Showing posts with label wilaya ya Nyasa. Show all posts
Showing posts with label wilaya ya Nyasa. Show all posts

Monday, January 22, 2018

NYASA NI MAARUFU KWA KILIMO CHA MATUNDA

 
Hapa ni kijiji cha Ndengele katika wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma tulimkuta kijana anauza ndizi mkungu mzima shilingi 2000 tu.


Katika eneo la Liuli tulikuta mananasi matatu yanauzwa shilingi 1000.

NB; Albano Midelo

Thursday, February 18, 2016

BADO TUENDELEE NA WILAYA YA NYASA HAMU HAIJAISHIA ..BIO CAMP HII IPO KATIKA KIJIJI CHA NDEGERE KARIBUNI SANA...!

Mwenzenu bado nipo Nyasa kwangu...na hapa ni sehemu ya jengo la mapumziko katika ufukwe wa ziwa Nyasa kwenye  kijiji cha NDENGERE. Sehemu hiyo ni maarufu kwa jina la BIO CAMP.

Monday, February 15, 2016

WIKI HII TUANZE NA KUTEMBELEA ALIKOZALIWA KAPULYA WENU KIJIJI CHA LUNDO/ WILAYA YA NYASA


 Hapa ni kilimo cha maksai katika kijiji cha Lundo Wilaya ya Nyasa
Na hapa ni Beach ya BioCamp-Kijiji cha Ndengere Wilaya hiyo hiyo ya Nyasa...  yaani nimefurahi, furahi mno kupata tena taaswira ya vijiji hivi  Ndengere, Lundo, nk...ni sehemu zangu nilizokulia yaani  nimekumbuka  mengi sana hasa mlo wa samaki na ugali wa mhugo:-)  hapa ndipo nilikotoka...