Showing posts with label jumatano ya marudio. Show all posts
Showing posts with label jumatano ya marudio. Show all posts

Wednesday, August 22, 2012

WANAWAKE KUTEMBEA NUSU UCHI, KUMBE WANA LAO JAMBO.....!

Leo katika KIPENGELE CHETU CHA JUMATAN YA MARUDIO YA MADA AU MATUKIO MBALIMBALI.  KATIKA PITA PITA ZANGU LEO NIMEPAMBANA NA HII  KWA MZEE WA UTAMBUZI.

 Kuna wakati wanaume hudhani kwamba, wanawake wanaovaa nusu uchi huwa wanafanya hivyo kwa sababu ya kutafuta soko kwa wanaume. Inawezekana kukawa na wale ambao wana sababu hizo, lakini wapo wale ambao wanalipa fidia kutokana na kuamini kwao kwamba, sura zao zimewaangusha, hivyo miguu yao mizuri inabidi kuziba pengo au udhaifu huo.


Wakati mwingine hata wanawake wanaodhani au kudhaniwa kuwa ni wazuri, wamekuwa wakivaa nguo fupi zinazoonyesha maungo yao. Hawa nao ni lazima wanalipa fidia ya kasoro fulani waliyo nayo. Inawezekana wameshindwa kulinda ndoa zao, au inawezekana hawajaolewa na sasa wanataka kuonyesha kwamba, pamoja na kutoolewa kwao, bado wao wana sura na miguu au miili mizuri.

Udhaifu wowote ambao unamkera mwanamke iwe ni wa moja kwa moja au kupitia nyuma ya ubongo wake, unaweza kuonyeshwa kwa mwanamke huyo kuyatangaza yale maeneo ya mwili wake ambayo anaamini ni mazuri. Kuyatangaza huko humpa ahueni kwa kuamini kwamba bado anayo thamani, kwani ataangaliwa sana na wanaume, kusifiwa na pengine kutongozwa.

Hebu angalia wanawake ambao wanavaa nguo za kubana huku wakiwa na makalio makubwa. Hawa mara nyingi wana sura ambazo wao au wengi huamini kwamba ni mbaya. Huvaa nguo hizi ili kuonyesha kwamba, pamoja na ubaya wa sura zao, bado wao ni wazuri sana katika maeneo mengine ya mwili ambayo wanaume na hata wanawake wengi huyapenda au kutamani kuwa nayo.
Wengi hawavai tu nguo hizi za kubana kwa sababu ni fasheni, la hasha, wengi hili ni kimbilio la udhaifu wao.
PANAPO MAJALIWA TUONANE TENA JUMATANO IJAYO KATIKA KIPENGELE HIKI CHA MARUDIO.!!!



Wednesday, August 1, 2012

TUNAJENGA TAIFA LA WALEVI?


Ni ile JUMATANO YA KIPENGELE CHA MARUDIO YA MATUKIO MBALIMBALI NA LEO NIMETEMBELEA HAPA NA KUKUTANA NA HII HABARI NIMEIPENDA NA NIMEONA TURUDIE ILI KUJIFUNZA ZAIDI.

Mtu mmoja akiwa amelala porini baada ya kuzidiwa na kilevi

Pombe ni kiburudisho muhimu sana kwa walio wengi. Mamilioni ya wanaume na wanawake ulimwenguni wanatumia au wamewahi kutumia pombe wakati fulani katika maisha yao.

Umaarufu wa pombe bila shaka unatokana na uwezo wake katika kumfanya mtumiaji ajisikie vizuri na kusahau matatizo yanayo mkabili japo kwa muda. Pombe huondoa aibu, huufanya mwili kusisimka na kuleta furaha.

Kwa sababu hiyo pombe ni kimbilio la watu wengi wenye furaha, na wenye matatizo na shida za aina mbalimbali. Kwa mtazamo wa haraka haraka tunaweza kusema pombe ni nzuri na inafaa kutumiwa kama kiburudisho endapo mtumiaji atakuwa na kiasi na kuitumia kwa namna inayofaa.

Kwa upande mwingine pombe ni kitu kibaya sana kwani madhara yake yanazidi faida na hasa kwa kuzingatia kwamba ni watu wachache sana wanaoweza kufuata mashalti ya utumiaji kileo kama inavyotakiwa. Leo hii pombe ni chanzo kikubwa cha ajali za barabarani zinazo sababisha mauaji ya maelfu ya watu wasiokuwa na hatia.

Pombe ni hatari kwa wajawazito
Pombe pia ni chanzo kikubwa cha matatizo ya kijamii ikiwa ni pamoja na kusambaratika kwa familia, na ongezeko la talaka jambo linalosababisha mateso makubwa kwa watoto.

Aidha, pombe inachangia sana katika kuleta umaskini kwa mtu binafsi, familia na hata taifa. Pombe husababisha uzembe kazini, kupunguza uwezo wa kufikiri na kutoa maamuzi na kusababisha madhara katika ubongo hasa kwa watumiaji wenye umri mdogo (watoto).

Pombe pia husababisha matatizo ya kiafya kwa watoto walioko tumboni (ambao hawajazaliwa). Wanawake wajawazito wanaotumia pombe hujiweka katika hatari kubwa ya kuharibu akili (ubongo) za watoto wanaowabeba matumboni mwao.

Ni kwa sababu hiyo nchi zilizoendelea (kama Marekani na baadhi ya nchi za ulaya) zimepiga marufuku uuzaji wa pombe kwa vijana wenye umri chini ya miaka 18, na zinaendesha kampeni za kuwaelimisha akina mama kuepuka matumizi ya pombe katika kipindi chote cha ujauzito.

