Kuna simulizi nyingi sana ninazipata kutoka huko nyumbani Tanzania ambazo huwa zinanishangaza sana. Awali ilikuwa ni wanawake ndio waliokuwa waathirika lakini sasa hivi na wanaume nao inasemekana wameingia katika mkumbo huo mpaka najiuliza, sababau ni nini hasa. Je ni uelewa mdogo au ndio athari za utandawazi zinawaathiri ndugu zangu?
Kuna wanawake wengi wamekuwa ni wahanga wa madawa ya Kichina ya kuongeza makalio, kiasi kwamba wengine wamepoteza maisha. Ni jambo la kushangaza kidogo kuona kwamba serikali yetu imeshindwa kusimamia na kudhibiti uingizwaji wa haya madawa ya kichina yenye athari lukuki kwa binadamu mpaka pale zinapotokea athari za wazi.
Haya, sasa mambo yamegeuka, wanaume nao wameingia kwenye mkumbo huo. Hivi karibuni kuna habari zimesambaa huko nyumbani kuwa kuna mwanaume mmoja amejikuta akiwa na maumbile ya sehemu zake za siri makubwa kupita kiasi, inasemekana hata mkewe amemkimbia. Kisa, alitumia dawa za kichina za kukuza maumbili ya wanaume.
Habari zaidi zinadai kuwa mkewe alikuwa anatoka nje ya ndoa sana na baada ya mume huyo kumuuliza mkewe sababu ta kutoka nje ya ndoa ndio akajibiwa kuwa ana maumbile madogo na ndio maana akaona akatafute dawa za kichina ili akuze maumbile yake kumridhisha mkewe. Lakini kinyume na matarajio yake, maumbile yake yakawa makubwa kupindukia, hata mkewe akamkimbia.
Kuna wakati niliwahi kuandika juu ya wanaume kununua dawa za kuongeza nguvu za kiume maarufu kama mkuyati, kama ukitaka kujikumbusha bofya hapa. Nakumbuka nilipata upinzani mkubwa kutoka kwa wanaume, lakini naamini kwa hili watakubaliana na mimi.
Kwangu mimi wale wanawake wenzangu wanaokimbilia dawa za kichina ili kuongeza makalio yao na wale wanaume wanaotumia dawa za kuongeza nguvu za kiume maarufu kama mkuyati na dawa za kichina ili kuongeza maumbile yao nawaona kama watu wasiojiamini.
Mara nyingi tunapozungumziwa matatizo katika ufanyaji wa tendo la ndoa huwa tunafikiria matatizo ya ufanyaji kazi wa viungo vyetu tunavyotumia katika kutekeleza tendo hilo. Kwa kawaida tendo la ndoa halina kanuni moja, yaani sio jambo ambalo kila mtu anaweza kulifanya kwa kufuata kanuni moja na akaridhika, inategemea kwa kiasi kikubwa kuwa mhusika analichukuliaje tendo hilo ukilinganisha na kile alichojifunza juu ya tendo hilo tangu utotoni.
Kuna wengine wanalifurahia kutegemeana na mkao wakati wa tendo hilo, wengine watasema wanalifurahia zaidi pale walifanyapo na mtu wampendaye kwa dhati, ili mradi kila mtu atakwambia sababu ya kulifurahia tendo hilo, lakini je, vipi kuhusiana na ukubwa wa maumbile ya wanaume, yanayo nafasi kubwa kiasi gani katika kuwafurahisha wenzi wao katika tendo?
Katika hilo kuna kiwango kikubwa sana cha dhana kuhusiana na ukubwa wa maumbile ya wanaume na tendo la ndoa. Dhana hii imekuzwa kwa kiasi kikubwa sana na wanaume wasiojiamini kiasi kwamba imepewa nafasi na jamii na kuonekana kama jambo la msingi sana wakati hakuna uhusiano wowote kati ya ukubwa wa maumbile na ufanisi katika tendo la ndoa. Hata baadhi ya wanawake nao wameingia katika mtego huo na kuona kama hilo ni jambo la msingi wakati swala hilo halina kanuni.
