Showing posts with label harusi. Show all posts
Showing posts with label harusi. Show all posts

Thursday, August 11, 2011

NILIPOKUWA NYUMBANI SONGEA/RUHUWIKO:- NILIPATA BAHATI SIKU HII MTAANI PALIKUWA NA HARUSI YA KIISLAM!!

Hapa bibi harusi ni huyo aliyejitanda kanga yaani wa pili. Hapo tayari amekwisha funga ndoa/harusi na sasa akisindikizwa kwa mume wake. Nilivyosikia ni kwamba, bibi harusi inabidi siku ya harusi anafungia hiyo ndoa/harusi nyumbani kwake na baadaye ndio aenda kwa mume wake. Ila hapa kwa mimi inanitatanisha kidogo. Kwa sababu utawezaje kufunga ndoa bila bwana kuwa pembeni? Niliuliza lakini sikupata jibu kamili. Naamini hapa kibarazani nitasaidiwa kupata jibu.



Safari inaendelea ....na hapo kulia ndio ilipo nyumba yetu...bahati mbaya sikualikwa kwenye sherehe yenyewe :-)



Thursday, May 5, 2011

HIVI HARUSI "NDOA" NI NINI?

Mara nyingi nimekuwa nikijiuliza hivi harusi "ndoa" ni nini? je ni mavazi, mwonekano, usafiri, chakula, vinywaji, muziki, watu, au ni UPENDO WA DHATI WA WATU WAWILI WAPENDANAO? Ebu angalia picha hizi hapa chini na sema unavyofikiri wewe karibuni ndugu zanguni:-

Picha hii ya kwanza mnaona wanaharusi ni harusi rahisi kabisa unadhani unaweza kufahamu yupi ni bibi harusi na yupi ni bwana harusi. picha toka kwa kaka Mjengwa

Na picha ifuatayo ni harusi "ndoa" iliyofanyika Ijumaa iliyopita kati ya Prince William na Kate.