Showing posts with label mihogo. Show all posts
Showing posts with label mihogo. Show all posts

Wednesday, January 17, 2018

BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO IMEONA HII IWE PICHA YA WIKI

Nikiangalia hii picha nakumbuka/najikumbuka mwenyewe jinsi tulivyokuwa kule kijijini KINGOLE tulikuwa na shamba la mihogo mbali kidogo mtaa wa LEGEZA...Basi nakumbuka  sana enzi zile.

Tuesday, August 30, 2016

KARIBUNI TUJUMUIKE KATIKA MLO HUU AUPENDAO KAPULYA......

 Mlo ni ni kachumbali, safu ya kwanza kwenye hicho chombo cha bluu karibu na kachumbali ni mihogo,katikati ni viazi vitabu na mwisho ni ndizi....
.....na hapa ni sahani yangu ilivyojazwa na cha kuteremshia   ni kinywaji cha uhai  si kingine ni MAJI

Saturday, April 26, 2014

HAYA NI MAPISHI YA JIONI YA JUMAMOSI YA LEO.......KARIBUNI KUJUMUIKA NASI!!

 Maandalizi:- Muhogo, Kabichi/Kebichi, kiazi kitamu, nyanya, binzari, chumvi, limau, kitunguu saumu,  kitunguu cha kawaida, tui la nazi, nyanya kopo,  maharagwe, mchele na mafuta.
 Wali wa nazi, Kachumbali, Maharagwe yaliyoungwa kitunguu, nyanya moja, chumvi na kijiko kimoja cha chai cha binzari, Kabichi/Kabichi iliyoungwa kwa nyanya na kitunguu, na mihogo na viazi vitamu vilivyokaangwa (chips)
Na hapa ndivyo ilivyoonekana sahani ya Kapulya jioni hii  na cha kuteremshia si kingine tena bali ni maji. KARIBUNI SANA...MIJA UPO...NA WENGINE WOTEEEE....TWAWATAKIENI JUMAMOSI NJEMA SANA WOTE!

Tuesday, October 29, 2013

NIMETAMANI SANA CHAKULA HIKI MIHOGO KWA SAMAKI

Nimetumiwa picha hii na mdogo wangu Sarah Mgaya sasa hivi ni mihogo na samaki ni chakula ambacho nimekula sana nawaza kusema ndicho kilichonikuza. Kama si hivyo basi ugali wa muhogo na samaki...nimetamani mno...ahsante

Sunday, February 5, 2012

JUMAPILI NJEMA...KARIBUNI CHAI KWA MIHOGO YA KUCHEMSHA!!!!

Mihogo ya kuchemsha.......
Na chai ya rangi

Karibuni tujumuika, mimi napenda zaidi mihogo ya kuchemsha. kuna wengine wanapenda ya kuweka nazi, karanga au nyanya na vitunguu. Je wewe unapenda mihogo yako itayarishweje? Haya ngoja niwatakieni wote jumapili njema sana. Mimi nakunywa chai yangu hapa maana baridi si mchezo!!!!

Friday, September 16, 2011

KARIBUNI KIKOMBE CHA CHAI...NINYIME VITU VYOTE LAKINI SIO CHAI!!!


You´re Just my Cup of Tea,

Our Love Warms my Heart.

Najua wote mnajua mie ni mpenzi sana wa chai tena ile isiyo na sukari(Chingambu) :-).

Kichwa cha habari hapo juu kinasema kuwa "NINYIME VITU VYOTE LAKINI SI CHAI" Duh ! naungama ni kwamba nimesema uongo kwani mimi ni mdhaifu/mpenzi sana wa smaki pia kama ilivyo kwenye chai......



Ngoja tusikilize wimbo huu wa Nuru ft Mr Chocolate Flavour - Muhogo Andazi!!!




NAPENDA KUWATAKIENI WOTE MWANZO MWEMA WA MWISHO WA JUMA ....MUWE NA AFYA NJEMA , AMANI NA FURAHA ZITAWALE NYUMBANI MWENU/WAKO.......IJUMAA NJEMA!!!!

Thursday, December 11, 2008

JINSI YA KUANDAA MIHOGO(KUMENYA)


Hapa nimekumbuka wakati nilikuwa mdogo hapo ni mama, mimi na kakangu kama sikosei. Ha ha ha ha. Halafu nimekumbuka sana wakati nasoma Songea pale Majengo chakula changu kilikuwa chips mihogo.Miaka ya 1990, kazi kwelikweli.