Pamoja na madhara makubwa yanayoletwa na unywaji wa pombe, ni ajabu kwamba nchini mwetu pombe tumeigeuza kuwa sehemu ya maisha. Watu wengi wenye kipato cha kawaida hujiingiza katika unywaji pombe wa kupindukia kutokana na kasumba iliyojengeka nchini mwetu kwamba watu wanaokunywa pombe kila siku wana pesa nyingi. Watu wanaojiingiza katika ulevi hufanya hivyo kwa kudhani wanainua 'status' zao.

Wengi wa walevi hawa hujikakamua kununua pombe zenye bei kubwa zaidi ili kuonesha kuwa wana pesa na kuwakoga wasiokuwa nazo. Baadhi ya wanywaji hufikia hatua ya kuweka bili katika mabaa na store zinazouza pombe ili waweze kunywa pasipo kukosa hata kama hawana pesa (na kulipa mwisho wa mwezi) jambo linalowaingiza katika umaskini wa kujitakia pasipo kujua.

Ni kutokana na ongezeko kubwa la wanywaji wa pombe makampuni mbalimbali yanayo tengeneza na kusambaza vileo yameivamia Tanzania kwa nguvu na kumwaga pombe za kila aina mitaani. Makampuni haya hujitengenezea faida kubwa isiyoelezeka.

Aidha wafanya biashara wengi nchini wameacha kuwekeza katika vitega uchumi vingine vya kimaendeleo kama kilimo, ufugaji, viwanda vidogo vidogo, elimu n.k na kugeukia biashara ya pombe ambayo inaelekea kutokuwa na mpinzani katika kuingiza faida. Si ajabu kwamba katika miji yetu kuna baa katika kila kona.

Mbaya zaidi ni kwamba serikali haifanyi jitihada zozote kudhibiti uuzaji na matumizi ya kileo katika nchi yetu (pengine kutokana na kodi kubwa inayokusanya kutoka katika biashara ya vileo). Matokeo yake pombe huuzwa kwa mtu yeyote bila kujali umri wake, muda wala mazingira inapouzwa pombe hiyo.

Leo hii makampuni makubwa yanayouza vileo ikiwa ni pamoja na kampuni ya TBL yanafanya matangazo mengi ya kuwashawishi wananchi kunywa pombe bila kujali matangazo hayo yanawavutia watoto wadogo. Hebu fikiri yale magari yanayotangaza bia mitaani kwa kupiga muziki huku kina dada warembo wakicheza mayenu na kugawa zawadi za bia kwa wananchi waliokusanyika.

Ni hivi juzi tu kampuni maarufu ya bia nchini iliendesha tamasha kubwa la muziki ambapo kiingilio ilikuwa kopo la bia ambayo mteja alipaswa kuinunua uwanjani hapo. Katika tamasha hilo washiriki wengi walikuwa vijana wadogo wenye umri chini ya miaka 18 ambao waliuziwa pombe bila hofu wala aibu.

Ni lazima tukubali ukweli kwamba pombe ni hatali kwa afya na maendeleo. Ndio maana nchi zilizoendelea (Marekani, Ulaya na hata baadhi ya nchi za kiarabu) zimeweka taratibu kali za kudhibiti matumizi ya vileo ikiwa ni pamoja na kuzuia uuzaji wa pombe kwa vijana wenye umri chini ya miaka 21 (kwa USA), kuzuia unywaji wa pombe hadharani, kupanga masaa maalum ya uuzaji wa pombe na kuzuia aina zote za matangazo ya pombe yanayo walenga vijana wadogo.

Ni jambo lililo dhahiri kwamba ulevi ni adui wa maendeleo na hivyo kuendelea kujenga taifa la walevi ni hatari kwa maendeleo, afya na usalama wa jamii yetu. Ni kwa sababu hiyo tunaishauri serikali kutoa elimu kwa umma kuhusu madhara ya utumiaji vileo.

Aidha ni vema serikali ikatunga sheria kali za kudhibiti uuzaji holela wa vileo ikiwa ni pamoja na kupiga marufuku uuzaji wa pombe kwa watoto wenye umri chini ya miaka 18.Ni muhimu sheria hizo pia zifafanue aina ya matangazo ambayo makampuni ya uuzaji vileo yanaruhusiwa kufanya ili kudhibiti matangazo yanayowalenga vijana wadogo, na pia kutamka maeneo na muda unaoruhusiwa kuuza vileo kisheria.

Kama serikali isipochukua hatua za haraka kudhibiti ongezeko la walevi nchini, si ajabu nchi yetu ikaendelea kudidimia katika wimbi kubwa la umaskini wa kujitakia. Na watu wengi wataendelea kuamini kuwa serikali inaendekeza ulevi ili wananchi wengi wasione hali ngumu ya maisha iliyoko nchini na kuipigia kelele serikali.
Na Mwana Dikala
TUONANE TENA PANAPO MAJALIWA!!!

Wednesday, July 11, 2012

NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMATANO NJEMA NA UJUMBE HUU!!!

HAYA NDUGU ZANGUNI NI ILE JUMATANO YA KIPENGELE CHA MARUDIO YA MATUKIO MBALIMBALI. KWA HIYO LEO NIMEONA NIWEKE PICHA HII AMBAYO NILISHAWAHI KUIWEKA. KARIBUNI....

Macho ya huruma hufurahisha moyo, habari huburudisha mwili. Kuchukiana huendekeza fitina, kupendana husitiri makosa yote. Nilikuwa mgonjwa ukaja kuniona .Nilikuwa na njaa ukanilisha. Kumhudumia mgonjwa ni wito. JUMATANO NJEMA KWA WOTE . NA KUMBUKENI WOTE MNAPENDWA!!! NA PANAPO MAJALIWA BASI TUONANE TENA WAKATI MWINGINE.

