Showing posts with label muziki. Show all posts
Showing posts with label muziki. Show all posts

Monday, March 29, 2010

Karibu kwenye ulimwengu wa Ku-blog kaka Renatus Kiluvia!!!




Mimi ni mwandishi wa habari na mtangazaji wa kituo cha redio cha 87.8 Ebony fm cha Iringa lakini mimi niko Dar-Mini Studio, naitwa Renatus Kiluvia,ni mmoja wa wafuatiliaji wazuri wa blog yako,naomba msaada wako wa kunitangazia blog yangu mpya http://www.muzikinamaisha.blogspot.com/ ,blog yangu inahusu muziki na maisha katika nyanja tofauti-tofauti,pia itahusika kuzungumzia burudani zingine kama filamu n.k.
Akhsante!!!!!!!!!!!

Friday, January 29, 2010

Napenda kuwatakia mwema wa juma hili pia ijumaa ya mwisho ya mwezi huu wa kwanza!!

Kunywa lakini kumbuka pombe si maji (na kumbuka kama utaendesha usinywe ugimbi mwingi)

Wazee na vijana wa kijiji cha kibaa wakicheza bao kama sehemu ya kupoteza muda baada ya kumaliza kazi.
Au ngoja tumsikilize Dada Saida Karoli ili wenye kuselebuka

Muwe na wakati mzuri wote

Friday, January 22, 2010

MZIKI NI MOJA YA MAISHA YETU LEO NGOJA TUMSIKILIZE DADA HUYO SOPHIA GEORGE!!



Mwaka ulikuwa 1992 kulikuwa na sherehe, katika ukumbi wa sherehe Wilima sec.school. EEhhh!! bwana we wacha watu wajimwage kwa mziki wa dada huyu. Kwa hiyo leo nimekumbumbuka sana Wilima-Matetereka na hasa siku ile. Ebu sikilizeni nawatakieni usikilizaji mwema na pia ikibidi uchezaji mwema. Muwe na wakati mzuri wa mwisho wa juma hili. Nataka kusema tuanza mwisho wa juma na muziki. TUTAONANA WAKATI MWINGINE!!!

Thursday, October 15, 2009

MUZIKI NI MOJA YA MAISHA TUMSIKILIZE DADA NURU LEO



Maisha yetu wengine hawawezi kuishi bila kusikiliza mziki hata siku moja na wengine hawawezi kusikiliza redio hata siku moja na wengine kusoma vitabu na magazeti. Kila mtu anapata habari kwa namna ya pekee. Haya leo nimeona tumsikilize Mwanablog mwenzetu Da Nuru the lihgt.!!!!