Tuesday, May 30, 2017

MSIBA MKUBWA UMETUPATA UKOO WA AKINA NGONYANI PERAMIHO /LUNDUSI BABA/BABU NA KIONGOZI WETU KATUTANGULIA MBELE ZA MUNGU LEO MAPEMA ASUBUHI

 Hii picha ni wakati wa uhai wake hapa ilikuwa 2005 nyumbani kwetu LITUMBANDYOSI yeye ni huyo mwenye miwani yupo pamoja na wdogo zake.
Na hapa yupo na moja wa wajukuu zake ilikuwa mwaka 2016 November. Babu yetu Lotary  amekuw akiugua tangu kipindi cha pasaka
Na hapa ni picha yake ya mwisho iliyopigwa 28/12/2016.Wewe Ulikuwa Kiongozi wa ukoo wa akina Ngonyani, babu yetu,  baba yetu na pia mshauri mzuri sana pale mtu atakapo ushauri. TUNAMUOMBA MWENYEZI MUNGU  ATUTIE NGUVU KWA KIPINDI HIKI CHA MAOMBELEZO. BWANA AMETOA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIDIMIWE. UPUMZIKE KWA AMANI BABU YANGU/YETU. AMINA

Sunday, May 28, 2017

TUMALIZE JUMAPILI YA MWEZI HUU WA TANO KIHIVI,,,ASUBUHI NA NAFASI MPYA YA NDOTO ZAKO KUWA DHAHIRI

Asubuhi ni nafasi mpya ya kuzifanya ndoto zako kuwa dhahiri:- Fursa mpya, mipango mipya ...huja katika fikra.
Usifikiri sana kuhusu jana, juzi wala siku yoyote ambayo pengine ulikosa au ulishindwa jambo fulani...anza siku ya leo kwa kukiri kuwa itakuwa siku njema kuliko nyingine zote.
Siku, ni sehemu ndogo katika "MAISHA" ambayo Mungu hutuzawadia. Itumie vizuri, ifanye iwe ya MAANA KWAKO, USIPOTEZE TUMAINI....USIKATE TAMAA MUNGU YUPO PAMOJA NAWE SONGA MBELE DAIMA . Kumbuka "unaweza mambo yote katika yeye (MUNGU) akutiae nguvu" FIL 4:13 NAKUTAKIA ASUBUHI NJEMA, SIKU NA JUMAPILI YENYE BARAKA, AMANI NA FURAHA. AMINA!

Saturday, May 27, 2017

FAHARI YA TANZANIA:- PUNDAMILIA WA TARANGIRE

UTALII NDANI YA NCHI:- NAWATAKIENI WOTE MTAKAOPITA HAPA JUMAMOSI NJEMA SANA!

Wednesday, May 24, 2017

UJUMBE WA WIKI HII: MAISHA HAYAMTAMBULISHI MTU KWA WATU....

Maisha hayamtambulishi mtu kwa watu atakaokukutana nao. Kuna wakati, maisha yaweza kukukutanisha na watu ambao uliwahitaji/unawahitaji kukutana nao ili wakupe msaada, ili wakuumize, ili wakuongoze, ili wakuache mpweke, ili wakupende na ili wakupe/wakutie nguvu katika hatua ya  kukuimarisha ili uwe mtu imara katika maisha yako.....TUPO PAMOJA!

Tuesday, May 23, 2017

MBOGA NA MATUNDA NI MUHIMU KWA KILA BINADAMU

Lakini pia inasemekena tuwe makini , yaani kila kitu kiwe wastani tusizidishe. Maana utakuta mtu anaacha kula vyakula vingine na akawa anakula matunda tu...kumbuka katika matunda kuna sukari sana. NI UJUMBE WANGU KWENU...Kapulya wenu.

Sunday, May 21, 2017

JUMAPILI NJEMA...

 Vazi la Jumapili ya leo....nimekumbuka mtindo wa kufunga mkanda zilipendwa mmeona eeeh!
Kama kawaida mbwembwe  tu hapa nilikuwa sijui nikiomba?