Wednesday, June 6, 2012

SALAMU NI NUSU YA KUONANA

Au tu kwa vile ni jumatano ya marudio basi ngoje turudie  na hii. nimeipata hapa
Tusalimiane japo kwa maneno machache wakati wowote bila kujali majukumu yetu ndani mikikimikiki ya maisha kwa kuwa kila mmoja anamhitaji mwenzake kwa nyakati tofauti ijapokuwa nyakati nyingine waweza kuhisi kuwa mtu fulani siyo muhimu sana kwako lakini wakati wa uhitaji ndiyo unatambua bila fulani mchakato wa maisha na mafanikio hauwezi kufikia tamati.
Kama wingi wa viungo mwilini kwa kutazama lakini wakati wa mahitaji kila kimoja kwa nafasi yake humtimizia binadamu haja yake.
"Salamu ni daraja la urafiki"
Wasalamu na shukrani;
 

JUMATANO NJEMA!!!

Wanafunzi hawa wanafanyishwa vibarua


Ije jumatano ya KIPENGELE CHETU CHA MARUDIA NDIO LEO NA LEO NIMEONA KWA VILE WIKI ILIYOPITA TULIZUNGUMZIA KIDOGO KUHUSU ELIMU BASI TUENDELEE KIDOGO NA MADA HII YA SHULE NA ELIMU.
Wanafunzi wa shule ya msingi Ndingine mwambao mwa ziwa Nyasa wilayani Mbinga mkoani Ruvuma wakifanyishwa kazi ya kusomba tofali muda wa masomo
LICHA ya serikali kupiga marufuku walimu kuwafanyisha vibarua wanafunzi wakati wa masomo,bado baadhi ya shule hasa katika maeneo ya vijijini,zinaendelea na tabia hiyo hali ambayo inachangia kuzorotesha elimu nchini.
Uongozi wa shule ya msingi Ndingine iliyopo kata ya Ngumbo mwambao mwa ziwa Nyasa wilayani Mbinga mkoani Ruvuma bado unaendelea kuwafanyisha vibarua wanafunzi licha ya afisa elimu wa wilaya hiyo kupiga marufuku jambo hilo.
Uchunguzi ambao umefanywa na mwandishi wa habari hizi katika kijiji cha Ngumbo hivi karibuni ulibaini wanafunzi baadhi wakiondolewa madarasani tena majira ya asubuhi na kwenda kufanyishwa kibarua cha kubeba tofali za kuchoma kutoka kwenye tanuli lililokuwa mtoni hadi mahali ambapo nyumba inajengwa umbali wa kilometa tatu.
Wanafunzi wa darasa la tatu na la sita kutoka shule hiyo walishuhudiwa wakisomba tofali hadi nne kichwani huku wakilalamika kuwa wanafanya kazi ambayo hawanufaiki nayo licha ya kuambulia maumivu kutokana na mzigo na umbali.
Baadhi ya wanafunzi wanasoma darasa la sita walipohojiwa ,walidai kuwa mwalimu amewaambia huo ni mradi wao ambao utawawezesha kupata fedha kwa ajili ya sherehe za mahafali ya kumaliza elimu ya msingi hapo mwakani watakapomaliza darasa la saba.
Hata hivyo wanafunzi wa darasa la tatu walilalamika kuwa wao wamelazimishwa na mwalimu kwa kuwa hawapati chochote na kwamba fedha zote wanachukua walimu,ingawa tofali zinachangia kuchafua sare zao za shule ambazo wakirudi nyumbani inawalamu wazazi kununua sabuni ili kufua nguo zao.
Miongoni mwa wazazi waliohojiwa kuhusiana na watoto wao kuendelea kufanyiwa kazi za vibarua,waliomba serikali ya wilaya kuwachukulia hatua walimu wa kata za Ngumbo na Liwundi kwa kuwa wamezoea kuwafanyisha kazi wanafunzi wao licha ya wazazi na walezi kukataa.
“Sisi wazazi kwenye vikao tulishakubaliana tutachangia shilingi 2000 kila mzazi ,walimu waache tabia ya kuwafanyisha kazi watoto wetu badala yake waendelea na kusoma lakini walimu bado wanaendelea kuwafanyisha kazi mbalimbali wanafunzi kama vile kuchota maji ya walimu,kubeba tofali,kukata matete,kubeba kuni pamoja na kazi nyingine nyingi’’,alisema Martha Nchimbi mkazi wa Mkili.
Hata hivyo mwalimu mkuu wa shule ya msingi Ndingine Aidan Mbilinyi alipohojiwa kuhusiana na kuwafanyisha kazi za vibarua wanafunzi alidai kuwa katika shule yake wanafunzi hawafanyishwi vibarua badala yake wazazi wanachangia kila mwaka shilingi 2000 kwa ajili ya sherehe za mahafali ya darasa la saba .
Katika kikao cha walimu wakuu wote wa wilaya ya Mbinga ambacho kiliitishwa na idara ya elimu chini ya mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga Septemba 23 mwaka huu pamoja na mambo mengine waliazimia kuacha kuwafanyisha vibarua wanafunzi vikiwemo kusomba tofali na kuvuna kahawa.
Afisa elimu wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga David Mkali amekemea tabia ya walimu wakuu kuendelea kuwafanyisha kazi wanafunzi na kusisitiza kuwa kuanzia sasa atachukua hatua za kinidhamu kwa walimu wakuu wote ikiwa ni pamoja na kuwashusha vyeo vyao.
“Maazimio yalipitishwa tangu mwezi Septemba mwaka huu marufuku wanafunzi kufanyishwa vibarua,shule zibuni miradi ya kujitegemea itakayowawezesha kupata fedha,pia walimu kuwapatia wanafunzi maarifa ya kujitegemea kwa mfano kulima bustani baada ya saa za masomo’’,alisisitiza.
Mkali aliyataja mambo ambayo yamechangia kushuka kwa elimu na ufaulu kwa wanafunzi wa shule za msingi wilayani Mbinga kuwa ni pamoja na wanafunzi kufanyishwa vibarua,utoro na ulevi kwa baadhi ya walimu,walimu kutofundisha siku zote 195 zilizopangwa na wizara,walimu wakuu kutofuatilia ufundishaji,ukaguzi wa maandalio na kazi za watoto.
Takwimu zilizokusanywa katika shule 321 katika Halmashauri ya wilaya ya Mbinga kuanzia darasa la tatu hadi la saba zinaonesha kuwa wanafunzi 15,128 kati ya 116,966 hawajui kusoma,kuandika na kuhesabu
Makala hii nimeipata hapa JAMIIFORUM IMEANDIKWA NA  Albano Midelo hapo decemba 13th 2011 pia kwa kuweza kusoma habari nyingi inayofanana na hii ingia hapa. TUKUTANO TENA JUMATANO IJAYO PANAPO MAJALIWA.
 

