Showing posts with label boga na chai. Show all posts
Showing posts with label boga na chai. Show all posts

Wednesday, September 18, 2013

NILIKUWA NATEGEMEA KULA HAYA MABOGA LEO KUMBE....HAYALIWI .....

Mavuno ya maboga..Nimepata manne na leo nilipanga iwe siku ya kuyala nilitaka kutengeneza supu, kuchemsha na futari. Lakini wifi yangu kaniambia hayaliwi eti ni chakula cha nguruwe tu na yeye ndiye alinipa mbegu. Sasa hapa najiuliza kama nguruwe anakula na kupona kwanini binadamu asile...Kuyatunza kwote nilikofanya yaani ni kazi ya cheka bure kweli???,,Na ndo nikaamua niwaulize ndugu zanguni je ni kweli?...Maana majani yake yana  mibamiba zikukuchoma zinawasha na majani ni mapana kuliko ile mboga ya maboga ya Njombe na ile ya kawaida...Au sijui ni mabuyu/ yale ya kutekea maji au kunywea maji yaani kata?...Duh kaaaazi kwelikweli hapa sasa nimekwama inabidi nianza upya kuwaza cha kula:-(.

Tuesday, August 21, 2012

CHAKULA CHA ASUBUHI YA LEO..DADA PENINA UPOOOO??? KARIBU PIA NA WENGINE WOTE...!!!

Haya ni maoni ya Dada Penila Simon kutoka katika picha hii hapa."Hongera, jitihada zako nimeziona, nakupenda ulivyo na pia, the way ulivyo busy na pia husahau asili. i real loe u baby.
Napenda na naomba unionjeshe kidogo picha baada ya kulipika lilisindikizwa na nini na lilikaaje mezani plz..." Nami nimeona si vibaya kama nikifanya kama dada P alivyoniomba hivi ndivyo mambo yalivyokuwa dada P, pamoja na wengine wote..fuatana nami.....

 Nimeamka asubuhi. Nimeingia katika shambani/bustani yangu na  kuchuma boga..kama nilivyowaambia hapo juzi na ....hivi ndivyo ilivyokuwa....boga
Nimechemsha na halafu tayari kwa Chakula cha asubuhi. Yaani boga kwa chai ya rangi. Kwa mimi chai yangu kama kawaida bila sukari hapo nimelifaidi na kulamba mikono si mchezo..je wewe unapenda kula boga lako vipi? au unalitemshia na nani?....mmmhhh sijui mchana huu nipike/nile nini? Natamani.. naacha sisemi mtaona baadaye kidogo tu...:-)