJEMA/GOD JUL.

Sunday, November 29, 2009

JE? UNANIKARIBISHA NYUMBANI MWAKO!!!!!!! PIA LEO NI JUMAPILI/DOMINIKA YA KWANZA YA MAJILIO YA MWAKA C



Naondoka nyumbani kwa Yasinta sasa na nimeacha baraka, je? unanikaribisha kwako? Nipokee kwa upendo na unitume kwa wengine/nyumba nyingine ili niweze kuwabariki wao pia. Uwe na siku yenye baraka. Nipo mlangoni, nabisha hodi. Kama kuna mtu ananisikia na afungue mlango. Nitaingia ndani na kula nao/nanyi katika meza yenu/yao. Sasa anaenda nyumbani kwako mwache yeye akubariki na umwonyeshe nyumbanyingine. MUNGU NI MKUBWA!!!!!!!JUMAPILI NJEMA KWA WOTE!!!