Showing posts with label jioni. Show all posts
Showing posts with label jioni. Show all posts

Monday, March 11, 2013

KAZI YA MIKONO YANGU:- MLO WA JIONI YA LEO LASAGNE...

 Hapa ni maandalizi :- kwanza ni aina ya mchuzi mweupe ambao nimetengeneza kwa unga wa ngano,maziwa,chumvi pilipili manga na baadaye chizi..halafu unaweka kwenye hicho chumbo kwanza mchuzi huo mweupe, halafu aina ya pasta bapa kidogo na halafu nyama ya kusaga iliyokaangwa na kuungwa na nyanya ya kusaga,kitunguu na kitunguu saumu..unafanya hivyo mara tatu au nne....
 Baada ya hapo naweka ndani ya oven 200°, dakika 30 baada ya hapo tayari kwa kuliwa

Na hapa unaona jinsi sahani ya Kapulya ilikuwa pembeni kuna spenchi, nyanya,na aina ya tango kinywaji machi ambayo yana limao kwa mbali...Chakula hili ni maalum zaidi Italia..Samahani kwa wala waiokula nyama msiogope kuja huwa kuna chakula aina nyingine kwa akiba..kama vile Kamala na Chacha ndio ninaowajua ambao hawali nyama.....JIONI YENU IWE NJEMA NA YENYE AMANI...TWIWONAGE CHILAWO BE..SIJUI NIMEPETIA...:-)

Friday, August 24, 2012

Tuesday, June 19, 2012

JINSI NILIVYOWAZA NINI CHA KUPIKA JIONI YA LEO/NIMETAMANI MBOGA!!!



Nimeiangalia picha hii na kujikuta :-) ebu angalia hayo matembele na naona hapo kwenye hilo kapu kuna zaidi ila nikakaza moyo na kuendelea kuwaza.....

Jioni inaingia nimekaa hapa nawaza nini cha kupika mwanamke mimi...Ghafla natoka nje naangalia bustani . Uwiiiii..bado  bado kabisa. Naingia tena mtandaoni ili kupata mawazo nakutana na picha hii. Kamoyo kanadunda na hamu ya kupa huo mchicha, matembele,chaina ...halafu naangalia akina mama walivyojipanga hapa nami naanza kupata wazo nitawauzia majirani mboga zangu...ujanja eeeh:-)  Picha kutoka kwa Mjengwa.