.......ebu angalia hizo rangi na jinsi lilivyorembwa, nimelipenda mno . Swali sijui nami nitapendaza kama lilivyompendeza huyu dada?:-)
Showing posts with label heshima. Show all posts
Showing posts with label heshima. Show all posts
Thursday, March 15, 2012
NIMELIPENDA GAUNI HILI MNO....
.......ebu angalia hizo rangi na jinsi lilivyorembwa, nimelipenda mno . Swali sijui nami nitapendaza kama lilivyompendeza huyu dada?:-)
Saturday, October 15, 2011
MAJIBU KWA NDUGU MANGI NA KAKA SIMON KITURURU!!!
JUMAMOSI NJEMA WAPENDWA!!!!!
Friday, September 2, 2011
HAKUNA BINADAMU ALIYE MKAMILIFU!!
Habari jamani!
Leo nimeona si vibaya kama nikiongelea jambo hili, katika maisha kuna kupenda/kumpenda mtu na kuna kuchukia /kumchukia mtu. Yaani kumtendea mtu mema na kumtendea mabaya. Hii huwa inakuwa ni ngumu sana kwa sisi binadamu kusema /kutamka hili neno SAMAHANI/NISAMEHE. Basi mimi leo nimeona sina budi kuomba msamaha kwa yeyote yule ambaye nimemkosea/nilimkosea, nimemkwanza/nilimkwaza yule ambaye nilimwahidi jambo na sijaweza kulitimiza. Kwani naamini mimi pia ni binadamu na ni rahisi kukosa/kukosea. NISAMEHENI NDUGU ZANGUNI!
Habu TUENDELEE na WIMBO huu WA kaka BONNY mwaitege NISAMEHE....
TUPO PAMOJA DAIMA TUSISAHAU HILI NA WOTE MNAPENDWA!!!!IJUMAA NJEMA:-)
Leo nimeona si vibaya kama nikiongelea jambo hili, katika maisha kuna kupenda/kumpenda mtu na kuna kuchukia /kumchukia mtu. Yaani kumtendea mtu mema na kumtendea mabaya. Hii huwa inakuwa ni ngumu sana kwa sisi binadamu kusema /kutamka hili neno SAMAHANI/NISAMEHE. Basi mimi leo nimeona sina budi kuomba msamaha kwa yeyote yule ambaye nimemkosea/nilimkosea, nimemkwanza/nilimkwaza yule ambaye nilimwahidi jambo na sijaweza kulitimiza. Kwani naamini mimi pia ni binadamu na ni rahisi kukosa/kukosea. NISAMEHENI NDUGU ZANGUNI!
Habu TUENDELEE na WIMBO huu WA kaka BONNY mwaitege NISAMEHE....
TUPO PAMOJA DAIMA TUSISAHAU HILI NA WOTE MNAPENDWA!!!!IJUMAA NJEMA:-)
Friday, January 14, 2011
MAVAZI YA WANAWAKE
Nimelipenda shairi hili kwani linasema ukweli limeandikwa na Katekista Rafael Mlelwa katika gazeti la Mwenge:-
Natembea natazama, ni hali ya kushangaza,
Mitaani akina mama, mambo wanayoigiza,
Wengine watuwazima, inakuwaje nawaza,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Vazi la Mtanzania, tangu kale heshima,
Watu walijivunia, wa lika zote nasema,
Haya nawasimulia, walivaa akina mama,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Suruali mwavalia, mfanane na wazungu,
Asili mwaikimbia, mnanitia uchungu,
Watu wote angalia, mnamdharau Mungu,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Vimini mwajibalia, mwana kama vikatuni,
Nyingine mnapasua, makusudi mapajani,
Mapaja twaangalia, pia na nguo za ndani,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Siketi taiti pia, mitaani mwavalia,
Hiyoni ya kulalia, maungo yaoneshea,
Mitaani mwatembea, watu kwa kuangalia,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Kweli mwatia karaha, moyoni nasononeka,
Singerendi mwavalia, maziwa yanaonekana,
Mitaani mnahaha, kutwa nzima mwazunguka,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Kwa umbo mmeumbika, kwa uzuri asilia,
Uarabu mwautaka, tena kwa kujichubua,
Kama Mungu angetaka, mngekuwa Saudia,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Wengine watu wazima, tena ni wake za watu,
Watoto wenu lazima, watawaigeni tu,
Malazi yao lazima yatakuwa yenye kutu,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Hapa mimi nasimama, naomba mnisikie,
Wanamama wenye hekima, hali hii tukemee,
Hakika mimi nasema, tena isiendelee,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Natembea natazama, ni hali ya kushangaza,
Mitaani akina mama, mambo wanayoigiza,
Wengine watuwazima, inakuwaje nawaza,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Vazi la Mtanzania, tangu kale heshima,
Watu walijivunia, wa lika zote nasema,
Haya nawasimulia, walivaa akina mama,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Suruali mwavalia, mfanane na wazungu,
Asili mwaikimbia, mnanitia uchungu,