Friday, May 19, 2017

NIMETUMIWA ZAWADI YA DAGAA NYASA

Ukiwa na hamu ya vyakula vya nyumbani na marafiki wanakutumia ni raha sana. Leo nimebahatika kutumiwa dagaa nyasa  na rafiki yangu mpendwa ....angalao nile kwa macho:-(. IJUMAA NJEMA KWA WOTE.

Thursday, May 18, 2017

MAMA HIVI ULIMPA MUNGU SHILINGI NGAPI?


Baada ya miaka saba ya ndoa bila kupata mtoto, Magreth alimuambia mumewe Benjamin kuwa atafute mwanamke mwingine wa kuzaa naye. Walishahangaika sana kuzunguka mahospitalini na kwa waganga wa kienyeji bila mafanikio.

Nyumba yao ilikua na amani na Ben alishakubaliana na ile hali, lakini ndugu zake walikua wanasumbua sana, walimtukana mkewe matusi mengi, wakimuambia kula, kulala anawajazia choo, walimnyanyasa sana na Mage hakuwa na raha.

Aliona njia pekee ni kumruhusu mumewe kuoa mwanamke mwingine ili angalau apate mtoto na ndugu zake waache kumsakama. Ben hakuwa tayari kuoa mwanamke mwingine, alikataa katakata lakini mkewe alisisitiza huku akitishia kuondoka kama asingeoa mke mwingine.

Siku moja Ben aliamua kuwaita ndugu zake wote, na wote waliitikaa wito  aliwaambia ana kitu kikubwa cha kuwaambia kwani na yeye alishachoka suala la mtoto na alitaka kufanya mamauzi makubwa. Wakiwa na shauku ya kujua ni nini walifika.

Ben aliwapokea vizuri na baada ya chakula Ben alimuambia mkewe akachukue begi liko kitandani. Ndugu zake walitabasmu wakijua mtoto wao kaamka na sasa anamfukuza mkewe ili atafute mke mwingine na kupata mtoto.

Mkewe alienda kitandani, alichukua begi kubwa na kulileta pale. Ndugu walikaa kimya, Ben alilichukua na kulifungua, lilikua limejaa pesa tu, noti za shilingi elfu kumi  zimepangwa vizuri.

Kila mtu alishangaa na hata mkewe alishangaa. Ben alianza kuongea. “Ndugu zangu nimewaita hapa kwa kuwa  nina tatizo kubwa nyie wote mna watoto Mungu kawabariki hata wewe mdogo wangu hapa ni mjamzito na Mungu akijaalia utajifungua salama.

Lakini mimi na mke wangu Mungu hajatubariki kuwa na  watoto” Alitulia kidogo huku akifuta machozi, yaliyotaka kudondoka. “Sasa nimewaita hapa mnisaidie kitu kimoja tu. Nianze na wewe Mama kwani kila siku umekua ukiniambia kuhusu mjukuu.

Aliongea huku akimgeukia Mma yake. “Chochote mwanangu…” Mama yake aliitikia kwa shauku. “Ninachotaka Mama ni kwamba uniambie ulimpa Mungu shilingi ngapi mpaka akakupa watoto…

Maana mimi nimejaribu imeshindikana, hizi ni hela zote nilizonazo benki na  kesho nitaongea na Dalali ili tuuze nyumba mimi na mke wangu tukapangishe lakini tupate mtoto.”

Alitulia kidogo, watu wote walimshangaa, lakini aliendelea. “Ndugu zangu nisaidieni, nyie mna watoto mlimpa Mungu shilingi ngapi au nini mlitoa, mlimuona wapi mkampelekea, mimi nipo tayari kutoa kila kitu katika maisha yangu ili tu na mimi niitwe Baba na mke wangu aitwe Mama.

