SWALI:- Je? ni nchi gani/zipi haina/hazini herufi A katika bara la Afrika?
NAWATAKIA KILA LA KHERI. PAMOJA DAIMA!!!
Showing posts with label changamoto. Show all posts
Showing posts with label changamoto. Show all posts
Monday, May 19, 2014
Monday, March 17, 2014
EBU JUMATATU HII YA LEO TUANZE NA MSEMA HUU CHEKA UNENEPE:- VICHEKESHO VYETU!!
Katika kuhakikisha wanafunzi wa darasa la kwanza wanaelewa, mara nyingi walimu hutumia mifano mingi sana, nakumbuka baba yangu alivyokuwa akitupatia mifano mingi ili tuelewe...haya fuatana nami na mahojiano yafuatayo ambayo mwalimu alikuwa anajitahidi kuwaelewesha wanafunzi wake:-
Mwalimu:- Nikikupa chapati sita halafu ukala mbili zitabaki chapati Ngapi?
Mwanafunzi:- Ukinipa na chai ya maziwa haitabaki hata chapati moja.
HAYA NIKUTAKIE JUMATATU NJEMA SANA NA PANAPO MAJALIWA TUTACHEKA TENA JUMATATU IJAYO:-)
Mwalimu:- Nikikupa chapati sita halafu ukala mbili zitabaki chapati Ngapi?
Mwanafunzi:- Ukinipa na chai ya maziwa haitabaki hata chapati moja.
HAYA NIKUTAKIE JUMATATU NJEMA SANA NA PANAPO MAJALIWA TUTACHEKA TENA JUMATATU IJAYO:-)
Thursday, October 3, 2013
ZILIPENDWA...UNAWAFAHAMU WATU HAWA AU UNAJUA HAPA NI WAPI?
Wametulia hapo bila wasiwasi inaonekana ni mahali pazuri na penye utulivu...Haya karibuni kufumbua fumbo la leo....:-) Sijui itakuwa mwaka gani hapa????
Thursday, October 20, 2011
NGOJA LEO TUPATE CHANGOMOTO KIDOGO!!
Ni hivi:- Maria na kaka yake mdogo aitwaye Juma wanataka tuhesabu miaka /umri wao. Juma anasema ukizidisha umri wangu mara mbili halafu jumlisha jawabu na umri wa Maria na pia zidisha mara mbili, jawabu litakuwa 7148.
Na Maria naye anasema ukizidisha umri wangu mara mbili halafu jumlisha na jawabu la umri wa Juma pia zidisha mara mbili, jawabu litakuwa 5274. Je? Maria ana umri gani? na Juma ana umri gani?....Nawatakieni kila la kheri kwa changamoto hii pia Alhamis njema....Kapulya.
Na Maria naye anasema ukizidisha umri wangu mara mbili halafu jumlisha na jawabu la umri wa Juma pia zidisha mara mbili, jawabu litakuwa 5274. Je? Maria ana umri gani? na Juma ana umri gani?....Nawatakieni kila la kheri kwa changamoto hii pia Alhamis njema....Kapulya.
Tuesday, June 14, 2011
Friday, May 20, 2011
Changamoto ya ijumaa ya leo!!!
Nimetumiwa ujumbe huu kutoka kwa msomaji wa Maisha na Mafanikio ambaye ni mkazi wa Njombe. Pia naweza nikamwita kama kaka yangu kwa jina anaitwa Salehe Msanda. Sitaki kuwa mchoyo nimeona ni vema nikiweka hapa ili tusaidiane kwa pamoja kwani kwenye wengi ni pazuri. Pia umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Kaka Salehe alianza kama ifuatavyo:-
-------------------------------------------------------------------------------------
Dada Yasinta naomba tusaidiane katika suala hili lifuatalo
Kwanini tulio wengi tu wazito wa kuthubutu katika nyanga fulani za msingi na muhimu kwa ustawi wa mtu mmojammoja, familia na jamii kwa ujumla?. Mfano tu-wagumu wa kuwekeza kwa ajili ya kuweza kupata mahitaji yetu ya msingi katika maisha ya kila siku (chakula, mavazi, malazi na uhakika wa afya zetu) au kubadilika kutoka katika mazoea yanayohatarisha ustawi wa familia na jamii na familia, lakini tu wepesi wa kuthubutu na kutenda mambo yanayohatarisha maisha na ustawi wa mtu na jamii.
