......Furaha inakuwa ni ya ajabu...hapa ni mwalimu mtaafu Eusebius Mlelwa na mwal. Klaesson walikuwa wanafanya kazi pamoja Wilima Secondary hapa walikutana mwaka huu mjini Songea. Hapa ni stendi kuu ya Songea
Sio wao tu walipata bahati ya kuonana ..la hasha Yasinta/kapulya naye alionana na rafiki yake ambaye walisoma chuo pamoja ni Pendo Mapunda. Nilifurahi sana kuonana na Penda miaka mingi tulipoteana. Hapa ni Lizabon Songea.....Raha eeeehhhh....
Showing posts with label raha. Show all posts
Showing posts with label raha. Show all posts
Tuesday, February 26, 2013
Saturday, July 28, 2012
NDIYO NIPO NANYI ...JUMAMOSI NJEMA WANDUGU,,,!!!
Likizo hii nimeona niwe hapa hapa si kwenda mbali sana kwa hiyo hizi siku nilizopotea nilikuwa hapa summer house ni mahali pazuri kwa kupumzika na kutafakari...wavuvi hao wanakwenda kutafuta kitoweo baba na kijana wake.....
...ila inakuja wakati lazima kurudi kuvuna mavuno hapa ni mboga za maboga, Bei rahisi fungu moja mia,,,:-)
Hapa ni ni sehemu ambayo watu wengi wanapenda kwenda na watoto wao au wao tu kufurahi. Ni Skandinavian sehemu kubwa ya "water land" SKARA SOMMAR LAND.
..Bado tulikuwa kule ilikuwa ALHASMIS ..baba na kamanda wake wakiendesha magari kama kucheza----
NAWAKUMBUKENI SANA NA TUPO PAMOJA,,,,KILA LA KHERI!!!!
Saturday, July 21, 2012
KATIKA MAISHA KUPUMZIKA NI MUHIMU/RAHA JIPE MWENYEWE!!!!
Unapokuwa na mapumziko ya siku mbili tatu hivi kabla hujapata likizo kamili basi unakimbia na kujificha hapa (SUMMER HOUSE/SOMMARSTUGA). Mahali ambapo unaweza kupumzika tu hakuna eti ngoja niangalia mtandaoni kuna nini HAKUNA.
Na ukitokwa na jasho au ukijisikia uchovu basi ni kujitupa tu majini huna haja ya kwenda mbali kutafuta maji.......
Ila kula ni muhimu ..akina mama wapo jikoni, na hapo ni mzee wa nyumba na pia ni raha kufikiwa na wageni aliyevaa kofia ni mgeni wetu mzee Masawe.......
...Wanapofika wageni ni raha kwani siku hii nilipata zawadi ambayo nilikuwa naitamani siku nyingiiiiii:-) Hiyo hapo juu UTAMADUNI !!!
Tunapojisikia hamu ya samaki basi ni kuchukua boti na kwenda kujaribu...wavuvi wadogo haoooo wanakwenda kutafuta kitoweo....
Baada ya muda wanarudi mikono mitupu hakuna kitoweo...hivi ndivyo ilivyokuwa siku mbili/tatu nilipokuwa kimya...NAWATAKIENI WOTE JUMAMOSI NJEMA.....KAPULYA:-)
Friday, January 20, 2012
PICHA ZILIZOCHAGULIWA NA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO KUWA PICHA ZA WIKI!!
Sunday, July 25, 2010
Barua fupi kwa wasomaji wa blog ya Maisha na Mafanikio!!
Nina furaha kuandika waraka huu na kuwataarifu ya kwamba nitakuwa nimeadimika adimika. Katika ulimwengu huu kila mtu anahihitaji mapunziko. Kwa hiyo mama Maisha na Mafanikio amepata liki kikazi na atakuwa likizo akiambatana na familia yake.
Na nimeona ni vema niwaage nitajaribu kupitapita pale nipatapo wasaa. Nawatakieni wote kila la kheri kwa lolotw mtakalotenda na tukutane panapo majaliwa.
TUTAONANA BAADA YA MUDA SI MREFU....KAPULYA aka Yasinta na pia NAWATAKIENI JUMAPILI NJEMA !!!
Thursday, May 20, 2010
Ujumbe/kichekesho au sijui kucheza na lugha
Mmasai kaingia hotelini akaagiza chai na mkate. Alipomaliza kunywa akataka ankara (bill) yake. Alipopewa akakuta imeandikwa, Chai shilingi 300 na mkate shiling 200 jumla ikawa shilingi 500. Mmasai akalipa shiling 200, alipoambiwa hela haitoshi, akajibu...ero mimi nalipa mukate na mukate italipa shai. Kwa sababu mimi nakula mukate na mukate nakunywa shai. Akiwa na maana kwamba alikuwa akichovyo mkate kwenye chai na kula kwa hiyo hakunywa chai bali mkate ndio uliokunywa chai......Hii nimetumiwa na rafiki nimecheka sana nikaona tucheke pamoja
Wednesday, February 10, 2010
Karibuni Wote Kikombe Hiki Cha Chai!!!!!