Wednesday, May 30, 2012

UNATAKA KUMUACHA MKE MKOROFI? FANYA HIVI.........!


Ni ile JUMATANO YA KIPENGELE CHA MARUDIO NA LEO NIMEIKUTA HII KWA KAKA YANGU WA HIARI KALUSE Hebu soma na halafu tujadili kwa pamoja.KARIBU...



Kuna wanaume ambao wametokea kuoa wanawake ambao wana tabia mbaya . ninaposema kuwa na tabia mbaya sina maana ya mwanamke kuwa Malaya, maana hiyo ni fasili rahisi ya tabia mbaya kwa watu walio wengi. Ninaposema tabia mbaya nina maana kwenda kinyume na matarajio ya mume na pengine hata kwenda kinyume na matarajio ya jamii. Mwanamke ambaye ana tabia kama ghubu, mdomo mdomo (mkosoaji), mtapanyaji wa mali, mpenda makuu na tabia nyingine za aina hiyo, ni mwanamke ambaye kwa kiasi kikubwa anaweza kumsababishia mume matatizo ya kimwili na kisaikolojia. Mwanamke wa aina hii anaweza hata kuathiri makuzi ya watoto na kuathiri uhusiano na mume na watu wengine waliyo karibu yake. Kama mwanamke wa aina hii ameolewa na mume mweledi ndoa inaweza isiyumbe sana, lakini hii ina mipaka na kiwango chake.

Kuna wakati matatizo haya huweza kufika mbali zaidi kiasi kwamba huanza kumwathiri mume. Mwanaume ambaye huchukua kila uamuzi unaohusu maisha yake kwa hadhari kubwa, anaweza kuendelea kuishi na mke huyu. Lakini mara nyingi kuendelea kuishi na mke huyu kuna maana ya matatizo zaidi kuliko ufumbuzi. Bila shaka mmeshawahi kusikia wanaume ambao wanalalamika kuhusu tabia mbaya za wake zao (hata hapa JF wapo wengi sana), lakini huku wakiendelea bado kuwa na wake hao. Ukiacha sababu ya kugawana mali, wanaume wengi huwa wanafikiria mambo mengi ambayo huwazuia kuchukua uamuzi wa kuachana na wake hao.

Nimeona itakuwa vizuri kuwaambia wanaume hawa kwamba, kama ndoa zao zimefikia mahali ambapo zinataka kuwatia kichaa, wakiwa na uhakika kwamba wake zao ndio wenye matatizo na sio wao, (hili inabidi waliangalie kwa makini) inabidi wafanye uamuzi kwa kujiangalia wao na watoto wao zaidi kuliko watu au vitu vingine. Baadhi ya mambo ya kuangalia ni haya:

1. Kuathirika kwao: wajiulize wanaumia kiasi gani kimwili na kisaikolojia kwa kuendelea kuishi kwao na wanwake hawa. Kama ni ghubu na kukosolewa, kunawaathiri kiasi gani,? Na kama ni utumiaji mbaya wa mali unawaathiri kwa kiasi gani? Kama athari za tabia mbaya alizo nazo mwanamke zinafaa kudharauliwa na mume anaweza kuzidharau ni vyema akafanya hivyo, na kuendelea na maisha. Na kama akiona kuzidharau tabia hizo itakuwa na maana ya angamio kwake na pengine mbaya zaidi kwa watoto, inabidi hiyo iwe ni sababu ya msingi kuachana na mke huyo.

2. Ndugu watasemaje: wanaume wengi hukwamia hapo. Kama wake zao wanaelewana vizuri na baadhi ya ndugu, au hata wazazi wao, wanaume hushindwa kutoa maamuzi wa kuwaacha kwa hofu ya kulaumiwa na kushangawa. Wakati mwingine mume huyu anaelewena sana na watu wa upande wa pili, yaani ndugu wa mke na hasa wazazi na pengine wote. Hiki nacho ni kikwazo kikbwa sana, kwani mume hufikiria jinsi atakavyoonekana kwa watu hawa, pale atakapoamua kuchukua uamuzi wa kumuacha mkewe.

3. Sifa moja nzuri: pamoja na kuwa na matatizo, kila binadamu anaweza kuwa na upande mzuri. Kama mwanamke huyu ana sifa fulani ambayo ni nzuri sana, tuseme ni mpishi hodari sana na mkarinu kwa wageni , au labda ni mwaminifu sana katika ndoa, mwanaume anaweza kukwama kutoa uamuzi kwa kudhani au kujidanganya kwamba huenda anaweza asipate mwanamke mwingine mwenye sifa kama hizo. Huku ni kujidanganya kwa sababu kila sifa aliyo nayo binadamu fulani, ya kitabia, ipo kwa binadamu mwingine hata kama siyo wengi.

Ukweli ni kwamba mwanaume anaweza kushindwa kumpa talaka mkewe ambaye anakaribia kumuuwa kwa matatizo yake kwa sababu ambazo mtu mwingine anaweza kuzishangaa. Lakini jambo la msingi kwa mwanaume kama huyu ni kujaribu kupima kwa makini, je hizo sababu zinazomfanya asite kuachana na mkewe huyu zina nguvu au maana kuliko maisha yake, hasa mwili na akili yake?.
Angalizo: Sishauri watu kuachana, lakini nashauri watu kujua kwamba ndoa zenye mashaka makubwa ni hatari kwa afya na maisha yao. 
TUKUTANE TENA PANAPO MAJALIWA..JUMATANO NJEMA.

