Ngoja tuendelee na mada hii lakini samahanini imekuwa kinyume.
Wapo watoto wengi wanaozaliwa wakiwa na matatizo mbali mbali, lakini mojawapo nitatizo la mtindio ya ubongo ambalo leo nimeona nilizungumzia kwa undani zaidi.
Matatizo ya mtindio wa ubongo yanatokana au kusababishwa na kizalia (Genetic), dawa alizotumia mama wakati wa ujauzito, matumizi ya madawa ya kulevya, pombe, hali ya hewa, au hata ajali. Mojawapo ya sababu hizo nilizozitaja zinaweza kusababisha kuzaliwa kwa mtoto mwenye mtindio wa ubongo au mtu kupata mtindio wa ubongo.
Nikianza na tatizo la pombe, ni kwamba pombe ina athari kubwa na mbaya kwa akina mama wajawazito. Lipo tatizo linalofahamika kitaalamu kama Fetal Alcoholic Syndrome (FAS) ambalo huwapata watoto ambao wazazi wao walikuwa wanatumia kiwango kikubwa cha pombe wakati wa ujauzito.
Watoto wanozaliwa na tatizo hili wanakuwa na nyuso ambazo sio za kawaida (FacialDeformities), kwa mfano watoto hawa wanweza kuwa na pua bapa na macho yaliyoingia ndani au kuwa na mtindio wa ubongo (Mental Retardations), matatizo ya kusikia na kutokuwa na uwezo wa kusoma.
Kwa hiyo unywaji wa pombe hata kwa kiwango kidogo katika kipindi cha mwezi mmoja hadi mitatu ya mwanzo kwa mama mjamzito huchangia kwa kiasi kikubwa kuzaliwa kwa watoto wenye matatizo haya.
Watot wote wenye matatizo haya ya mtindio wa ubongo wanaweza pia kujifunza kusoma iwapo watapewa msaada maalum na kuandaliwa mazingira mazuri yatakayowashawishi kujifunza kusoma. Malezi kwa watoto wenye matatizo haya, yanatakiwa yawe tofauti na yale ya watoto wa kawaida.
Watoto hawa wanahitaji kuoneshwa upendo, kusikilizwa na mengineyo ya aina hiyo. Hata hivyo swali la msingi tunalopaswa kujiuliza ni kwamba, tutawatambuaje watoto wenye tatizo hili la mtindio wa ubongo wakingali wadogo?
Ukweli ni kwamba ni vigumu sana kwa wazazi kuwatambua watoto wao wenye tatizo hili, kabla watoto hao hawajatimiza umri wa miaka mitatu au minne. Kwa kawaida inashauriwa kwamba mtoto yeyote ambaye anfanya mambo yake pole pole ukilinganisha na watoto wengine wa umri wake, inapaswa kupelekwa haraka hospitalini kwa daktari bingwa wa watoto ili afanyiwe uchunguzi wa kina.
Hata hivyo dalili zifuatazo zinaashiria kuwa mtoto ana tatizo hili Kwanza haoneshi dalili yoyote ya kulia au anaweza kulia kidogo sana. Pili huchelewa sana kutembea na hata kuongea. Tatu haoneshi kuvutiwa nna mazingira yanayomzunguka, kwa maana kwamba hata kama kuna vitu vya kuchezea hawezi kujishughulisha navyo. Nne ni vigumu sana kufundishika na hata kujifunza kusoma huwa ni kazi ngumu ukilinganisha na watoto wa rika lake.
Tano hawezi kula mwenyewe, kuvaa mwenyewe au kujifunza kutumia choo. Hata hivyo zipo dalili nyingi zinazoweza kujitokeza na mara nyingi zinatambuliwa na madaktari maalum wa watoto.
Jinsi wazazi wanavyoweza kuwasaidia watoto wenye tatizo hili:
Watoto wenye mtindio wa ubongo wanafundishika, iwapo tu watafundishwa kwa makini, utulivu na uvumilivu mkubwa, yaani mtu anayemfundisha mtoto wa aina hii hatakiwi kamwe kuwa na hasira, na pia inashauriwa sana kuwapongeza wanapofanya vizuri japo kidogo.
Mwalimu anatakiwa awe mpole na ufundishaji wake usiwe wa haraka haraka, aoneshe mapenzi kwa mtoto, hapaswi kumkemea hata kama anakaosea .
Watoto wa aina hii inashauriwa wapewe nafasi ya kujenga urafiki na watoto wenzao warika lao. Huko nyuma watoto wenye matatizo ya akili walikuwa wantengwa na watoto wenzao katika madarasa, kwa kuwekwa kwenye madarasa maalum.
Lakini siku hizi inashauriwa wachnganywe na wanfunzi wenzao wasio na matatizo ya akili, japo hata kwa nusu siku. Utaratibu huu hujulikana kitaalamu, kama mainstreaming.Itaendelea.....