Nini kifanyike kuibadili hali hii hasa kwa sisi waTanzania? Maana nionavyo mimi katika hii dunia ya UFAHAMU NA MAARIFA, wakati wenzetu wanaendelea kugundua mambo mapya kila siku sisi tumejikita zaidi katika burudani na starehe.
Kuna umuhimu wa kukumbushana katika kuifuta lugha ongozi ya kipindi au zama hizi za ufahamu na maarifa ambayo ni kuwa na taarifa na maarifa kadiri ya uwezo wetu.
Ijumaa njema!!!!!!!
-------------------------------------------------------------------------------------
Dada Yasinta naomba tusaidiane katika suala hili lifuatalo
Kwanini tulio wengi tu wazito wa kuthubutu katika nyanga fulani za msingi na muhimu kwa ustawi wa mtu mmojammoja, familia na jamii kwa ujumla?. Mfano tu-wagumu wa kuwekeza kwa ajili ya kuweza kupata mahitaji yetu ya msingi katika maisha ya kila siku (chakula, mavazi, malazi na uhakika wa afya zetu) au kubadilika kutoka katika mazoea yanayohatarisha ustawi wa familia na jamii na familia, lakini tu wepesi wa kuthubutu na kutenda mambo yanayohatarisha maisha na ustawi wa mtu na jamii.
Nini kifanyike kuibadili hali hii hasa kwa sisi waTanzania? Maana nionavyo mimi katika hii dunia ya UFAHAMU NA MAARIFA, wakati wenzetu wanaendelea kugundua mambo mapya kila siku sisi tumejikita zaidi katika burudani na starehe.
Kuna umuhimu wa kukumbushana katika kuifuta lugha ongozi ya kipindi au zama hizi za ufahamu na maarifa ambayo ni kuwa na taarifa na maarifa kadiri ya uwezo wetu.
Ijumaa njema!!!!!!!
Sunday, January 3, 2010
NILILAZIMIKA KUCHUKUA MAAMUZI MAGUMU
Ni furaha isiyo kifani kutumiwa barua kama hii na ukizingatia ndio mwaka umeanza tu. Kwa vile napenda kugawana na wasomaji wengine wa blog hii na pia wanablog wenzangu nimeona niufikishe ujumbe huu:- Karibuni sana KUSOMA hapa.
Kwako dada Yasinta, ni matumaini yangu kuwa umzima wewe na familia yako huko uliko.
Dada mimi ni msomaji wa blog yako na nimejifunza mengi sana kupitia blog yako hii ya maisha, kwani mijadala unayoianzisha katika blog yako imekuwa ikileta changamoto na migongano ya mawazo kiasi kwamba nimekuwa nikijifunza mambo mengi kupitia mijadala hiyo.
Kusema kweli nimekuwa ni mfuatiliaji wa blog yako na kupitia blog yako hiyo ya MAISHA nimekuwa nikijifunza mambo mengi juu ya maisha na mafanikio pia.
Mimi ninao uzoefu wangu ambao ningependa uuweke katika blog yako ili wasomaji waweze kujifunza kupitia uzoefu wangu huu.
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 37 na nina mke na watoto watatu. Kikazi mimi ni mtumishi serikalini na mke wangu by Professional ni mpishi na pia anao ujuzi kidogo wa ushonaji. Mke wangu alikuwa na ndoto za kumiliki biashara ya Catering wakati namuoa kwa sababu aliwahi kufanya kazi kwa mtu mwenye biashara hiyo alipokuwa kwao Mbeya kabla sijamuoa na kuhamia naye Dar, hivyo alitengetengeneza picha kuwa biashara ya Catering ndio biashara pekee yenye faida kubwa.