Wednesday, May 23, 2012

BWANA MATATA HAJUI KUSOMA+KUMBUKUMBU


Mada hii nilishawahi kuiweka hapa kibarazani, lakini jana katika pitapita nimekukta picha kwa prof. Matondo nikakumbuka  kitabu cha bwana Matata na nimeona si mbaya kama tukijadili tena kwa pamoja . NA UKIZINGATIA LEO NI KILE KIPENGELE CHA JUMATANO YA MARUDIO YA MAMBO MBALIMBALI..Haya soma haabari yenyewendiyo hii

Kwanza naanza na kusema NAMSHUKURU  babangu kwa kutunza kitabu hiki leo nimefurahi sananwaeza kuwasomea hata wanangu. Nadhani hata wenzangu mtafurahi pia kukumbuka hadithi hii:-
Bwana Matata yupo mjini, anauliza uliza njia ya hospital. Kuna kibao hapo njiani, lakini haui kusoma kibao.Bwana Matata anaona aibu kuuliza njia tena, anaona aibu kwa sababu hajui kusoma. Sasa anafuata njia ya bomani
Bwana Matata amechoka sana. Amechoka na safari, pia amechoka kuuliza uliza njia. Amelala kwenye kibao, kibao kinasema HATARI. Lakini Bwana Matata hajui kusoma, tena amechoka mno. Amelala njiani kwenye kibao

Bwana Polisi anapita, anamwona Bwana Matata amelala kwenye kibao. Bwana polisi anamwita, mzee vipi? Kwa nini unalala hapa? Huoni kibao? Lakini Bwana matata amechoka sana amelele kama gogo. Polisi amawita tena, kwa nini unalala hapa kama gogo? Kuna hatari hapa. Lakini bwana matata hana habari ya hatari hajui kusoma.

Bwana Matata akaamka, akasimama na kumwambia polisi, nataka kwenda hospitali. Mtoto wangu yupo hospitali ni mgonjwa sana, lakini nimepotea njia. Bwana polisi akasema, umepotea njia? Fuata hii Bwana Matata akafuata njia ile. Kinachoendelea naadhani mnajua 
JUMATANO NJEMA........

Wednesday, May 9, 2012

Tuwe na shukrani. Tusikate tamaa kabla hatujaona yote


Ni kile chetu cha KIPENGELE CHA JUMATANI YA MARUDIO..NA LEO KATIKA PITA PITA NIMEKUTANA NA HII. BINAFSI NIMEIPENDA MNO SI KWINGINE NILIKOIKUTA BALI NI KWA MZEE WA CHANGAMOTO. KARIBUNI.

------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Nakumbuka mwaka 2000 nilikuwa nikihudhuria mazoezi ya mgongo pale Muhimbili baada ya ajali ya Dec 1999. Siku moja niliamini kuwa katika maumivu makali saana. Na nilikuwa nikisubiri zamu yangu kwenda kuonwa na Daktari (pale taasisi ya mifupa) kabla ya kurejea mazoezini na nikiwa nimekaa nikaona wenzangu wakiongea na nilidhani hawakuwa katika maumivu kama niliyokuwa nayo. Nilihisi kuwa mwenye maumivu kuliko wote. Baada ya dk kama 30 kupita, ikaongezeka sauti ya kaka mwingine aliyekuwa akiongea kwenye simu kwa sauti ambayo haikuonesha kuwa anaumia. Mawazoni mwangu nikawaza tena kuwa "hawajui niko katika maumivu kiasi gani". Niliponyanyua uso, nikamuona kaka aliyesimama pembeni yangu ambaye alionekana kuharibiwa vibaya mguu wake ajalini. Nilishangaa kuwa ndiye aliyekuwa akiongea vile. Nilijihisi kupona na nilimpisha akae mahali nilipokuwa nimekaa. NIKAJIFUNZA.
Katika maisha ya kila mmoja kuna maanguko meeengi ambayo yanapotokea huwa tunajiona kama ndio tumefika mwisho wa maisha. Tunafikiria "kwanini" na pengine kuwaza kama "kuna anayepitia haya?" Hatujui kuwa wapo walio katika mataabiko zaidi ya tuliyopo.
Jana usiku nilienda kumtembelea mtoto mchanga wa rafiki yangu ambaye anaumwa saana. Na nikiwa katika hospitali hiyo ya watoto niliona watoto weeengi walio katika hali za kuendeshewa maisha yao kwa mashine. Nikasikitika. Nina mpenzi makubwa saana na watoto kwa hiyo hali hiyo ilichukua sehemu kubwa ya furaha ya asili ndani mwangu. Nilijiuliza maswali mengi saaana kuhusu hali ile na kunifanya kurejesha taswira za maisha yangu tangu pale nilipoweza kukumbuka. Kisha nikarejea katika ukweli kuwa na mimi nilikuwa mtoto kama wao na niliweza kuvuka umri walionao. Niliona nyuso za wazazi wakiwa na matumaini ilhali wana uoga mwingi na ilinifanya kumuomba Mungu juu ya watoto hao. Niliporejea nyumbani ilinichukua muda kurejea katika hali ya kawaida. Na bado naendelea kuwaza na kujiuliza kama NILISTAHILI KUWA NAKATA TAMAA NIPATAPO MAKWAZO / MAJARIBU? Najiuliza kama TUNA HAJA YA KUONA KAMA MUNGU HAYUKO UPANDE WETU KWA KUWA HATUNA UHAKIKA WA KUWA NA AKIBA YA KUTOSHA MPAKA WAKATI WA MALIPO YAJAYO, AMA KWA KUWA TUNAHISI TUTASHINDWA MTIHANI DARASANI AMA KWA KUWA HATUWEZI KUNUNUA TUNACHOPENDA KUWA NACHO AMA KWA KUWA TUMEPOTEZA KAZI.
Nikiwaangalia watoto wale, nilihisi kama wangepewa uchaguzi wa kuendelea kuwa pale walipo, ama wakue na wakutane na yale yatukatishayo tamaa, sina shaka wangekubali kukua na kupambana na tupambanayo sasa.
Nimezidi kugundua na kujifunza kuwa kila kitokeacho kina sababu na naamini Mungu ana kila sababu ya kutuweka mahala fulani, wakati fulani, tukutane na fulani na tujifunze kitu fulani. Safari yangu ya jana imenifungua macho ya ki-Imani na kunifanya kuuangalia uhai wangu kwa "vipindi" vifupifupi ambavyo nimejaribu kufikiri mengi niliyoepushwa katika vipindi hivyo. Maradhi na mapungufu ya kabla na baada ya kuzaliwa, ajali na hatari mbalimbali na nimeona kuwa wengi wetu (nikiwemo) tunaishi kama vile kila siku ILIAHIDIWA KWETU. Si kweli
Ni kwa kutojua namna tulindwavyo ama namna namna tulivyoepushwa ma vyanzo vingi vya kifo, tunashindwa kumshukuru Mungu kwa uwepo wetu licha ya yale tupambanayo nayo.
Tunastahili kumshukuru Mungu kwa maisha yetu, kisha kumuomba aendelee kutuonesha yaliyo mapenzi yake.
Hivi niandikavyo nakaribia kuelekea hospitali kuona hatua za mwisho za madaktari kuokoa maisha ya binti wa rafiki yangu huyo (hajatimiza hata mwezi mmoja) kabla hawajazima mashine zimsaidiazo kuishi sasa ambazo zimepangwa kuanza kuzimwa takriban masaa mawili kamili yajayo.
KATIKA KILA GUMU TUPITIALO, TUSHUKURU MUNGU NA TUSIKATE TAMAA KABLA HATUJAONA YOTE KWANI KUNA WEEENGI WANAOTAMANI KAMA WANGEKUWA TULIPO SISI PAMOJA NA MATATIZO YETU. Hawawezi na pengine hawatafika tulipo kwani hawana muda wa kuishi.
PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA NA RUDIO JINGINE..KILA LA KHERI!! MAISHA NA MAFANIKIO/KAPULYA

