Showing posts with label Swali. Show all posts
Showing posts with label Swali. Show all posts

Thursday, September 22, 2016

SWALI... UNADHANI HUYO KWENYE PICHA NI NANI NA YUPO WAPI?


TUTAONANA TENA MAJALIWA NA KAMA BASI NIWATAKIENI MWISHO WA JUMA UWE MWEMA...



Monday, June 20, 2016

SWALI KUTOKA KWA MSOMAJI WA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO

Habari za leo ndugu zanguni...nimetumiwa huu ujumbe kwa barua pepe yangu..nimeona ni kheri niweke hapa kibarazani ili tusaidiani maana kwenye wengi pana mengi. Karibu tumsaidie huyo dada................................................................

Habari,  mimi ni dada ninayeishi Iringa nina umri wa miaka 18 kwa bahati mbaya mpenzi wangu amenipa mimba na kutokana namna alivyo baba yangu Naamini akifahamu kwamba nina mimba ataniua Kwani mimi ni mwanafunzi.
Nimeongea na mchumba wangu tumekubaliana tukaitoe.
Hata hivyo bado najiuliza kama kutoa mimba  ni kitu sahihi? Na je, nifanyeje Kwani nipo kwenye njia panda.

Thursday, September 3, 2015

SWALI NILILOULIZWA NA MSOMAJI /MFUATILIAJI WA MAISHA NA MAFANIKIO:-

Swali lenyewe lipo hivi:- Hivi ni  kitu gani akina mama/wanawake kinawafanya wampende mtoto fulani zaidi kati ya watoto wao wa kawazaa?
Akaendelea:- Utamkuta mama ana watoto wanne, lakini anampenda mmoja zaidi ya wengine? Hii inakuwaje kwa upande wako? akanipa hili swali mimi......akaendelea nakuuliza kwa kuwa nadhani una watoto.....halafu akaendelea kusema ....Pia nadhani utakuwa umeshawahi kuisikia hii au inatokea.
Jibu langu lilikuwa kama ifuatavyo:- Binafsi kama mama nawapenda wanangu sawasawa na sijawahi kufikiria  KUWAPENDA  TOFAUTI.
Baadaye nikakumbuka kwanini niwashirikishe ninyi wasomaji/ ndugu zangu. Maana naamini palipo na wengi pana mengi
Hata hivo nami nikajiwa na swali:- Je?  Hiki kitu kipo? na kama kipo kwa akina mama/wanawake tu?  na sio akina baba/wanaume? Maana nao pia ni wazazi. NAOMBA TUJADILI KWA PAMOJA......Kapulya wenu!

Friday, July 17, 2015

SWALI/WAZO LA LEO!

Kama kungekuwepo na ndoto za kununua, je? Ni ndoto gani wewe ungenunua?

Thursday, April 23, 2015

DUH KAAAZI KWELIKWELI HAPA SIJUI MWALIMU ATAJIBU NINI???

Nimeipenda hii  angalia mwal. jinsi jasho linavyomtoka kwa kutafuta jibu. Watoto huwa wakweli sana na hawaoni aibu kuuliza swali....KILA LA KHERI.

Wednesday, November 12, 2014

SWALI LA LEO KUTOKA MAISHA NA MAFANIKIO A.K.A KAPULYA....

N imekuwa nikijiuliza kila siku na sijapata jibu, sasa leo nimeona niliweke  hapa kwani palipo na wengi hapaharibiki neno,   Ni hili hapa swali lenyewe:- Hivi kwa nini pilipili inamfanya/tufanya tupige chafya? Najua mtasema mbona kuna vingi vyatufanya kupiga chafya, lakini mimi naona pilipili ni zaidi.....naomba tujadili kwa kupamoja. JUMATANO NJEMA!!!

Wednesday, August 13, 2014

SWALI /TAFAKARI LANGU/YANGU LA/YA LEO ....NAOMBA TUTAFAKATI PAMOJA

Swali langu la leo:- Hivi tusemapo  NI MTU NA MJOMBA WAKE au Ni MTU NA SHANGAZI YAKE.
 JE? kati ya hao  MTU NI NANI NA MJOMBA/SHANGAZI  NI YUPI?
HAYA KILA LA KHERI  TUPO PAMOJA.....Kapulya wenu.

Monday, November 25, 2013

TUANZA JUMATATU HII NA SWALI HILI KUTOKA KWA KAKA BWAYA ...KUHUSU MAISHA NA FURAHA!!!

