Showing posts with label vyakula vya asili vitamu. Show all posts
Showing posts with label vyakula vya asili vitamu. Show all posts

Tuesday, April 26, 2016

NIMETAMANI SANA HIVI VYAKULA VYETU VYA ASILI/TULIVYOKUA NAVYO

 Nimekaa hapa nikiyafikiria matembele kwa ugali wa muhogo, lakini  duh  nimebaki kumezea mate tu...nikaanza kuota ndoto ya
...mahindi ya kuchoma hasa yale yanayochomwa moja kwa moja katika mkaa halisi wa kuni....mmmhhh maisha ....HAYA JAMANI KILA LA KHERI...PANAPO MAJALIWA...

Monday, September 14, 2015

VYAKULA VYETU VYA ASILI-----

Ulijua ya kwamba chakula kinachopikwa kwenye chungu ni kitamu sana kuliko kupika kwenye sufuria? Basi ngoja niwatakieni JUMATATU NJEMA NA PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA!

Tuesday, March 4, 2014

UTAMU WA VYAKULA VYA ASILI ..MABOGA, MAHINDI NA MAGIMBI

Asubuhi ya leo nimeamka huku nikiwa na hamu ya chakula hiki cha asubuhi. Maana huu ndio msimu wake hasa kwetu Songea maana ndio msimu wa mvua....mmmmhhh....halafu nikakumbuka ....

 ..mahindi jinsi mtu aendavyo tu shambani kukata/kuvunja mahindi na kwendajikono kuchoma au kuchemsha pamoja na maboga wakati huko nje mvua inanyesha..Ahhh nausikia utamu wake. Halafu nina kahadithi kamoja kuhusu mahindi  tulikuwa tunaitumia sana tulipokuwa wadogo inakwenda hivi:- Kila mtu anakuwa na muhindi, sasa wale wadogo huwa hawawezi kula basi wakubwa walikuwa wakiwaambia leta mimi nikutengenezee barabara ya kwenda ....anataja mji. Sasa yule mdogo aelewi anampa kumbe mwenzake yale mahindi atengenezayo barabara yote yanaingea tumboni ...Utoto bwana. Nilijaribu siku moja na wanangu, nilifanikiwa:-)...mmmhh ngoja niache  niwahi Madaba/matetereke

...maana ndiko nilikojifunza/onja mara ya kwanza Magimbi. Kwa hiyo leo nimekaa na kuota vyakula vingi. Natamani magimbi haya yawe mlo wangu wa mchana huu. Je kuna mlo ambao na wewe unautamani/hujala muda mrefu?

Tuesday, January 29, 2013

MILO AMBAYO NINGEPENDA SIKU YA LEO NILE NI HII HAPA...!!!

 
Chai ya rangi na ndizi mzuzu za kuchemsha
Mlo kama huu kwangu ni mali sana kuliko chai ya maziwa kwa mikate. Vyakula vyetu kama viazi, mihogo, magimbi na ndizi hakika jamani tuendelee kula kwanza unakula unashiba na halafu vina faida. Karibuni....na mchana...mmmmmhhh

 

Mchana, Nimekaa hapa naota mlo huu ugali, samaki, chuzi, mbogamboga na kachumbali kidogo bila kusahau pilipili... ila duh naona niishie kula kwa macho tu....au ...na jioni sijui itakuwaje ..hii ndiyo mara nyingi akina mama huwa tunawaza ili familia ipate chakula..tuna kazi kweli kweli......

Tuesday, August 21, 2012

NA MCHANA HUU NINGEPENDAA KUANDAA CHAKULA CHA AINA HII:- UGALI/WALI WA NAZI NA MBAAZI!!! LAKINI SASA MBAAZI NITAPATA WAPI?


WALI WA NAZI


 UGALI WA MAHINDI....
NA HAPA NI MBAAZI, Nimezikumbuka sana mbaazi.Kwa mimi ningependa wali kwa mbaazi lakini nimeona niweke na ugali maana kuna wengine wanapenda ugali...karibuni...

Friday, June 15, 2012

INAKARIBIA MCHANA NGOJA TU TUANGALIE VYAKULA MBALIMBALI KUTOKA TANZANIA LABDA UNAWEZA KUPATA WAZO NINI KUPIKA MCHANA HUU!!


NAWATAKIENI IJUMAA NJEMA SANA PIA MWANZO  WA KUANZA MAPUMZIKO UWE SALAMA. Najua wiki hii kwa wengi imekuwa na mikikimikiki mingi maana wengi sasa hasa wanafunzi wanaanza likizo (sommar lov) ...Labda nichukue nafasi hii pia kuwatakia wale wote ambao wapo LIKIZO..

Tuesday, August 16, 2011

VYAKULA VYA ASILI NA KINYWAJI CHA ASILI (TOGWA) AMBAVYO NIMEKULA NA KUNYWA WAKATI NIPO NYUMBANI SONGEA/RUHUWIKO!!!



Siku hii nilikuwa na furaha sana kwa kupata togwa kinywaji ambacho nakipenda sana, ila nasikitika sikuwa na kisonjo au kata (deve) ila hata hivyo ilipanda...:-)


Baadaye nikasema ni lazima nile karanga za kuchemsha kwa vile mimi si mpenzi wa mtesa wala mboga za kuweka karanga. Nipendacho ni karanga za kuchemsha au ziwe mbichi na halafu kukaanga hapa utanipatia...ni kweli nikazipata...nyumbani ni nyumbani......





Nilivyokuwa na bahati ulikuwa ni msimu wa viazi vitamu (mbatambata) au wengine wanasema makapa...basi nakwambia mikate, chapati, maandazi nk nikavitupilia mbali kabisa nikawa na vyangu nilivyovizoea tangu utoto...mihogo, ndizi na magimbi pia ingawa nilipitiwa kupiga picha kwa utamu:-) TUONANE TENA WAKATI MWINGINE ....!!!!!!


Friday, April 15, 2011

IJUMAA YA LEO: HEBU FIKIRIA MILO YETU HII YA ASILI, WANAODHARAU VYAKULA KAMA HIVI HAO WANA HASARA HASWA!!!

Najaribu kufikiria naamka asubuhi. Naingia shambani kuchuma boga, nalichemsha na halafu tayari kwa Chakula cha asubuhi. Yaani boga kwa chai ya rangi. Kwa mimi chai yangu kama kawaida bila sukari hapo nitafaidi na kulamba mikono. Na mchana ni ugali, samaki, mboga majani kidogo, mchuzi, maharagwe kinywaji maji. Mmmm!! yam yam yam!!utamu jamani ...karibuni tujumuike basi.... Jioni naona tubadili mboga, tutakula KISAMVU ..yaani hapa mimate hadi inanidondoka si mchezo ..karibuni sana jamani tufaidi uhondo huu... Picha hizi kutoka kwa kaka Mjengwa . IJUMAA NJEMA WANDUGU!!!