Wednesday, May 2, 2012

DUNIA HAINA SIRI......MNAIKUMBUKA HII?

Kama kawaida ni kipengele chetu cha JUMATANO YA MARUDIO YA MATUKIO MBALIMBALI  na leo katika kuperuzi nimekutana na hii. na nilipeperuzi ni hapa



Panapo majaliwa tukutane tena JUMATANO IJAYO na MARUDIO MENGINE/JINGINE...MUWE NA WAKATI MZURI WOTE!!!

Wednesday, April 18, 2012

NAMNA YA KUTOKA KWENYE UTUMWA WA NDOA…….

Habari za leo..Ni ile JUMATANO YA KIPENGELE CHA MARUDIO YA MAMBO MBALIMBALI. Leo nimeperuzi kwa kakangu Kaluse na kukutana na hii mada. KARIBUNI TUJADILI KWA PAMOJA.
Sio lengo langu kuwafundisha wanawake namna ya kuachana na wapenzi au waume zao. Lakini hebu fikiria kwamba kila wakati wanandoa au wapenzi wako kwenye vita. Hakuna amani, hakuna masikilizano. Kutwa nzima mtu anawaza kuhusu uhusiano wake mbaya hadi anashindwa hata kufanya kazi. Je, hali kama hii ina maana kwa mtu kuendelea kuwa kwenye ndoa?