Kama mnakumbuka mwezi uliopita niliweka picha hii hapa kibarazani na baadaye kulitokea na maoni. Na baadhi ya maoni aliyotoa msomaji mmoja ambaye ni kaka Bwaya ambaye alikuwa ameadimika kwa muda mrefu na sasa yupo nasi tena. Nachukua nafasi hii kumkaribisha Kaka Bwaya......Haya na maoni yenyewe yalisomeka hivi;-
Bwayasaid...
Tafiti zinaonyesha kuwa watu waishio katika maisha yanayoonekana kuwa duni, ndio wenye furaha zaidi. Mfano ni hawa. Swali: kwa nini? Naomba tusaidiane kujadili swali hili kwa pamoja....JUMATATU NJEMA!!!

Tuesday, September 17, 2013

UJUMBE /SWALI WA/LA LEO!!!

Kama huwezi kujisamehe mwenyewe na uliyoyafanya, utawezaje kuwasamehe wengine?
NAWATAKIENI WOTE JUMANNE NJEMA SANA NA KUMBUKENI TUPO PAMOJA DAIMA!!!Kapulya!

Thursday, August 15, 2013

NAOMBA TAFSIRI YA NENO KIONGOZI/VIONGOZI...MAANA LINANIKERA MNO.......!!!

Nimeamka leo nikiwaza hili neno KIONGOZI/VIONGOZI nikashindwa kuliwazua nikaamua kuchukua KAMUSI  SANIFU YA KISWAHILI CHETU. Nayo ikaniambia hivi:-KIONGOZI/VIONGOZI.....
1. mtangulizi wa jambo fulani au wa kikundi cha watu, mkubwa anayesimamaia shughuli maalumu kwa kueleza au kuelekeza. AU...
2. Kitu kinachosaidia kuonyesha au kuelekeza......
Je? hawa viongozi wanaongoza kweli au wanajiongoza? Naomba tutafakari au jadili kwa pamoja.
Ndimi Kapulya wenu:-)

Tuesday, July 23, 2013

SWALI LILILONISUMBUA SIKU YA LEO...!!!!

Nimeamka asubuhi hii na nimemshukuru Mungu kwa kunilinda. Nikaona ngoja ninyooshe viungo:- Yaani nikaende nje kama kawaida yangu kukimbia, nimekimbia, nimekimbia mara nikakutana na mkimbaji mwingine naye kawaza kama mimi anakimbia. Sasa hapa kitu kilichonipa swali ni kwamba mdada huyu alikuwa akikimbia na mbwa wake ambaye amemfunga kamba shingoni. Swali likanijia huyu dada ana uhakika kama huyu mbwa/kambwa anataka kukimbia? Maana niliona kama mbwa mwenyewe hata hakufurahia. Nikataka kusimama na kumuuliza.....lakini nikaacha. Muda wote nilipokuwa nakimbia swali lilizidi kunisumbua hivi kweli yule mbwa alipenda kukimbia?  Na pia nikazidi kuwaza....Nikaona niwape na wenzangu haka kakisa....TUSITENGANE TUWA  TUNAKUMBUKANA. PAMOJA DAIMA SIKU NJEMA. KAPULYA!!

Tuesday, October 16, 2012

KWANINI KUNA MAHINDI YA NJANO NA MAUPE?

 MAHINDI YA NJANO....
Na hapa ni mahindi MEUPE ambayo mimi binafsi nimeyazoea tangu nilipokuwa katoto kadogo. Ndiyo, nimewahi kuona mahindi mekundi meusi au mchanganyiko lakini hayo ya njano sijawahi kuona Tanzania yetu. Je? kwanini?

Tuesday, June 5, 2012

KWANINI PILIPILI MBUZI INAITWA HIVYO? NA JE KWA NINI HIKI CHOMBO ZA KUKUNIA NAZI PIA CHAITWA MBUZI?

Pilipili mbuzi zikiwa kwenye mti jee unajua kwanini zina itwa Pilipili Mbuzi? ni kwa kuwa zina faa sana kwenye supu ya Nyama ya Mbuzi au?
N ahap ni mbuzi mwenyewe , sioni kama kuna mfanano hapa...
 ...na hapa sasa ni kifaa cha kukunia nazi nacho kinaitwa MBUZI . Mara chache nimesikia wengine wakisema kikunio au je kuna jina jingine ambalo mimi sijawahi kulisikia...naamini kwa pamoja tutafika pahala pazuri. Mchana,jioni au sijui usiku mwema....KAPULYA



Monday, May 21, 2012

BAADA YA MAPUMZIKO NIMEONA TUANZA JUMATATU HII KIHIVI!!!