Our Love Warms my Heart.
Najua wote mnajua mie ni mpenzi sana wa chai tena ile isiyo na sukari(Chingambu) :-).
Friday, December 4, 2009
Hongera wajina wangu kwa siku ya kuzaliwa:- Yasinta
Friday, October 9, 2009
NAPENDA KUWATAKIA WOTE MWISHO WA JUMA NA MUSIKI HUU HAYA TUFURAHI PAMOJA
UJUMBE WA LEO:- UKITAKA KUJUA MENGI BASI ULIZA (FRÅGA OM DU VILL VETA MERA)
Thursday, September 17, 2009
MZIKI NI MOJA YA MAISHA NGOJA TUMSIKILIZA DADA LADY JAY DEE- NATAMANI KUWA MALAIKA
Dada Jay Dee hata mimi natamani kuwa malaika tu nimeupenda kweli wimbo huu mpaka nimeona niuweka hapa. Ahsante sana. Nadhani siku moja tutakuwa ru malaika.
Sunday, September 13, 2009
NAWATAKIENI JUMAPILI NJEMA KWA MLO HUU MTAMU WA NDIZI.
.jpg)
VIPIMO
Ndizi Mbivu 6
Nazi Kikopo 1
Sukari Vijiko 3 vya chakula
Hiliki Kijiko 1
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
1) Menya ndizi kisha zipasue kati utoe ule moyo wa kati.
2) Zikate size unayopenda mwenyewe, kisha uzipange ndani ya sufuria.
3) Weka maji kiasi na uzichemshe ndizi kidogo, karibu ya kuiva mimina tui.
4) Mimina sukari na hiliki ndani ya ndizi na ziwache zichemke mpaka tui libaki kidogo.
5) Ziondoe jikoni na uziweke kwenye sahani tayari kwa kuliwa. Huu ni mlo wangu wa leo karibuni.
KIDOKEZO:
Ni nzuri sana kuliwa na kitu cha chumvi kama nyama ya kukausha au kuku wa kuchoma.
Ndizi Mbivu 6
Nazi Kikopo 1
Sukari Vijiko 3 vya chakula
Hiliki Kijiko 1
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
1) Menya ndizi kisha zipasue kati utoe ule moyo wa kati.
2) Zikate size unayopenda mwenyewe, kisha uzipange ndani ya sufuria.
3) Weka maji kiasi na uzichemshe ndizi kidogo, karibu ya kuiva mimina tui.
4) Mimina sukari na hiliki ndani ya ndizi na ziwache zichemke mpaka tui libaki kidogo.
5) Ziondoe jikoni na uziweke kwenye sahani tayari kwa kuliwa. Huu ni mlo wangu wa leo karibuni.
KIDOKEZO:
Ni nzuri sana kuliwa na kitu cha chumvi kama nyama ya kukausha au kuku wa kuchoma.
Sunday, September 6, 2009
Thursday, July 30, 2009
Salamu wanablog I
Nimelipenda shairi hili na nimepewa idhini toka kwa aliyeandika Kaka Fadhy Mtanga kuwa niliweka hapa kwangu.
Nashika kalamu yangu, salamu nazituma,
Kwenu marafiki zangu, natumai mu wazima,
Nawaombea kwa Mungu, mjaliwe yalo mema,
Salamu wanablog.
Simon Kitururu, huzamia MAWAZONI,
Fikra zake ni huru, pia zina burudani,
Nasi tunamshukuru, hachoki tangu zamani,
Salamu wanablog.
Yupo dadetu Yasinta, yeye hupenda MAISHA,
Kamwe hawezi kusita, mazuri kutuonesha,
Sifa tele azipata, maana huelimisha,
Salamu wanablog.
Christian Bwaya yupo, hutaka tuJIELEWE,
Daima aandikapo, vichwa vyetu tusuguwe,
Ukweli daima upo, muhimu ujadiliwe,
Salamu wanablog.
Mubelwa Bandio pia, MZEE WA CHANGAMOTO,
Haishi kutuambia, mambo yalo motomoto,
Muziki hutupatia, yenye midundo mizito,
Salamu wanablog.