Hapa nazungumzia wale ambao wanashindwa kutoka kwenye uhusiano, ambao wanajua kabisa kwamba, unawatesa na kuwaumiza. Kuna sababu nyingi kwa nini watu hawa wanashindwa, lakini nyingine zinatokana tu na kutojua namna ya kutoka, sio utegemezi wa aina yoyote.
Moja ya sababu, ambazo ninaziona sana hasa kwa wanawake ni kujali jamii itasemaje. Mtu anaona kabisa uhusiano haufai na anatamani kutoka . lakini anajiuliza, hivi watasemaje? Kuna wakati ndugu wanamwambia, yeye ndiye mkorofi. Kama hii ndio sababu anachotakiwa kufanya mwanandoa ni kuhakikisha kwamba anajifunza kuishi kama yeye. Nijuavyo mimi, hata wanandugu au jamii hata ikisema vipi, anayeumia au kuepuka kuumia au kuuawa ni yule aliye kwenye mateso ya ndoa
Jambo la kujiliza hapa ni kama, jamii ndiyo inayopigwa, kutukanwa, kutelekezwa au kudhalilishwa? Lakini jambo kubwa zaidi la kufahamu ni kwamba mtu alishaolewa maana yake ni mtu mzima mwenye haki ya kuamua juu ya maisha yake. Akisubiri ndugu wamwamulie, basi huyo bado ni mtoto..
Jambo lingine ni lile la, je nikimwacha nitapata mwingine? kwani wanaume siku hizi ni shida sana? Ni ujinga unaowafanya wengi kuuliza swali hilo. Unahitaji mwingine wa nini? Unahitaji mwingine ili maisha yako yawe ya maana zaidi au? Kama hakuna mwingine ni vyema kwa sababu maana yake ni kwamba hakuna mwingine wa kukutesa. Lakini wanasaikolojia wanaamini kwamba, ‘kila bidhaa ina mnunuzi.’ Kama unataka mwingine, hata ukiwa na miaka sitini utampata. Huwezi kumpata wakati ukiwa ndani ya tanuru la mateso. Ni lazima utoke kwanza.
Kuna wale wanaoshindwa kutoka kwa sababu wanaamini kwamba mwanamke haruhusiwi kutoa talaka. Hi siyo kweli. Kuna wanaoshindwa kutoka kwa sababu dini zao zinakataza kuachana, hii pia siyo kweli. Mwanamke au mwanaume, yeyote anaweza kuomba talaka na ikatolewa, kama kuna sababu zenye kukidhi haja hiyo. Chombo pekee kinachoweza kutoa talaka au kuidhinisha wanandoa kuachana ni Mahakama, siyo dini au taasisi nyingine. Kinachoitwa ‘talaka tatu’ kwa mfano, ni ushahidi tu, na sio talaka.
Kuna wale ambao hawako tayari kutoka kwenye uhusiano mgumu kwa sababu ya mali. Wanaogopa watagawana mali na wenzao, jambo ambalo hawako tayari kulifanya na mara nyingi hawa ni wanaume. Wapo pia wanawake ambao wao ndio waliokuwa watafutaji wakuu. Swali la kujiuliza ni hili. ‘Ni kipi bora, ni mali au ni amani na utulivu na uhai wako?’ kama ni mali, basi hakuna anayeweza kukuingilia kwenye uamuzi wako.
Lakini, kwa ufahamu tu, ni kwamba, pasipo na amani, mali haina maana na pasipo na amani uhai ni wa kubahatisha pia.
Wengine wanashindwa kutoka kwenye husiano kwa sababu wazazi wa mume na ndugu wanampenda sana. Anaogopa kuwaudhi kwa kuondoka kwenye ndoa ya mateso ya mtoto wao na ndugu yao. Anataka wafurahi, hivyo hawezi kuondoka. Huu nao ni upungufu.
Hivi unakuwa umeolewa na ndugu na wazazi au na mume? Lakini, kwani ukiondoka utashindwa kuwa karibu na watu hawa? Hutashindwa na pengine urafiki wenu utakuwa wa kudumu. Ukiendelea kukaa kwenye ndoa ya mateso kuna siku utakosana hata na hawa, maana unaweza ukalipukwa ukamuuwa mtoto au ndugu yao.
Kuna wale wanaoshindwa kutoka kwenye uhusiano mgumu kwa sababu wana watoto na wanaogopa kwamba, watoto wao watateseka. Hivi ni kuteseka kupi kubaya, kule kwa utotoni au ukubwani? Mtoto anayeishi kwenye ndoa yenye vurugu, anaharibikiwa kuanzia utotoni hadi ukubwani. Lakini, hata hivyo kuachana kwa wazazi, sio lazima kuwe na maana ya watoto kuteseka.
Kuna wakati hata watoto wanamwambia mama atoke kwenye ndoa, halafu mama huyo huyo anadai anakaa kwenye ndoa hiyo kwa sababu ya watoto! Kuna haja ya kujiuliza maswali kwa upana zaidi.
Ukitaka kutoka kwenye ndoa ngumu jiulize maswali haya. Je, ndoa hii ni kwa faida ya nani? Je, niliolewa au kuoa ili kupata shida au amani na upendo? Je, bila ndoa,nisingeweza kuishi mwenyewe? Tafuta mifano ya wasio na ndoa ambao wanafurahia maisha.
Jiulize ni kwa kiasi gani wengine wanasaidia kukusukuma zaidi kwenye ndoa hiyo? Jiulize ukamilifu wako. Je, wewe ni nusu mtu au mtu kamili? Kama ni mtu kamili , basi ishi kama mtu kamili. TUONANE TENA PANAPO MAJALIWA JUMATANO IJAYO. UPENDO DAIMA!!

Wednesday, March 28, 2012

PIKINIKI MAKABURINI! Je ukimchungulia mtu mzima Utapofuka macho?