Ni kweli kuwa biashara ya Catering ina faida kubwa lakini inategema na mtaji utakaoanzishia biashara hiyo. Kusema ukweli nilikuwa na dhamira ya kumuanzishia biashara hiyo ya Catering na nilianza mchakato wa kutekeleza azma yangu, lakini nikakutana na vikwazo vingi sana, kwani ili kuanzisha biashara hiyo ni lazima uwe na vifaa kama Serving Dishes, maturubai, viti na meza, vyombo vya kupikia, sahani, vifaa vya Mziki na MC. Kama ukimudu kuwa na vitu hivyo basi na faida yako itakuwa kubwa kwani shuguli utakazokuwa unapata zitakuwa ni kubwa na zenye kulipa faida kubwa. Kwa mfano hapa Dar shughuli kama harusi, Send Off, Kitchen Party, Misiba, na kumaliza misiba wengine huita kumaliza arobaini, Vipa imara achilia mbali semina ndogo ndogo za kidini na za NGO’s, zote hizo ni kazi ambazo zinategemea sana watu hawa wa Catering, lakini kutokana na mtaji wangu kuwa mdogo nikajikuta nikikwama kwa sababu nilikuta vifaa hivyo vinauzwa ghali kutokana na watu wengi kukimbilia biashara hiyo kwa kuwa inalipa.
Nilikata shauri kumfungulia biashara nyingine ili japo asikae bure bila kazi na pia kuokoa hizo pesa tusije tukazifuja bure. Kwa haraka, niliamua kuanzisha biashara ya ushonaji, pamoja na uuzaji wa vifaa vya ushonaji.
Awali nilipata upinzani mkubwa sana kwa mama watoto na hakupenda hilo wazo langu kabisa, nilipata wakati mgumu sana kumuelimisha mpaka akakubali lakini hakuwa na mwamko wa kuipenda kazi hiyo. Sikukata tamaa, niliendelea kumuelimisha huku nikiendelea kununua vifaa kama vyerehani vitatu na ya kudarizi kimoja pamoja na vifaa vya ushonaji vya kuweka dukani kwa ajili ya kuuza na vifaa vingine muhimu kama makabati nakadhalika na kulifungua duka hilo rasmi. Hata hivyo nilimuahidi kuwa ahadi yangu iko pale pale, nitamfungulia biashara yake ya Catering kama nilivyomuahidi wakati ukifika.
Hata hivyo mwanzoni hakuipenda biashara hiyo na nilikuwa kama vile namlazimisha kwenda dukani kufungua kila siku asubuhi, lakini sikukata tamaa.
MSHANGAO………..
Dada siku za karibuni biashara ikaanza kukua na wateja wakaanza kuja kwa wingi kununua bidhaa, na mtaji umeanza kukua sasa. Hivi karibuni katika mazungumzo yangu na yeye nikamwambia kuwa mpaka mwezi wa pili mwakani nitakuwa nimemfungulia biashara yake ya Catering kama nilivyoahidi, ili ndoto yake itimie, lakini kwa mshangao aliruka na kukataa kabisa kuwa hataki tena biashara ya Catering kwani ile biashara ya ushonaji ina faida na ameipenda sana.
Sikuamini masikio yangu. Unajua wakati nabishana naye kuhusu kuanzisha biashara ya ushonaji nilidhani yeye yuko sahihi kuwa hiyo biashara haifai, na ilikuwa nusura nikubaliane naye, ila kuna kitu huwa tunaita machale au mlango wa sita wa fahamu, ambao huwa nautumia katika kufanya maamuzi magumu.