Subi dada yetu sote, wa NUKTA SABA SABA,
Ili mengi tuyapate, blog yake yashiba,
Asichoke asisite, ajaze hata kibaba,
Salamu wanablog.
Chib naye ni rafiki, hutumia HADUBINI,
Kazi yake haichoki, popote ulimwenguni,
Magharibi mashariki, hutujuza kulikoni,
Salamu wanablog.
MWANAMALENGA Kissima, hutuonesha MWANGAZA,
Makala zenye hekima, na mambo kuyachunguza,
Kwa ushairi ni vema, tungo zake zapendeza,
Salamu wanablog.
Serina Serina huyo, ana UPANDE MWINGINE,
Yale ayaandikayo, hupendwa nao wengine,
Kwa mawazo si mchoyo, hufanya tushikamane,
Salamu wanablog.
Koero Mkundi pia, hutuambia VUKANI,
Hachoki kutuletea, yatokeayo nchini,
Daima hukumbushia, tutoke usingizini,
Salamu wanablog.
Ndugu yetu Mumyhery, kabobea kwa MAVAZI,
Vitu vyake ni vizuri, hilo mbona lipo wazi,
Yupo kwenye mstari, hachoki kufanya kazi,
Salamu wanablog.
Kamala tunamjua, wa nyegerage KIJIWENI,
Fikra apambanua, ili tutoke kizani,
Sote tukajitambua, tujijue kina nani,
Salamu wanablog.
Masangu wa Nzunzullima, CHAKULA chake KITAMU,
Hatosahau daima, kutupa yote muhimu,
Ujuzi wake kisima, haisaliti elimu,
Salamu wanablog.
Markus Mpangala, KARIBUNI sana NYASA,
Yeye wala hajalala, mengi ameshayaasa,
Kabobea mijadala, ya jamii na siasa,
Salamu wanablog.
Lumadede mshairi, USHAIRI MAMBOLEO,
Mashairiye mazuri, tena yale ya kileo,
Huukuza ushairi, na kuupa mwelekeo,
Salamu wanablog.
Na MWANASOSHOLOJIA, siachi kumsifia,
Elimu kutugawia, na picha kutuwekea,
Mazuri hutuambia, ndani ya hii dunia,
Salamu wanablog.
Nami MWANANCHI MIMI, wa DIWANI YA FADHILI,
Tungo zangu siwanyimi, nawapenda kiukweli,
Tena mara kumi kumi, tena na kwa kila hali,
Salamu wanablog.
Ambao sijawataja, lipo shairi jingine,
Sote tungali pamoja, kwa mema tuombeane,
Tusichoke zetu hoja, hivyo na tushikamane,
Salamu wanablog.
Nashika kalamu yangu, salamu nazituma,
Kwenu marafiki zangu, natumai mu wazima,
Nawaombea kwa Mungu, mjaliwe yalo mema,
Salamu wanablog.
Simon Kitururu, huzamia MAWAZONI,
Fikra zake ni huru, pia zina burudani,
Nasi tunamshukuru, hachoki tangu zamani,
Salamu wanablog.
Yupo dadetu Yasinta, yeye hupenda MAISHA,
Kamwe hawezi kusita, mazuri kutuonesha,
Sifa tele azipata, maana huelimisha,
Salamu wanablog.
Christian Bwaya yupo, hutaka tuJIELEWE,
Daima aandikapo, vichwa vyetu tusuguwe,
Ukweli daima upo, muhimu ujadiliwe,
Salamu wanablog.
Mubelwa Bandio pia, MZEE WA CHANGAMOTO,
Haishi kutuambia, mambo yalo motomoto,
Muziki hutupatia, yenye midundo mizito,
Salamu wanablog.
Subi dada yetu sote, wa NUKTA SABA SABA,
Ili mengi tuyapate, blog yake yashiba,
Asichoke asisite, ajaze hata kibaba,
Salamu wanablog.
Chib naye ni rafiki, hutumia HADUBINI,
Kazi yake haichoki, popote ulimwenguni,
Magharibi mashariki, hutujuza kulikoni,
Salamu wanablog.
MWANAMALENGA Kissima, hutuonesha MWANGAZA,
Makala zenye hekima, na mambo kuyachunguza,
Kwa ushairi ni vema, tungo zake zapendeza,
Salamu wanablog.
Serina Serina huyo, ana UPANDE MWINGINE,
Yale ayaandikayo, hupendwa nao wengine,
Kwa mawazo si mchoyo, hufanya tushikamane,
Salamu wanablog.
Koero Mkundi pia, hutuambia VUKANI,
Hachoki kutuletea, yatokeayo nchini,
Daima hukumbushia, tutoke usingizini,
Salamu wanablog.