Watu wote angalia, mnamdharau Mungu,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Vimini mwajibalia, mwana kama vikatuni,
Nyingine mnapasua, makusudi mapajani,
Mapaja twaangalia, pia na nguo za ndani,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Siketi taiti pia, mitaani mwavalia,
Hiyoni ya kulalia, maungo yaoneshea,
Mitaani mwatembea, watu kwa kuangalia,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Kweli mwatia karaha, moyoni nasononeka,
Singerendi mwavalia, maziwa yanaonekana,
Mitaani mnahaha, kutwa nzima mwazunguka,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Kwa umbo mmeumbika, kwa uzuri asilia,
Uarabu mwautaka, tena kwa kujichubua,
Kama Mungu angetaka, mngekuwa Saudia,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Wengine watu wazima, tena ni wake za watu,
Watoto wenu lazima, watawaigeni tu,
Malazi yao lazima yatakuwa yenye kutu,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Hapa mimi nasimama, naomba mnisikie,
Wanamama wenye hekima, hali hii tukemee,
Hakika mimi nasema, tena isiendelee,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Saturday, April 18, 2009
MAVAZI YA WANAWAKE
Nimelipenda shairi hili kwani linasema ukweli limeandikwa na Katekista Rafael Mlelwa katika gazeti la Mwenge:-
Natembea natazama, ni hali ya kushangaza,
Mitaani akina mama, mambo wanayoigiza,
Wengine watuwazima, inakuwaje nawaza,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Vazi la Mtanzania, tangu kale heshima,
Watu walijivunia, wa lika zote nasema,
Haya nawasimulia, walivaa akina mama,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Suruali mwavalia, mfanane na wazungu,
Asili mwaikimbia, mnanitia uchungu,
Watu wote angalia, mnamdharau Mungu,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Vimini mwajibalia, mwana kama vikatuni,
Nyingine mnapasua, makusudi mapajani,
Mapaja twaangalia, pia na nguo za ndani,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Siketi taiti pia, mitaani mwavalia,
Hiyoni ya kulalia, maungo yaoneshea,
Mitaani mwatembea, watu kwa kuangalia,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Kweli mwatia karaha, moyoni nasononeka,
Singerendi mwavalia, maziwa yanaonekana,
Mitaani mnahaha, kutwa nzima mwazunguka,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Kwa umbo mmeumbika, kwa uzuri asilia,
Uarabu mwautaka, tena kwa kujichubua,
Kama Mungu angetaka, mngekuwa Saudia,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Wengine watu wazima, tena ni wake za watu,
Watoto wenu lazima, watawaigeni tu,
Malazi yao lazima yatakuwa yenye kutu,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Hapa mimi nasimama, naomba mnisikie,
Wanamama wenye hekima, hali hii tukemee,
Hakika mimi nasema, tena isiendelee,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama-
Natembea natazama, ni hali ya kushangaza,
Mitaani akina mama, mambo wanayoigiza,
Wengine watuwazima, inakuwaje nawaza,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Vazi la Mtanzania, tangu kale heshima,
Watu walijivunia, wa lika zote nasema,
Haya nawasimulia, walivaa akina mama,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Suruali mwavalia, mfanane na wazungu,
Asili mwaikimbia, mnanitia uchungu,
Watu wote angalia, mnamdharau Mungu,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Vimini mwajibalia, mwana kama vikatuni,
Nyingine mnapasua, makusudi mapajani,
Mapaja twaangalia, pia na nguo za ndani,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Siketi taiti pia, mitaani mwavalia,
Hiyoni ya kulalia, maungo yaoneshea,
Mitaani mwatembea, watu kwa kuangalia,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Kweli mwatia karaha, moyoni nasononeka,
Singerendi mwavalia, maziwa yanaonekana,
Mitaani mnahaha, kutwa nzima mwazunguka,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Kwa umbo mmeumbika, kwa uzuri asilia,
Uarabu mwautaka, tena kwa kujichubua,
Kama Mungu angetaka, mngekuwa Saudia,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Wengine watu wazima, tena ni wake za watu,
Watoto wenu lazima, watawaigeni tu,
Malazi yao lazima yatakuwa yenye kutu,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.