HAYA JAMANI NI ILI JUMATANO YETU YA KIPENGELE CHA MARUDIO MBALIMBALI NA PIA NI JUMATANO YA MWISHO YA MWEZI HUU. MADA KATIKA PITAPITA ZANGU NIKAKUTANO NA MADA HII SIO KWINGINE TENA BALI NIMEIPATA MAWAZONI KARIBUNI SANA.
Naamini mila na desturi zetu wabongo bado zina nguvu sana ingawa watu wanadai hizi ni zama ya bongo fleva. Naamini kuwa katika shule zetu za jadi mbinu mbalimbali zilitumika kuwezesha mambo fulani katika jamii kwenda shwari na kulindwa kwa nguvu zote na jamii. Mimi ni mchanganyiko wa Kipare na Kijita na katika makabila yote haya mawili njia za kuelimisha zilitumia mbinu nyingi ikiwa pia na vitisho. Mfano kwa Wapare maswala ya kufundishwa kuwa mwanamume wa shoka yaliendana na vitisho na maumivu. Kama wewe ni mwanamume basi lazima uweze kuvumilia maumivu .Nadhani kwa walioenda jando watakumbuka! Kulikuwa mpaka kuna simba wamsituni akumezaye ukishindwa kufanikisha mambo fulani ya kidume. Hii maana yake ulikuwa unauawa ingawa ilidaiwa umeliwa na Simba. Sasa njia hizi za kutufundisha heshima , maisha na hekima nyingine nyingi zikajakuuawa na wakoloni na wengine walioleta tamaduni mpya. Basi unaweza kudhani kwa sababu Wakoloni waliua shule za jadi basi na baadhi ya mambo tuliyokuwa tunatishiana yamekwisha!Utadhani mpaka sasa tumeweza kuelewa au hata kujiuliza ni kwanini mambo mengine yalitishalo kabila moja, hayalitishi jingine hata hivi sasa baada ya makabila ya Tanzania kuchanganyika na kutawanyika katika mikoa mbalimbali . Jibu bado tukopalepale. Tunaamini wachawi wanapaa na ungo ingawa hata kushuhudia hatuja shuhudia. Tunaamini kibibi fulani kichawi kwasababu macho yake mekundu bila kushuhudia aliyelogwa. Tuna chanja na kuvaa hirizi kibao bila ya uhakika hata wa ni nini hasa tunakiogopa. Sitaki kukataa kuwa hakuna uchawi kwa sababu hili ni jambo lililorekodiwa miaka mingi tu na vitabu vingi vimelizungumzia. Lakini mimi ninachoamini ni kwamba uchawi mkubwa ni hofu ya kibinadamu itokanayo naupungufu wa kibinadamu wakutokujua. Na upungufu huu kwa bahati mbaya hauna dawa. Upungufu huu umefanya wengine waabudu miti ili kuujazia, wengine Yesu, na Wengine Mtume Mohamedi. Tatizo jingine la upungufu huu uko kama njaa, kila siku unahitaji kupewa chakula ilikujazilizia pengo la upungufu wa kibinadamu ilikupata uhaueni. Mimi naamini pamoja na kuwepo wachawi, moto wa ahera na mambo yote hayo, lakini upungufu wa kibinadamu wenyewe hulenga binadamu kitofauti kutokana na binadamu mwenyewe alivyo na mazingira yake katika kumuelekeza binadamu huyu kuamini nini kinampa ujazo na uhaueni. Basi utakuta huku wanaogopa makaburi, kule wanaogopa mbuyu na hata wengine kukimbia vifuu vya nazi kutokana na mazingira yao. Basi unaweza ukakuta kutokana na mlengwa hirizi ikajazia na kuziba hofu hiyo, dini au hata kujinyonga. Naamini ubongo wa binadamu unanguvu kiasi kwamba hufanyia kazi hofu za binadamu na kuzipa uhai na uhalisi.Na naamini asilimia kubwa ya wajulikanao kama wachawi, waganga wa kienyeji au hata uchawi wenyewe haukuthibitika ingawa una uhalisi. Halafu si kweli zote ni zakufundisha maana nyingine ni zakutishana kwa madhumuni yakutishana tu.Na nyingi za mila na desturi hizi hatakama zilikuwa zinafundisha zamani hazina mchango mkubwa sasa hivi katika kuifundisha jamii ya leo.Na kama kuna sababu zakuzikubali hizi dini za kuletwa moja ni kwamba kwa sasa ndio zimeshikilia ukanda katika kuipa jamii muelekeo, ingawa hata kwa hili sina uhakika zitaweza jukumu hili mpaka lini kama jamii haifumbui macho nakuelewa mchango wake bila ya kukariri na kufuata kiulimbukeni. Lakini hizi mila za kutishana kwa dhumuni la kufundisha kitu haziko afrika pekee. Na rafiki yangu Myahudi alikuwa anatishwa na wazazi wake asiweke Tattoo kwa sababu hata weza kuzikwa kiyahudi akiwa na tattoo, kitu ambacho baadaye akagundua hakina ukweli. Nakumbuka pia nilipotembelea Russia mitaa ya Viborg nishawahi kuwatisha wenyeji wangu kwa kuwa nilipiga mluzi ndani ya nyumba na wao waliamini kabisa kwa kupiga mluzi ndani ya nyumba unaleta bomba la balaa. Kitu ambacho mimi siamini, kwani mimi nilifundishwa usipige miluzi porini. Hivyo hizi mila na desturi ambazo zina mambo haya ya kutishana haziko Afrika tu. Duh !Unakumbuka kitabu kiuzacho kuliko vyote siku hizi cha Harry Potter kinastori gani za kichawi?Sasa ngojea nikupe stori fupi kuhusu uoga wangu wa makaburi.Nakumbuka tokea utotoni nilizoea kusikia habari za kutisha kuhusu maeneo ya makaburini. Nakumbuka kunakipindi nilikuwa nang'ang'ania kutokwenda kulala mapema ilikuendelea kusikiliza stori za wakubwa, basi ilikutaka kunifanya niondoke wanaanza kusimulia stori za kutishatisha. Sehemu kubwa za stori hizi zilikuwa zinalenga maswala ya majini mashetanishetani na maeneo ya stori yanakuwa makaburini. Basi nisitake kukuongopea mara nyingi ilivyokuwa inaingia giza nilikuwa natishika kukatizia njia yoyote inayokatizia makaburini.Kilichokuja kunishinda ni pale nilipokuwa natembelea Upareni kwani kule ni kawaida kabisa marehemu kuzikwa katika eneo la nyumba. Sasa kutokana na kukulia mikoani ambako kunatamaduni za kuogopa maeneo ya makaruri ilinichukua muda kidogo kuzoe mpaka kuona ni kawaida.Kama nakumbuka vizuri Wachaga nao hawana uoga sana na makaburi hivyo nadhani kwa waogopa makaburi wanaweza kupata taabu sana uchagani na Upareni pia. Lakini akipata tabu Uchagani atatokwa na jasho akikatiza katika anga kama za Ufini ambako kuna mpaka siku katika mitaa ya krismasi ambapo makaburini ndio pakwenda sio kikilio bali kimatembezi. Mila na desturi zetu nyingi ni nzuri lakini hatuzisomi na kuzielewa sasa hivi tunapo ingia katika tamaduni za bongo fleva. Tatizo linalojitokeza ni kwamba mila nyingi nzuri zitapotea, halafu na zipo mila na desturi nyingi zisizo na manufaa sana kwetu tutaendelea kuzitunza. Bahati mbaya mila ambazo zitatunzika ni zile tuziogopazo! Je ukimchungulia mtu mzima utapofuka macho?Je , utakwenda pikiniki makaburini?

PANAPO MAJALIWA TUTAONANA JUMATANO NYINGINE TENA. KILA LA KHERI!!!!