Showing posts with label penda. Show all posts
Showing posts with label penda. Show all posts

Tuesday, April 17, 2012

MAISHA: NAIPENDA MIKOBA YANGU NA NAZIPENDA SKAFU/SHALI ZANGU!!!

HAPA NI BAADHI YA MIKOBA NIIPENDAYO
HAPA NI BAADHI YA MIKOBA YANGU

NA HAPA NI SKAFU ZANGU
NA HAPA NI SKAFU ZANG
Katika maisha sisi binadamu tupo tofauti kwa kila namna. Tukianzia tabia, sura, mwili, kupenda nk. Leo napenda kuzungumzia neno KUPENDA/TAMAA. Lakini si kule kupenda kwa kimapenzi hapana ni kupenda kwa kupenda vitu au kupenda kununua vitu hata kama anavyo vya kutosha:- Yaani utakuta mtu anapenda kikombe chake cha chai kweli kiasi kwamba mwingine akikigusa ni balaa. Mwingine anapenda kweli shati moja tu ambalo anaweza kulivaa kila siku utazani hana lingine. Mwingine akawa anapenda sweta kiasi kwamba hata kulifua anasahau. Halafu kuna hawa wanaonununua viatu, utakuta mtu ana pea za viatu chumba kizima huwa nashangaa sana je atavivaa lini? lakini hii yote ni basi tu yaani tamaa . Na kuna wanaokusanya/nunua vitabu. Kwa hiyo leo nataka kuwaambia mimi ni MDHAIFU SANA wa SKAFU/SHALIna MIKOBA. Hapo juu ni zaidi ya ishirini na bado natamani zaidi kwani nataka niwenazo rangi zote. NAPENDA SANA SKAFU.....NA PIA MIKOBA Swali je wewe ni mpenzi/mkusanyaji wa nini?

Thursday, March 17, 2011

MAISHA: NAZIPENDA SKAFU/SHALI ZANGU!!!

SKAFU ZANGU
Katika maisha sisi binadamu tupo tofauti kwa kila namna. Tukianzia tabia, sura, mwili, kupenda nk. Leo napenda kuzungumzia neno KUPENDA/TAMAA. Lakini si kule kupenda kwa kimapenzi hapana ni kupenda kwa kupenda vitu au kupenda kununua vitu hata kama anavyo vya kutosha:- Yaani utakuta mtu anapenda kikombe chake cha chai kweli kiasi kwamba mwingine akikigusa ni balaa. Mwingine anapenda kweli shati moja tu ambalo anaweza kulivaa kila siku utazani hana lingine. Mwingine akawa anapenda sweta kiasi kwamba hata kulifua anasahau. Halafu kuna hawa wanaonununua viatu, utakuta mtu ana pea za viatu chumba kizima huwa nashangaa sana je atavivaa lini? lakini hii yote ni basi tu yaani tamaa . Kwa hiyoleo nataka kuwaambia mimi ni MDHAIFU SANA wa SKAFU/SHALI. Hapo juu ni zaidi ya ishirini na bado natamani zaidi kwani nataka niwenazo rangi zote. NAPENDA SANA SKAFU.....Swali je wewe ni mpenzi/mkusanyaji wa nini?

Wednesday, November 12, 2008

WENGI WANASEMA HIZI NI RANGI ZA WANARASTA




Je? ni kweli ni rangi za wanarasta kwani binafsi pia ni rangi zangu. Nisaidieni basi.Kazi kweli kweli.