Mwalimu aliingia katika darasa moja huko Iringa Vijijini na kuuliza wanafunzi wake. "Nani atanipa jibu la wingi wa Chumvi?" Mwanafunzi mmoja kwa kujiamini akasimama na kujibu, "Fyuvi!" Duh, kasheshe hiyo.....!
Showing posts with label kichekesho. Show all posts
Showing posts with label kichekesho. Show all posts
Wednesday, May 18, 2016
Wednesday, September 23, 2015
HEBU LEO TUANGALIE KICHEKESHO HIKI CHA MZARAMO V/S MCHAGA...KARIBU
Mzaramo alitangaza anatibu magonjwa yooooooote kwa tsh. 100,000/=
Na kama akishindwa kukutibu anakurudishia laki
yako nakukuongeza laki nyingine.
Na kama akishindwa kukutibu anakurudishia laki
yako nakukuongeza laki nyingine.
MCHAGA akaona hii fursa yakujipatia hela aiwezi mpita akaenda kutibiwa.
MZARAMO: "unaumwa nini?"
MCHAGA: "Sisikii ladha ya aina yoyote mdomoni kabisaaaa.."
MZARAMO: "sawa, toa laki kabisa.."
Mchaga akatoa.
Mchaga akatoa.
MZARAMO akamuagiza msaidizi wake; "Naomba kikopo no.27 mpe anywe huyu.."
MCHAGA akanywa akatema faster; "Puh puu puu, Aisee huu si mkojo huu..?"
MZARAMO: "Umepona karibu tena.."
Mchaga aka-mind sana Kesho yake akarudi tena hakuamini ameliwa pesa yake.
MCHAGA: aisee nina tatizo la kumbukumbu nasahau
sanaaaaa.."
sanaaaaa.."
MZARAMO akamwambia "hakuna tabu, toa laki tukupe tiba..'
MCHAGA akatoa pesa akijua leo lazima afanikiwe..'
MZARAMO: "nesi naomba kikopo no.27.."
MCHAGA: "ASA CHALII ANGU HICHO SI CHA JANA CHA MKOJO HICHO AISEE..?"
MZARAMO: "UMEPONA KUMBUKUMBU UNAYO.
PANAPO MAJARIWA TUTAONANA TENA!
Wednesday, March 25, 2015
UTANI KIDOGO- MLEVI NA MCHUNGAJI WAMEKUTANA!!
Ungana nami na utani huu nimeona si vizuri kupata elimu hii peke yangu ...nimetumiwa na msomaji wa Maisha na Mafanikio. KARIBU.....
MCHUNGAJI; "Unakunywa bia!?
MLEVI; "Ndio.
MCHUNGAJI; "Kwa siku
unakunywa bia ngapi!?
MLEVI; "Nakunywa bia tano!
MCHUNGAJI; "Bia moja bei
gani!?
MLEVU; "2500/
MCHUNGAJI; "Ulianza lini
kunywa bia!?
MLEVI; "Miaka 18
iliyopita!
MCHUNGAJI; "Kwa hiyo kwa
siku unatumia zaidi ya 10,000??
MLEVI; "Ndio!
MCHUNGAJI; "Kama u gekuwa
unatunza hiyo pesa 10,000 kwa siku leo hii si ungekuwa na Range
Rover!?
MLEVI; "Samahani, naweza
kukuuliza swali!?
MCHUNGAJI; "Uliza!
MLEVI; "Unakunywa bia!?
MCHUNGAJI; "Hapana!
MLEVI; "Nionyeshe Range
Rover yako!
MCHUNGAJI; "Akakimbia..... |
Monday, March 17, 2014
EBU JUMATATU HII YA LEO TUANZE NA MSEMA HUU CHEKA UNENEPE:- VICHEKESHO VYETU!!
Katika kuhakikisha wanafunzi wa darasa la kwanza wanaelewa, mara nyingi walimu hutumia mifano mingi sana, nakumbuka baba yangu alivyokuwa akitupatia mifano mingi ili tuelewe...haya fuatana nami na mahojiano yafuatayo ambayo mwalimu alikuwa anajitahidi kuwaelewesha wanafunzi wake:-
Mwalimu:- Nikikupa chapati sita halafu ukala mbili zitabaki chapati Ngapi?
Mwanafunzi:- Ukinipa na chai ya maziwa haitabaki hata chapati moja.
HAYA NIKUTAKIE JUMATATU NJEMA SANA NA PANAPO MAJALIWA TUTACHEKA TENA JUMATATU IJAYO:-)
Mwalimu:- Nikikupa chapati sita halafu ukala mbili zitabaki chapati Ngapi?
Mwanafunzi:- Ukinipa na chai ya maziwa haitabaki hata chapati moja.
HAYA NIKUTAKIE JUMATATU NJEMA SANA NA PANAPO MAJALIWA TUTACHEKA TENA JUMATATU IJAYO:-)
Wednesday, October 24, 2012
HIVI LINI UMECHEKA AU KUTABASAMU BASI UNGANA LEO NAMI KUHUSU HILI: Maongezi ya Mtoto na Baba'ke
Baba: We mtoto hebu niletee soda...
Mtoto: Cola au Pepsi?
Baba: Pepsi.
Mtoto: Kopo au Chupa?
Baba: Kopo.
Mtoto: Baridi au moto?
Baba: Baridi.
Mtoto: Ndogo au Bonge?
Baba: Aaa! Basi niletee tu maji.
Mtoto: Ya bombani au dukani?
Baba: We mtoto nitakupiga?
Mtoto: Na mti au chelewa?
Baba: N'takuua nakwambia!
Mtoto: Kwa kudu au bunduki?
Baba: Bunduki.
Mtoto: Kichwani au kifuani?
Baba: Mbaff, toka nje!
Mtoto: Sasa hivi au baadaye?
Baba: Sasa hivi.
Mtoto: Kwa hiyo maji hutaki tena?
Baba: (kimoyomoyo) "nilimwambia mke wangu tukilewa tusifanye, yeye anang'ang'ania, haya ndiyo matokeo yake..."
Source: http://www.wavuti.com
Mtoto: Cola au Pepsi?
Baba: Pepsi.
Mtoto: Kopo au Chupa?
Baba: Kopo.
Mtoto: Baridi au moto?
Baba: Baridi.
Mtoto: Ndogo au Bonge?
Baba: Aaa! Basi niletee tu maji.
Mtoto: Ya bombani au dukani?
Baba: We mtoto nitakupiga?
Mtoto: Na mti au chelewa?
Baba: N'takuua nakwambia!
Mtoto: Kwa kudu au bunduki?
Baba: Bunduki.
Mtoto: Kichwani au kifuani?
Baba: Mbaff, toka nje!
Mtoto: Sasa hivi au baadaye?
Baba: Sasa hivi.
Mtoto: Kwa hiyo maji hutaki tena?
Baba: (kimoyomoyo) "nilimwambia mke wangu tukilewa tusifanye, yeye anang'ang'ania, haya ndiyo matokeo yake..."
Source: http://www.wavuti.com
Sunday, April 3, 2011
HEBU SIKILIZA HAPA JINSI WALIVYOJUA KUIGIZA...KAAZI KWELIKWELI
Muda mrefu nimekuwa mkimya bila kusikiliza miziki kwa ajiliya machungu yaliyonipata katika upekuzi wangu nimekutana nao hau kwa kweli wamenifanya nitabasamu kiduchu.. sijui nanyi wenzangu mtajiunga nami???
Subscribe to:
Posts (Atom)