Baada ya kutafakari sana niliamua kufungua hiyo biashara, na sasa nimepata jibu kuwa nilikuwa sahihi, maana ameuona ukweli kuwa wazo langu lilikuwa ni sahihi. Kuna msemo mmoja unasema kuwa mwanaume ni kichwa cha nyumba, ki ukweli sikuwa nauzingatia huo msemo kwa kuwa niliona ni dalili ya kujikweza na kuwadhalilisha wanawake, lakini nadhani hiyo dhana ina ukweli fulani.
Nimejifunza jambo moja, kuwa kuna wakati mwanaume analazimika kuwa dikteta ili kufikia maamuzi fulani magumu, hasa pale mke anapoonekana kupinga bila kutoa wazo mbadala au kutoa ushauri.
Sio kwamba wanawake hawawezi kutoa ushauri au wazo zuri, la hasha, ninachomaanisha hapa ni kwamba kuna wakati kunapohitajika maamuzi magumu, mume anatakiwa kupewa nafasi ili aamue. Ila inategemea tabia za mume huyo.
Inasemwa kuwa nyuma ya mafanikio ya mume kuna mke na nyuma ya anguko la mume kuna mke pia, lakini huwa najiuliza, je utamjuaje mke ambaye maamuzi yake yanakupeleka shimoni?
NAWATAKIENI JUMAPILI HII YA KWANZA YA MWAKA 2010 IWE YA FURAHA TELE!!
Kwako dada Yasinta, ni matumaini yangu kuwa umzima wewe na familia yako huko uliko.
Dada mimi ni msomaji wa blog yako na nimejifunza mengi sana kupitia blog yako hii ya maisha, kwani mijadala unayoianzisha katika blog yako imekuwa ikileta changamoto na migongano ya mawazo kiasi kwamba nimekuwa nikijifunza mambo mengi kupitia mijadala hiyo.
Kusema kweli nimekuwa ni mfuatiliaji wa blog yako na kupitia blog yako hiyo ya MAISHA nimekuwa nikijifunza mambo mengi juu ya maisha na mafanikio pia.
Mimi ninao uzoefu wangu ambao ningependa uuweke katika blog yako ili wasomaji waweze kujifunza kupitia uzoefu wangu huu.
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 37 na nina mke na watoto watatu. Kikazi mimi ni mtumishi serikalini na mke wangu by Professional ni mpishi na pia anao ujuzi kidogo wa ushonaji. Mke wangu alikuwa na ndoto za kumiliki biashara ya Catering wakati namuoa kwa sababu aliwahi kufanya kazi kwa mtu mwenye biashara hiyo alipokuwa kwao Mbeya kabla sijamuoa na kuhamia naye Dar, hivyo alitengetengeneza picha kuwa biashara ya Catering ndio biashara pekee yenye faida kubwa.
Ni kweli kuwa biashara ya Catering ina faida kubwa lakini inategema na mtaji utakaoanzishia biashara hiyo. Kusema ukweli nilikuwa na dhamira ya kumuanzishia biashara hiyo ya Catering na nilianza mchakato wa kutekeleza azma yangu, lakini nikakutana na vikwazo vingi sana, kwani ili kuanzisha biashara hiyo ni lazima uwe na vifaa kama Serving Dishes, maturubai, viti na meza, vyombo vya kupikia, sahani, vifaa vya Mziki na MC. Kama ukimudu kuwa na vitu hivyo basi na faida yako itakuwa kubwa kwani shuguli utakazokuwa unapata zitakuwa ni kubwa na zenye kulipa faida kubwa. Kwa mfano hapa Dar shughuli kama harusi, Send Off, Kitchen Party, Misiba, na kumaliza misiba wengine huita kumaliza arobaini, Vipa imara achilia mbali semina ndogo ndogo za kidini na za NGO’s, zote hizo ni kazi ambazo zinategemea sana watu hawa wa Catering, lakini kutokana na mtaji wangu kuwa mdogo nikajikuta nikikwama kwa sababu nilikuta vifaa hivyo vinauzwa ghali kutokana na watu wengi kukimbilia biashara hiyo kwa kuwa inalipa.