Ni matumaini yangu kuwa wengi wetu  twnajua/twakumbuka hapa ni wapi. Labda tu niuliza Je? unajua hapa ni wapi?...Nawatakieni mwanzo wa juma hili uwe mwema.

Tuesday, April 24, 2012

SWALI HILI LIMENIKERA SANA:- MAJINA YA SAMAKI YANATOKA WAPI???

HAPA NI SAMAKI AINA YA MAGEGE
Ni muda mrefu sana nimekuwa nikijiuliza kuhusu majina ya samaki. Juzijuzi nilikuwa nikiangalia habari/pragramu kuhusu ziwa Nyasa, ziwa Viktoria na Tanganyika. Nikakumbuka majina ya samaki kama vile :- Kambale, Mbofu, Mbelele/sengefu, Magege, Vitui, Vindogo, Mbasa nk. Nikawa najuiliza hivi ni maeneo ya ziwa nyasa tu tunawaita hawa samaki hivi au? Na kama ni hivi nani aliwapa samaki hawa haya majini? Sikupata jibu...nikaona niliweke hapa kibarazani  hili swali. Kama nisemavyo/nijuavyo palipo na wengi hapaharibiki kitu. Tuwe pamoja katika kamjadala haka

Friday, March 30, 2012

SWALI LA WIKI HII!!!!

Umewahi kufanya maamuzi magumu sana kwenye maisha yako? ilikuwa ni kuhusu nini?haya funguka sasa!
NAWATAKIENI WOTE KILA LA KHERI NA MUWE NA MUDA MZURI NDANI YA MWISHO WA JUMA HILI LA MWISHO WA MWEZI HUU WA TATU.UPENDO DAIMA.

Tuesday, January 31, 2012

ULIKUWA UNAJUA MATUNDA HAYA YANAITWA MABUNGO?.....

......na yanapatikana ZANZIBAR. Je? kuna anayejua kama yanapatikana sehmu nyingine? kuna dada mmoja alikuwa huko na alionja na akayapenda. Binafsi sijawahi kuonja. Natumaini nitapata jibu kwani nimeulizwa swali hilo na nimeshindwa kujibu na nikaona hapa nitapata tu jibu..Natanguliza shukrani....

Monday, January 23, 2012

TUANZE JUMATUTA KIHIVI:-JE? NI PICHA GANI AMBAYO IMEVUNJA REKODI MWAKA 2011 KATIKA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO?

Ni ombi kutoka kwa dada Mija:-"Ombi..tuongezee ile juu kwenye page yako ya blogu, ulovaa tisheti ya njano, sketi nyeupe na mkanda wa kipepeo.."


mwaka 1992 Wilima (Matetere) Madaba



Picha hii nilipiga mwaka 2008 mwezi wa sita



Na hii nilipiga mwa jana 2011 mwezi wa kumi....




...............hii pia mwaka jana mwezi wa kumi na mbili kijapani:-)



Hii ni ya mwaka huu 4/1 2012




Saturday, January 7, 2012

NIMEULIZWA SWALI HILI NA BINTI YANGU....

Ilikuwa mwaka jana siku ya Noeli ...Binti yangu Camilla akaniuliza:- Mama, hivi kwa nini Yesu alizaliwa tarehe 25/12..Lakini, kipindi cha Pasaka huwa tuna sema kuwa Yesu anakufa, kwa nini ile tarehe ya kufa huwa haiwi ileile kila mara? Je kuna Yesu wangapi?...Mmmhhh!! hapa nikawa natafakari na sijapata jibu na leo nimeona niombe msaada hapa kibarazani kwani palipo na wengi huwa hakiharibiki kitu....

Tuesday, December 13, 2011

HATA MIGUU NAYO HUPENDEZESHWA!!!! SWALI JE NI VIBAYA?



Vikuku ni urembo au?


KUNA mtu kanitumia hiyo picha anauliza hizo shanga za miguuni zinavaliwa kujiremba au zina maana nyingine?Kwa mujibu wa maelezo yake, amewahi kusikia kwamba, shanga hizo a.k.a vikuku zina maana yake hivyo anaomba kufahamu kama ni kweli. Anasema, kaelezwa kwamba, kikuku kikivaliwa mguu wa kulia ina maana yake, na kikivaliwa kushoto kinakuwa na maana nyingine, ni kweli?Kama kila mguu una maana yake, vikivaliwa miguu yote inamaanisha nini?


Pia nimesikia nchi kama Ivory Cost ukivaa mguu wa kulia basi inaonyesha kuwa wewe ni msagaji /shoga. Je ni kweli?