Vipi kuhusiana na swala la hamu ya tendo la ndoa nalo? Kuna dhana imejengeka kuwa wanaume ndio wenye uchu mkubwa wa kufanya tendo la ndoa ukilinganisha na wanawake, dhana ambayo ina ukweli kwa kiasi fulani ingawa sio mara zote.
Je na wale wanawake wenye uchu wa tendo la ndoa kuliko wenzi wao inakuwaje? Hapa ni vigumu swala hili kuwekwa wazi sana na wahusika kutokana na kile tulichojifunza. Jamii imetufundisha kuwa wanawake ni wa kungoja tu waombwe tendo na sio vinginevyo. Pale mwanamke napokuwa hajaridhika na tendo la ndoa na mwanaume kuonekana kukosa hamu ya kuendelea, ujumbe unakwenda kichwani kwa mwanamke ni kujiona kama vile mumewe hampendi au amepata mwanamke mwingine nje ya ndoa au wakati mwingine hujihisi kupoteza ule uzuri wake uliomfanya mumewe ampende.
Je na ukubwa wa makalio ya wanawake nao unayo nafasi kubwa kiasi gani katika kuwavutia wanaume linapokuja swala la kufanya tendo la ndoa? Hii nayo ni dhana ambayo imepewa nafasi kubwa na wanaume na kuonekana kama vile ni jambo la msingi sana, wakati yale ni maumbile ya kawaida tu ambayo hayana uhusiano wowote na ufanisi katika tendo la ndoa. Lakini kutokana na ushabiki tu wa wanaume, hasa baada ya hii mitindo ya mavazi iliyoingia ambayo huacha maumbile ya wanawake wavaao mavazi hayo nusu uchi, na ndio maana swala hilo limepewa nafasi.
Bado tunayo safari ndefu sana katika kufikia muafaka juu ya swala hili, je ukubwa wa maumbile ya wanaume na ukubwa wa makalio ya wanawake unayo nafasi kiasi gani katika kulifurahia tendo la ndoa?
Tutafakari kwa pamoja……………………..
Kuna wanawake wengi wamekuwa ni wahanga wa madawa ya Kichina ya kuongeza makalio, kiasi kwamba wengine wamepoteza maisha. Ni jambo la kushangaza kidogo kuona kwamba serikali yetu imeshindwa kusimamia na kudhibiti uingizwaji wa haya madawa ya kichina yenye athari lukuki kwa binadamu mpaka pale zinapotokea athari za wazi.
Haya, sasa mambo yamegeuka, wanaume nao wameingia kwenye mkumbo huo. Hivi karibuni kuna habari zimesambaa huko nyumbani kuwa kuna mwanaume mmoja amejikuta akiwa na maumbile ya sehemu zake za siri makubwa kupita kiasi, inasemekana hata mkewe amemkimbia. Kisa, alitumia dawa za kichina za kukuza maumbili ya wanaume.
Habari zaidi zinadai kuwa mkewe alikuwa anatoka nje ya ndoa sana na baada ya mume huyo kumuuliza mkewe sababu ta kutoka nje ya ndoa ndio akajibiwa kuwa ana maumbile madogo na ndio maana akaona akatafute dawa za kichina ili akuze maumbile yake kumridhisha mkewe. Lakini kinyume na matarajio yake, maumbile yake yakawa makubwa kupindukia, hata mkewe akamkimbia.
Kuna wakati niliwahi kuandika juu ya wanaume kununua dawa za kuongeza nguvu za kiume maarufu kama mkuyati, kama ukitaka kujikumbusha bofya hapa. Nakumbuka nilipata upinzani mkubwa kutoka kwa wanaume, lakini naamini kwa hili watakubaliana na mimi.
