Showing posts with label ufhaibuni. Show all posts
Showing posts with label ufhaibuni. Show all posts

Saturday, October 23, 2010

Sweden:- Kwanini iwe hivi?


MUUAJI ATINGISHA JIJI LA MALMÖ NCHINI SWEDEN

Kuna mlenga shabaha anae washuti wahamiaji wanaoshi nchini Sweden Katika jiji la Malmö. Mlenga shabah huyo hatari anachagua wageni tuu ndio anaowapiga risasi.

Mpaka sasa idadi ya waliolengwa imefikia 15 ndani ya siku tatu..
Hali imezikuwa kuwa tata na wasiwasi sio kwa wageni tuu hata Polisi vichwa vinawauma maana mpaka sasa hawajapata muelekeo maalum ukoje.

Katika Mkoa wa Skåne ndiko kilipo chama cha wasiopenda na wana idadi kubwa sana ya wanachama wao kuliko miji mingine ya Sweden..Kwa habari zaidi soma Aftonbladet.se
habari kutoka blog ya kaka Michuzi
Mdau wa Iceland.
Nami ngoja niongezee hapa:- Tunamwomba Mwenyezi Mungu mauaji yasizidi kutokea kwani sasa kila mtu ambaye si raia wa Sweden anaogopa hata kwenda nje, dukani hospital hata kupeleka watoto chekechea na hata kwenda kazini ni woga sana. Kwa kweli hili ni jambo la masikitiko sana na wengi wanajiuliza kwa nini? Pamoja Daima.