HAPA NI BAADHI YA MIKOBA NIIPENDAYO
HAPA NI BAADHI YA MIKOBA YANGU
NA HAPA NI SKAFU ZANGU
NA HAPA NI SKAFU ZANG
Katika maisha sisi binadamu tupo tofauti kwa kila namna. Tukianzia tabia, sura, mwili, kupenda nk. Leo napenda kuzungumzia neno KUPENDA/TAMAA. Lakini si kule kupenda kwa kimapenzi hapana ni kupenda kwa kupenda vitu au kupenda kununua vitu hata kama anavyo vya kutosha:- Yaani utakuta mtu anapenda kikombe chake cha chai kweli kiasi kwamba mwingine akikigusa ni balaa. Mwingine anapenda kweli shati moja tu ambalo anaweza kulivaa kila siku utazani hana lingine. Mwingine akawa anapenda sweta kiasi kwamba hata kulifua anasahau. Halafu kuna hawa wanaonununua viatu, utakuta mtu ana pea za viatu chumba kizima huwa nashangaa sana je atavivaa lini? lakini hii yote ni basi tu yaani tamaa . Na kuna wanaokusanya/nunua vitabu. Kwa hiyo leo nataka kuwaambia mimi ni MDHAIFU SANA wa SKAFU/SHALIna MIKOBA. Hapo juu ni zaidi ya ishirini na bado natamani zaidi kwani nataka niwenazo rangi zote. NAPENDA SANA SKAFU.....NA PIA MIKOBA Swali je wewe ni mpenzi/mkusanyaji wa nini?