Kwangu mimi wale wanawake wenzangu wanaokimbilia dawa za kichina ili kuongeza makalio yao na wale wanaume wanaotumia dawa za kuongeza nguvu za kiume maarufu kama mkuyati na dawa za kichina ili kuongeza maumbile yao nawaona kama watu wasiojiamini.
Mara nyingi tunapozungumziwa matatizo katika ufanyaji wa tendo la ndoa huwa tunafikiria matatizo ya ufanyaji kazi wa viungo vyetu tunavyotumia katika kutekeleza tendo hilo. Kwa kawaida tendo la ndoa halina kanuni moja, yaani sio jambo ambalo kila mtu anaweza kulifanya kwa kufuata kanuni moja na akaridhika, inategemea kwa kiasi kikubwa kuwa mhusika analichukuliaje tendo hilo ukilinganisha na kile alichojifunza juu ya tendo hilo tangu utotoni.
Kuna wengine wanalifurahia kutegemeana na mkao wakati wa tendo hilo, wengine watasema wanalifurahia zaidi pale walifanyapo na mtu wampendaye kwa dhati, ili mradi kila mtu atakwambia sababu ya kulifurahia tendo hilo, lakini je, vipi kuhusiana na ukubwa wa maumbile ya wanaume, yanayo nafasi kubwa kiasi gani katika kuwafurahisha wenzi wao katika tendo?
Katika hilo kuna kiwango kikubwa sana cha dhana kuhusiana na ukubwa wa maumbile ya wanaume na tendo la ndoa. Dhana hii imekuzwa kwa kiasi kikubwa sana na wanaume wasiojiamini kiasi kwamba imepewa nafasi na jamii na kuonekana kama jambo la msingi sana wakati hakuna uhusiano wowote kati ya ukubwa wa maumbile na ufanisi katika tendo la ndoa. Hata baadhi ya wanawake nao wameingia katika mtego huo na kuona kama hilo ni jambo la msingi wakati swala hilo halina kanuni.
Vipi kuhusiana na swala la hamu ya tendo la ndoa nalo? Kuna dhana imejengeka kuwa wanaume ndio wenye uchu mkubwa wa kufanya tendo la ndoa ukilinganisha na wanawake, dhana ambayo ina ukweli kwa kiasi fulani ingawa sio mara zote.
Je na wale wanawake wenye uchu wa tendo la ndoa kuliko wenzi wao inakuwaje? Hapa ni vigumu swala hili kuwekwa wazi sana na wahusika kutokana na kile tulichojifunza. Jamii imetufundisha kuwa wanawake ni wa kungoja tu waombwe tendo na sio vinginevyo. Pale mwanamke napokuwa hajaridhika na tendo la ndoa na mwanaume kuonekana kukosa hamu ya kuendelea, ujumbe unakwenda kichwani kwa mwanamke ni kujiona kama vile mumewe hampendi au amepata mwanamke mwingine nje ya ndoa au wakati mwingine hujihisi kupoteza ule uzuri wake uliomfanya mumewe ampende.
Je na ukubwa wa makalio ya wanawake nao unayo nafasi kubwa kiasi gani katika kuwavutia wanaume linapokuja swala la kufanya tendo la ndoa? Hii nayo ni dhana ambayo imepewa nafasi kubwa na wanaume na kuonekana kama vile ni jambo la msingi sana, wakati yale ni maumbile ya kawaida tu ambayo hayana uhusiano wowote na ufanisi katika tendo la ndoa. Lakini kutokana na ushabiki tu wa wanaume, hasa baada ya hii mitindo ya mavazi iliyoingia ambayo huacha maumbile ya wanawake wavaao mavazi hayo nusu uchi, na ndio maana swala hilo limepewa nafasi.
Bado tunayo safari ndefu sana katika kufikia muafaka juu ya swala hili, je ukubwa wa maumbile ya wanaume na ukubwa wa makalio ya wanawake unayo nafasi kiasi gani katika kulifurahia tendo la ndoa?
Tutafakari kwa pamoja……………………..
