Matunda, tusisahau kula matanda jamani....kwa kawaida inatakiwa tule angalao kila siku matunda kama matano hivi. Lakini kwa bahati mbaya si wengi tuna nafsi ya kula hata tunda moja kwa siku. Na pengine wale wanye nafasi hawali. Jambo hili la kutokula matunda huhatarisha miili yetu kuto jengeka yaani vile virutubisho vya kuujenga mwili na kuuimarisha. kikinga. Na ndio hapo tunapojikuta miili yetu haina kinga za kutosha.
Wote tunajua mwili uwapo dhaifu ni rahisi sana kushambuliwa/kupatwa na maradhi hatari. Kama vile saratani, pia mboga majani nazo husaidia tuzile kwa wingi nazo pia. Kuna wakati unaweza kushangaa, kuona mtu anamaliza mwezi mzima hajala hata tunda moja. Tuchukue ule msimu wa machungwa, unaingia mpaka unaisha hajala hata chungwa moja. Ukija msimu wa maembe nao ni hivyo hivyo. Halafu utakuta maembe yanadondoka tu chini na kuoza na pia wengine wanayaokota na kulisha nguruwe. Au wanyama wengine lakini yeye mwenyewe anajisahau.
Wengi huona ya kwamba matunda siyo sehemu ya vyakula muhimu. Tuache tabia hii tule matunda na tuepukane na maradhi. Ukitaka kulifaidi tunda, basi kula pale ambapo tumbo lipo tupo/kabla hujala kitu chochote tanguliza matunda kwanza na baada ya nusu saa au saa moja, ndiyo unashauriwa ule mlo wako kamili.
NAWATAKIENI JUMAMOSI HII YA KWANZA YA MWEZI HUU WA TISA IWE NJEMA SANA!!!