Ndugu yetu Mumyhery, kabobea kwa MAVAZI,
Vitu vyake ni vizuri, hilo mbona lipo wazi,
Yupo kwenye mstari, hachoki kufanya kazi,
Salamu wanablog.
Kamala tunamjua, wa nyegerage KIJIWENI,
Fikra apambanua, ili tutoke kizani,
Sote tukajitambua, tujijue kina nani,
Salamu wanablog.
Masangu wa Nzunzullima, CHAKULA chake KITAMU,
Hatosahau daima, kutupa yote muhimu,
Ujuzi wake kisima, haisaliti elimu,
Salamu wanablog.
Markus Mpangala, KARIBUNI sana NYASA,
Yeye wala hajalala, mengi ameshayaasa,
Kabobea mijadala, ya jamii na siasa,
Salamu wanablog.
Lumadede mshairi, USHAIRI MAMBOLEO,
Mashairiye mazuri, tena yale ya kileo,
Huukuza ushairi, na kuupa mwelekeo,
Salamu wanablog.
Na MWANASOSHOLOJIA, siachi kumsifia,
Elimu kutugawia, na picha kutuwekea,
Mazuri hutuambia, ndani ya hii dunia,
Salamu wanablog.
Nami MWANANCHI MIMI, wa DIWANI YA FADHILI,
Tungo zangu siwanyimi, nawapenda kiukweli,
Tena mara kumi kumi, tena na kwa kila hali,
Salamu wanablog.
Ambao sijawataja, lipo shairi jingine,
Sote tungali pamoja, kwa mema tuombeane,
Tusichoke zetu hoja, hivyo na tushikamane,
Salamu wanablog.
Monday, July 13, 2009
Saturday, June 27, 2009
Tuesday, June 2, 2009
KISWAHILI
Mara nyingi huwa nakasirishwa kuona / kusikia watu wanatumia vibaya baadhi ya maneno ya kiswahili. Hapa nimechukua au nataka kutoa mfano haya maneno matatu. Karibu, Jambo na Habari
Karibu: Ni kuto kuwa mbali kwa wakati au mahali, kiasi cha kukadria. Lakini watu wengi wanaelewa zaidi karibu ni tamko litumikalo kuitikia hodi au wakati mtu anapokaribishwa au kupokewa mahali fulani.
Jambo: Watalii wengi wanafikiri wanaweza kiswahili, kusalimia wasemapo jambo hawajui kwamba Kiswahili sananifu hutamkwa hujambo/haujambo/hamjambo? kwani ukisema hivi anashindwa kuitikia sijambo. Si afadhali hata wangefundishwa kusema hali yako.....
Habari: Neno habari limekuwa linanitatanisha sana. Kama kawaida maneno mengi ya kiswahili yana maana mbili azu zaidi. (1) Habari ni melezo ya jambo fulani lililotokea, taarifa, ujumbe na ripoti.
2) Habari hutumika katika kuamkiana na kuulizana hali. Lakini inaonekena wengi hatuwazi sana tunapoongea hili neno litumikeje.
Karibu: Ni kuto kuwa mbali kwa wakati au mahali, kiasi cha kukadria. Lakini watu wengi wanaelewa zaidi karibu ni tamko litumikalo kuitikia hodi au wakati mtu anapokaribishwa au kupokewa mahali fulani.
Jambo: Watalii wengi wanafikiri wanaweza kiswahili, kusalimia wasemapo jambo hawajui kwamba Kiswahili sananifu hutamkwa hujambo/haujambo/hamjambo? kwani ukisema hivi anashindwa kuitikia sijambo. Si afadhali hata wangefundishwa kusema hali yako.....
Habari: Neno habari limekuwa linanitatanisha sana. Kama kawaida maneno mengi ya kiswahili yana maana mbili azu zaidi. (1) Habari ni melezo ya jambo fulani lililotokea, taarifa, ujumbe na ripoti.
2) Habari hutumika katika kuamkiana na kuulizana hali. Lakini inaonekena wengi hatuwazi sana tunapoongea hili neno litumikeje.
Wednesday, April 15, 2009
MGANDA+BURUDANI/UTAMADUNI=MAISHA
Tuesday, March 31, 2009
Sunday, March 29, 2009
Sunday, March 15, 2009
KARIBUNI CHAI BORA+JUMAPILI NJEMA

Ukitaka kukosana nami basi ninyime chai, tena bila sukari hapo tutakosana sana. Kama wasemavyo wakati wowote ni wakati wa chai.
lebo:
burudani afrika,
chai,
kinywaji,
Kumbukumbu,
raha,
tanzania
Subscribe to:
Posts (Atom)