Hapa mimi nasimama, naomba mnisikie,
Wanamama wenye hekima, hali hii tukemee,
Hakika mimi nasema, tena isiendelee,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama-
Friday, December 5, 2008
UNDUGU WA NAMNA TOFAUTI KWA MANUFAA YA JAMII
Nitajaribu kidogo kuelezea Ninakotoka mimi vipi tunaitana
Babu - Bibi
Upande wa mama
Mama
Mama mdogo, mdogo wa mama
Mama mkubwa, dada yake mama
Mjomba kaka ya mama
Upande wa baba
Baba
Baba mdogo, mdogo wake baba
Baba mkubwa, kaka yake baba
Shangazi, dada yake baba.
VIPI KUITANA
Watoto wa mama mkubwa na mdogo
Wa kike nitamwita dada au kama ni mdogo basi mdogo wangu
Wa kiume nitamwita kaka hata kama ni mdogo
Watoto wa mjomba ni binamu zangu
Watotot wa baba mkubwa na mdogo
Wa kiume nitamwita kaka naye ataniita dada
Wa kike nitamwita dada, naye ataniita mdogo wake inategemea nani mkubwa
Watoto wa Shangazi ni binamu zangu
Watoto wa kaka zangu wataniita mimi Shangazi na watoto wa wadogo zangu wa kike wataniita mimi mama mkubwa.
Watoto wa binamu wataniita mimi mama na kaka zangu baba.
Mama na baba yangu watawaita watoto wangu wajukuu na wao watawaita wazazi wangu babu na bibi.
Watoto wangu watawaita kaka zangu wajomba
Bibi ya mama/baba yangu mimi nitamwita mama na babu ya mama/baba nitamwita baba.
Naomba kama nimesahau kitu basi tusaidiane.
Sasa nina maswali:- Je? mke wa mjomba ni mjomba pia? na je? mume wa shangazi ni shangazi pia?
Babu - Bibi
Upande wa mama
Mama
Mama mdogo, mdogo wa mama
Mama mkubwa, dada yake mama
Mjomba kaka ya mama
Upande wa baba
Baba
Baba mdogo, mdogo wake baba
Baba mkubwa, kaka yake baba
Shangazi, dada yake baba.
VIPI KUITANA
Watoto wa mama mkubwa na mdogo
Wa kike nitamwita dada au kama ni mdogo basi mdogo wangu
Wa kiume nitamwita kaka hata kama ni mdogo
Watoto wa mjomba ni binamu zangu
Watotot wa baba mkubwa na mdogo
Wa kiume nitamwita kaka naye ataniita dada
Wa kike nitamwita dada, naye ataniita mdogo wake inategemea nani mkubwa
Watoto wa Shangazi ni binamu zangu
Watoto wa kaka zangu wataniita mimi Shangazi na watoto wa wadogo zangu wa kike wataniita mimi mama mkubwa.
Watoto wa binamu wataniita mimi mama na kaka zangu baba.
Mama na baba yangu watawaita watoto wangu wajukuu na wao watawaita wazazi wangu babu na bibi.
Watoto wangu watawaita kaka zangu wajomba
Bibi ya mama/baba yangu mimi nitamwita mama na babu ya mama/baba nitamwita baba.
Naomba kama nimesahau kitu basi tusaidiane.
Sasa nina maswali:- Je? mke wa mjomba ni mjomba pia? na je? mume wa shangazi ni shangazi pia?
Subscribe to:
Posts (Atom)