Nilikata shauri kumfungulia biashara nyingine ili japo asikae bure bila kazi na pia kuokoa hizo pesa tusije tukazifuja bure. Kwa haraka, niliamua kuanzisha biashara ya ushonaji, pamoja na uuzaji wa vifaa vya ushonaji.
Awali nilipata upinzani mkubwa sana kwa mama watoto na hakupenda hilo wazo langu kabisa, nilipata wakati mgumu sana kumuelimisha mpaka akakubali lakini hakuwa na mwamko wa kuipenda kazi hiyo. Sikukata tamaa, niliendelea kumuelimisha huku nikiendelea kununua vifaa kama vyerehani vitatu na ya kudarizi kimoja pamoja na vifaa vya ushonaji vya kuweka dukani kwa ajili ya kuuza na vifaa vingine muhimu kama makabati nakadhalika na kulifungua duka hilo rasmi. Hata hivyo nilimuahidi kuwa ahadi yangu iko pale pale, nitamfungulia biashara yake ya Catering kama nilivyomuahidi wakati ukifika.
Hata hivyo mwanzoni hakuipenda biashara hiyo na nilikuwa kama vile namlazimisha kwenda dukani kufungua kila siku asubuhi, lakini sikukata tamaa.
MSHANGAO………..
Dada siku za karibuni biashara ikaanza kukua na wateja wakaanza kuja kwa wingi kununua bidhaa, na mtaji umeanza kukua sasa. Hivi karibuni katika mazungumzo yangu na yeye nikamwambia kuwa mpaka mwezi wa pili mwakani nitakuwa nimemfungulia biashara yake ya Catering kama nilivyoahidi, ili ndoto yake itimie, lakini kwa mshangao aliruka na kukataa kabisa kuwa hataki tena biashara ya Catering kwani ile biashara ya ushonaji ina faida na ameipenda sana.
Sikuamini masikio yangu. Unajua wakati nabishana naye kuhusu kuanzisha biashara ya ushonaji nilidhani yeye yuko sahihi kuwa hiyo biashara haifai, na ilikuwa nusura nikubaliane naye, ila kuna kitu huwa tunaita machale au mlango wa sita wa fahamu, ambao huwa nautumia katika kufanya maamuzi magumu.
Baada ya kutafakari sana niliamua kufungua hiyo biashara, na sasa nimepata jibu kuwa nilikuwa sahihi, maana ameuona ukweli kuwa wazo langu lilikuwa ni sahihi. Kuna msemo mmoja unasema kuwa mwanaume ni kichwa cha nyumba, ki ukweli sikuwa nauzingatia huo msemo kwa kuwa niliona ni dalili ya kujikweza na kuwadhalilisha wanawake, lakini nadhani hiyo dhana ina ukweli fulani.
Nimejifunza jambo moja, kuwa kuna wakati mwanaume analazimika kuwa dikteta ili kufikia maamuzi fulani magumu, hasa pale mke anapoonekana kupinga bila kutoa wazo mbadala au kutoa ushauri.
Sio kwamba wanawake hawawezi kutoa ushauri au wazo zuri, la hasha, ninachomaanisha hapa ni kwamba kuna wakati kunapohitajika maamuzi magumu, mume anatakiwa kupewa nafasi ili aamue. Ila inategemea tabia za mume huyo.
Inasemwa kuwa nyuma ya mafanikio ya mume kuna mke na nyuma ya anguko la mume kuna mke pia, lakini huwa najiuliza, je utamjuaje mke ambaye maamuzi yake yanakupeleka shimoni?
NAWATAKIENI JUMAPILI HII YA KWANZA YA MWAKA 2010 IWE YA FURAHA TELE!!
Subscribe to:
Posts (Atom)