Showing posts with label ubongo. Show all posts
Showing posts with label ubongo. Show all posts
Friday, May 15, 2009
Thursday, May 14, 2009
WATU WENYE MTINDIO WA UBONGO NAO NI WATU KAMA SISI
Ni watu ambao akili zao zinachelewa kukua. Mtu mzima, mwenye miaka 60 lakini utamwona akili yake ni kama mtoto wa miaka 3. Kwa kweli ni jambo la kusikitisha sana:- Nasema hivi nikiwa na maana nilikuwa nyumbani TZ. Niliwahi kuona watu wengi wenye watoto wenye mtindio wa ubongo walikuwa wakiwaficha ndani ya nyumba kwa kuona aibu.
Baadaya ya kuishi hapa kwa muda huu nilioishi, nimefanya utafiti na kugundua ya kwamba sisi waAfrika/waTanzania. Kila kitu tufanyacho tupo nyuma yaani tunafanya baada ya wenzetu/Ughaibuni kupiga hatua mbele. Nasi tunafuata nyuma. Ni hivi katika utafiti wangu wao/Ughaibuni pia hapo zamani walikuwa wakipata mtoto mwenye mtindio wa ubongo waliona aibu na hawakumtaka yule mtoto. Walimpeleke kwenye nyumba maalumu. nyumba ya watoto "YATIMA". Ilikuwa ni kinyume na Afrika/TZ wao waliwatunza wenyewe ila hawakutaka waonekane.
Lakini sasa hapa niishipo wenye mtindio wa ubongo wote wanaruhusiwa kufanya chochote kile kutegemea na ulemavu gani anao. Wanaruhusiwa kwenda shule, yaani shule maalumu, wanafanya kazi kulingana na uwezo wao, wanaishi kwenye ghorofani "peke yao" huku wakisaidiwa na wafanyakazi yale mahitaji muhimu. Wamekuwa ni watu wa "kawaida" katika jumuia.
Tanzania pia wamefikia hatua kubwa kidogo ukilinganisha na miaka ya 1980. Kuanzia miaka ya 1990 kulikuwa/kumekuwa na shule ya wenye mtindio wa ubongo. Ila sasa tatizo ni kwamba wakishamaliza pale wanawaacha tu. Hakuna anayewajali watu hawa. Kwa mtazamo wangu naona wao wanaumuhimu wa mahitaji kama sisi wengine. Kwa sababu hawa hawahitaji kazi ya maana sana. Kinachotakiwa ni vijikazi vidogovidogo. Yaani kuwepo na sehemu (nyumba/jengo) ili wawe wanaenda kufanya kazi hata masaa mawili kuliko kuwaacha tu. TUSISAHAU YA KUWA BINADAMU WOTE NI SAWA!!!!
Baadaya ya kuishi hapa kwa muda huu nilioishi, nimefanya utafiti na kugundua ya kwamba sisi waAfrika/waTanzania. Kila kitu tufanyacho tupo nyuma yaani tunafanya baada ya wenzetu/Ughaibuni kupiga hatua mbele. Nasi tunafuata nyuma. Ni hivi katika utafiti wangu wao/Ughaibuni pia hapo zamani walikuwa wakipata mtoto mwenye mtindio wa ubongo waliona aibu na hawakumtaka yule mtoto. Walimpeleke kwenye nyumba maalumu. nyumba ya watoto "YATIMA". Ilikuwa ni kinyume na Afrika/TZ wao waliwatunza wenyewe ila hawakutaka waonekane.
Lakini sasa hapa niishipo wenye mtindio wa ubongo wote wanaruhusiwa kufanya chochote kile kutegemea na ulemavu gani anao. Wanaruhusiwa kwenda shule, yaani shule maalumu, wanafanya kazi kulingana na uwezo wao, wanaishi kwenye ghorofani "peke yao" huku wakisaidiwa na wafanyakazi yale mahitaji muhimu. Wamekuwa ni watu wa "kawaida" katika jumuia.
Tanzania pia wamefikia hatua kubwa kidogo ukilinganisha na miaka ya 1980. Kuanzia miaka ya 1990 kulikuwa/kumekuwa na shule ya wenye mtindio wa ubongo. Ila sasa tatizo ni kwamba wakishamaliza pale wanawaacha tu. Hakuna anayewajali watu hawa. Kwa mtazamo wangu naona wao wanaumuhimu wa mahitaji kama sisi wengine. Kwa sababu hawa hawahitaji kazi ya maana sana. Kinachotakiwa ni vijikazi vidogovidogo. Yaani kuwepo na sehemu (nyumba/jengo) ili wawe wanaenda kufanya kazi hata masaa mawili kuliko kuwaacha tu. TUSISAHAU YA KUWA BINADAMU WOTE NI SAWA!!!!
Subscribe to:
Posts (Atom)