Showing posts with label ngono. Show all posts
Showing posts with label ngono. Show all posts

Wednesday, April 25, 2012

MWANAFUNZI AKUTWA AKIFANYA NGONO NA NGÓMBE WA JIRANI!!

Kwa vile ni siku ya KIPENGELE CHA MARUDIO YA MADA BASI TUENDELEE KUSOMA NA HII. Binafsi imenisikitisha sana.... na nimestaajabika mno.

Habari na Ezekiel Kamanga, Kyela

Mwanafunzi wa Kidato cha Kwanza katika Shule ya Sekondari Ikolo, Wilaya ya Kyela Bakiro Hance (18), amekutwa akifanya mapenzi na ng’ombe wa jirani yake.

Tukio hilo limetokea Machi 28 mwaka huu majira ya saa sita mchana katika Kijiji cha Ikolo ambapo mtuhumiwa alimchukua ng’ombe mmoja kati ya wawili wanaomilikiwa na Bwana Dickson Mwakimi, waliokuwa wamefungwa karibu na nyumba anayoishi mmiliki huyo.

Bwana Mwakimi alisikia ng’ombe wake akitoa sauti isiyo ya kawaida, kisha akatoka nje na kumkuta mwanafunzi huyo akifanya mapenzi na ng’ombe, ambapo alimkamata mwanafunzi huyo alimpeleka kwa mzazi wake aitwaye Bwana Hance, na mwanafunzi huyo alikiri kutenda kosa hilo ingawa hakuweza kueleza sababu zilizompelekea kufanya kitendo hicho cha aina yake.

Ameongeza kuwa mara kadhaa amekuwa akitenda tendo hilo na kwamba alijaribu kumkamata ng’ombe wa kwanza lakini alikuwa mkali hali iliyopelekea kushindwa kutimiza azma yake mwingine wa Bwana Mwakimi, ndipo alipoamua kumkamata ng’ombe wa pili na kumfunga kamba kwenye mti uliokaribu na kisha kuanza kufanya naye mapenzi.

Hata hivyo familia zote mbili za mmiliki wang’ombe na mwanafunzi zinaendelea kufanya mazungumzo ili kuondoa tofauti zilizojitokeza za tukio hilo la ajabu lililofanywa na mwanafunzi huyo.
via blogu ya ChimbukoLetu
-----------------------------------------------------------------
Najiuliza:- Ama kweli sijui sijui huyu kijana aliwaza nini?


Monday, June 1, 2009

JE? NI VIGUMU KUISHI BILA NGONO?

Wengi tunajua/pia tunajadili ukimwi na ngono, lakini tunahitaji kukumbuka kuwa sio waTanzania wote ama binadamu wote ni hivyo. Cha muhimu ni kuelewa kuwa ugonjwa huu unaua binadamu, na kwamba, hawa binadamu wanatokea katika kila sekta ya maisha, wanadini, wapagani, wasio na elimu, wenye elimu, wamjini, wanavijiji, nk.
Je? kuna ubaya gani kuwaelimisha wengine kuhusiana na matumizi ya ndomu?

Tukumbuke ya kwamba baada ya Hawa na Adam kula lile tunda baya, sote tulizaliwa madhambini, na tunashawishika kirahisi. Yaani, hata Hawa na Adam , ghafla waligundua ya kuwa wako uchi, nadhani mle bustanini kulikuwa kuzuri na kulikuwa na hewa bora yaani jua lilikuwa haliwachomi, majani hayakuwakata.Walipofukuzwa ndio walilazimika kuvaa nguo kwa sababu ya jua kali, mavumbi, miiba nk. Hakuna aliyewaamrisha kuvaa nguo.

Ngono inashawishiwa maishani kwa mbinu nyingi ambazo ni vipofu tu wasioziona. Katika magazeti, mavazi, sinema, hadithi za waliojaribu, umbea nk. Ni kama vile Hawa na Adamu, walivyoshawishika kula lile tunda hata walivyojua Mungu wao aliwakataza, lakini sisi wengine tunashawishika kirahisi kula hili tunda liitwalo "ngono". Wote tunajua tukishalionja tunda hata yeyote akikuambia "basi acha" wengi tunacheka ana kushangaa? Hii in kama vile mtoto akishaonja pipi, halafu ategemewe kutotamani pipi mbeleni.

Pipi zitakuwepo duniani kwa miaka mingi, vishawishi vya ngono vitakuwepo duniani kwa miaka mingi. Hii ndio sababu tunahitaji kuelimishwa kuwa pipi si nzuri kiafya. Lakini pia tunahitaji kuelimishwa kuwa wale watakao tamani basi wale nyingi na wasisahau kupiga mswaki. Naamaanisha, ujumbe wa kuacha ngono uambatane na ujumbe wa kupunguza kufanya ngono na watu wengi NA elimu ya kutumia ndomu.