Niambieni tu ni bei gani Mungu anapokea?” Wote walinyamaza kimya, hakuna aliyeongea tena, walimuangalia huku wakiangaliana kwa aibu. Hakuna aliyejaribu kunyanyua mdomo.

“Sasa ndugu zangu kama hamjui kiasi ambacho Mungu anapokea ili kutoa watoto basi sitaki kusikia tena hili suala. Mimi na mke wangu tuna furaha, sitaki mtuingilie, siku mkitaja mtoto mje mniambie anauzwa wapi na bei gani nitanunua!

Kama nyie mlinunua au ni wajanja sana mpaka mkampata nifundisheni huo ujanja….Mama…” Alimgeukia Mama yake. “Nakupenda sana lakini mimi sina uwezo wa kujipa mtoto, kama unajua Mungu anataka kiasi gani basi niambie ila kama na wewe hujui basi sitaki umsumbue mke wangu.

Kila siku mnampigia kelele kuwa hazai hazai hivi mnafikiri yeye hataki mtoto, mnafikiri yeye hataki kuitwa Mama, sasa mimi nimemaliza, hizi pesa narudisha ndani siku mkisikia Mungu anauza watoto basi niambieni nitakuja kununua la sivyo mtuache na ndoa yetu..”

Alimaliza kuongea, wote walitoka kimyakimya bila kuongea chochote. Tangu siku hiyo hakukuwa na maneno tena ya mtoto wala nini. Ben na mkewe bado hawajajaaliwa kupata mtoto, wameamua kuasili mtoto yatima na wanaishi naye kama mtoto wao na wote wanafuraha.

***** Imeandikwa Na. Iddi Makengo

Kabla hujamnyanyasa mtu kwa kitu ambacho hana uwezo nacho hembu jiulize wewe ulimpa nini Mungu mpaka akakupa hicho kitu?

 Kwani kuna watu ambao wanadhani kuwa Mungu anawapenda wao zaidi na wao ni bora kuliko wengine.

Monday, May 15, 2017

WANAUME NAO HUNYANYASIKA KIJINSIA MAKAZINI TOFAUTI NA INAVYODHANIWA !

Kama uki google kwa picha ‘Unyanyasaji wa kijinsia makazini’ utashangaa, kwani takribani asilimia 90 ya mapicha picha utakayoyaona yanawaonyesha wanawake wakifanyiwa unyanyasaji wa kijinsia na wanaume.

Lakini ukweli ambao hausemwi ni kwamba wanawake ni wachokozi zaidi ya mara 9 kwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia katika maeneo ya kazi. Najua kuna baadhi ya wanawake wanaweza kutokwa na povu lakini huo ndiyo ukweli wenyewe.

Kwa kawaida unyanyasaji wa kijinsia ni kitendo cha kumchokonoa mtu wa jinsia tofauti au hata jinsia moja kwa kumfanyia vitendo au ishara za kimapenzi kwa nia ya kumtega, kumshawishi au kumlazimisha kufanya naye mapenzi.

Na hii inaweza kufanywa na mtu mwenye madaraka mahali pa kazi dhidi ya walio chini yake au kati ya wafanyakazi wenyewe kwa wenyewe. Na tatizo hili dhidi ya wanaume limekuwa likikua siku hadi siku katika maeneo ya kazi hapa nchini ni vile tu halisemwi kama linavyosemwa pale muathirika anapokuwa ni wa jinsia ya kike.

Wanawake wamekuwa wakijificha kwenye kichaka cha kujiona kama vile wao ndiyo waathirika wakubwa wa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia mahali pa kazi wakati wanaume kwa upande wao wamekuwa wakifanyiwa vitendo vya namna hiyo lakini wamebaki wakiumia ndani kwa ndani kwa sababu hawana pa kusemea.

