Nikajaribu na njegere ...aaahhh mama yangu nusu nilie ndo kama muonavyo sijui kama tutakula. pia kumezuka konokono wanakula mimea yotr walayo binadamu kwa hiyo mie nikipanda ikijitokeza tu wao wanafyeka/kula tu....Inakatisha tamaa
Na mwisho nikaona nijaribu kutumia makopo/ndoo ili kuweza kupanda na kuona kama itakuwaje matokeo yake ni haya Nyanya, pilipili, pilipili hoho na maua na kuviweka kwenye varanda vimekubali. Lakini sasa nitakulaje viungo tu bila mboga na ugali?:-)
Naomba kwa yeyote mwenye ushauri anishauri la kufanya.... JUMATATU NJEMA!