Showing posts with label BUSTANI 2016. Show all posts
Showing posts with label BUSTANI 2016. Show all posts

Monday, July 25, 2016

NASIKITIKA SANA MWAKA HUU BUSTANI YETU HAISTAWI KAMA MIAKA MINGINE....

 ...Nimejaribu mara zaidi ya mara sita kupanda mbegu za mbogamboga kama nifanyavyo lakini zimenigomea. Nikaona labda nijaribu kupanda kwenye kopo nikafanikiwa ndo hili/ huu mmea wa boga muuonao:-(. Kwanza nilifikiri ardhi  imechoka nikaweka mbolea lakini wapi....

 Viazi mviringo afadhali vimekubali na kama muonavyo nitavuna karibuni maana majani yameanza kukauka pia....
 Nikajaribu na njegere ...aaahhh mama yangu nusu nilie ndo kama muonavyo sijui kama tutakula.   pia kumezuka konokono wanakula mimea yotr walayo binadamu kwa hiyo mie nikipanda ikijitokeza tu wao wanafyeka/kula tu....Inakatisha tamaa
Na mwisho nikaona nijaribu kutumia makopo/ndoo ili kuweza kupanda  na kuona kama itakuwaje matokeo  yake ni haya Nyanya,  pilipili, pilipili hoho na maua  na kuviweka kwenye varanda vimekubali. Lakini sasa nitakulaje viungo tu bila mboga na ugali?:-)
Naomba kwa yeyote mwenye ushauri anishauri la kufanya.... JUMATATU NJEMA!