Ni nani asiyejua kwamba wanawake licha ya kuvaa mavazi yenye kuacha sehemu ya miili yao ya faragha wazi lakini pia mikao yao isiyo ya staha inawaweka baadhi ya wanaume katika wakati mgumu na kushindwa kufanya kazi. Hilo linaweza likaonekana si tatizo, lakini je vipi kuhusu mazungumzo yenye kushawishi ngono yanayofanywa na wananawake au vitendo vya kuwashika wanaume sehemu zao za siri ili kupima maumbile yao, vitendo vya aina hii viitweje kama siyo unyanyasaji wa kijinsia. Je vitendo vya kuwatomasa tomasa wanaume kunakofanywa na baadhi ya wanawake pale wanapoelekezwa kazi au kufundishwa kazi fulani huo siyo unyanyasaji wa kijinsia?

Kuna baadhi ya mabosi wanawake wamekuwa wakiwataka kimapenzi wanaume walio chini yao kwa nguvu na kama wakikataa watakiona cha mtema kuni. Wapo baadhi ya vijana wa kiume wamegeuka kuwa watumwa wa ngono wa mabosi wao na hawathubutu kufanya fyoko maana hatma ya kazi yao imo mikononi mwa hao mabosi wanawake.

Kuna haja sasa ya wanaume kusema sasa basi imetosha na sisi tutafute jukwaa la kusemea madhila yetu maana wenzetu wamejiweka kwenye kundi la waathirika wa vitendo hivyo kumbe na wao wamegeuka Chui ndani ya ngozi ya kondoo.

Kwa hisani ya Mtambuzi
JF

Friday, May 12, 2017

Wednesday, May 10, 2017

KWANINI KHANGA LISIWE VAZI LA TAIFA TANZANIA?


Wakina mama wa Kitanzania wakiwa na vazi la Khanga,kwa mfano kama tukipendekeza vazi la taifa liwe khanga hivi kuna ubaya?

Tuesday, May 9, 2017

BLOGG YA MAISHA NA MAFANIKIO IMEONA HII IWE PICHA YA WIKI...

Nimeiangalia hii picha na kumpongeza huyu mama watoto wanne  na yeye mwenyewe jumla ni watu watano kwa baiskeli moja ....Duh! maisha haya kaaazi kwelikweli...lakini hata  hivyo kilichonifanya niipende picha hii ni nyuso zao wanaonekana wenye furaha na amani pia.....UJUMBE:- UKIWA NA FURAHA PIA AMANI MAISHA HUWA RAHISI KUYAKABILI. KAPULYA WENU.

Sunday, May 7, 2017

HUU NI MSIBA WA TAIFA ULIOTOKEA MEI SITA /POLENI SANA WANAKARATU

KWA PAMOJA WATANZANIA  TUNALIA...KIKUBWA TUWAOMBWA MALAIKA HAWA
PUMZIKENI KWA AMANI  TULIKUWA BADO TUNAWAHITA lakini wote tunapita katika hii dunia . Mmetangulia nasi tutafuta . Pole kwa wazazi/walezi Mwenywzi Mungu awape nguvu kwa kipindi hiki kigumu cha majonzi na maombelezo.

Friday, May 5, 2017

BADO NIPO RUHUWIKO/SONGEA NAKULA VYETU VYA ASILI

ASUBUHI... Karibu chai na maboga
Na baada ya chai na maboga mchana huu karibu tule mahindi ya kuchoma

Wednesday, May 3, 2017

PALE MNGONI ANAPOTAMANI KWAKE RUHUWIKO KULA ALIVYOPANDA

KAZI YA MIKONO YANGU ..NDIZI

Mtoto wa mkulima ni mkulima. Utakula ulichopanda, lakini pia mkulima ni mmoja lakini walaji wengi. leo nimeikumbuka sana migomba yangu  nakula kwa macho tu:-)

Monday, May 1, 2017

TUANZE MWEZI HUU MPYA PIA JUMATATU HII NA HII PICHA

Siku zinakimbia kweli mara hii ni mwezi wa tano...kwa hiyo blog ya Maisha na Mafanikio imeona picha hii iwe mwanzo mzuri wa kuanza wiki pia mwezi.