Showing posts with label wasukuma. Show all posts
Showing posts with label wasukuma. Show all posts
Friday, October 19, 2012
LEO TUWATEMBELEE NDUGU ZETU WASUKUMA HUKO MWANZA NA UTAMADUNI WAO WA ASILI
NAWATAKIENI WOTE MWISHO WA JUMA UWE MWEMA SANA...
Friday, April 8, 2011
MAJINA YETU/LEO TUANGALIE MAJINA YA KISUKUMA!!!
Kuna wakati niliwahi kuandika kuhusu majina/vibongo vya wangoni. Kwa kujikumbusha zaidi au kwa wale waiowai kusoma basi ingia hapa .Utaona hayo majina na pia maoni ya watu. Na sasa leo katika upekuzi wangu nimekutana na majina ya wenzetu Wasukuma ebu angalia hapa napo, majina haya nimeyapata Jamii Foum.
Majina ya Kisukuma
1. Masanja Mawenge 2.N'kwabi N'gwanakilala 3.Rupondije Inuka 4.Mabula Nkwimba 5.Nyeunge Maneno 6.Budodi Nzobhe ya Siketi JidulamabambasiN'gwanangwa Masabhuda, Masumbuko, Wangaluke, Nchimika, Ng'wana Malundi, shindike Bunani Jidalu, Jidiku ikong'oro, Igunani Matanda, Isungangwanda Kidalu, 6: Sawaka Ng'wana gandila, Itendegu Jibinza, Shija, Mabura, Kasase, Nzungu, Midelo, Lufulo Ndama Nyangwaka Ndili, Lisolilo Ligasu, Kaswalala Buyonzi, Nyanzobe Mayunga, Ngw'ana Nh'wani, Jodoki Mpembele, Ngwizukulu jilala, nyanzala ng'wandu, mwanasabuni lushanga, manyilizu shiganga, kabadi madilisha, mashenene masagida, chenge saguda, pula kiheka, tabu lukelesha, ngasa ingombe, masanja malale, malila lushumbu, luhende mwanansale, Ngosha Magonya, Manyanza, Jongh'ela, Nkulukulu, Ngw'alali, Ngh'ungulu, Zanzui, Sanagu, Shushu. TUKUTANE TENA WAKATI MWINGINE!!!!!! IJUMAA NJEMA KWA WOTE!!!!
Friday, September 26, 2008
JAMII YA WASUKUMA!
MAANA YA NENO WASUKUMA Wasukuma ni mkusnyiko wa makundi madogomadogo kutoka maeneo jirani , na kwamba kundi kubwa zaidi likiwa limetoka Kusini mwa eneo hili la mkoa wa Mwanza.Jina hili limetokana na neno SUKUMA maana yake wa lugha ya Kisukuma na Kinyamwezi KASKAZINI, yaani moja wapo wa ya pande nne a dunia yetu. Wanyamwezi ambao lugha yao inafanana sana na Kisukuma hutuita sisi tulio Kaskazini mwao "Bhasukuma" yaani watu wa KASKAZINI. Nasi huwaita "Bhadakama" yaani watu wa KUSINI.
Tangu siku zote, wasukuma na wanyamwezi walijulikana kuwa wao ni "Bhantu" na kutokana na neno hilo kumekuja kujulikana kundi linaloitwa WABANTU. Kundi hili mara zote limetambulikana kwa lugha wanayozungumza ya KIBANTU. Hivyo, Wanyamwezi, Wakimbu hadi Wabemba walioko Zambia ni kundi kubwa la wabantu kufuatia lugha wanazozungumza.
Taarifa zingine kuhusu chimbuko la wasukuma kutoka kwenye mtandao wa internet…kwenye anwani hii.www.mwanzacommunity.com.org
Tangu siku zote, wasukuma na wanyamwezi walijulikana kuwa wao ni "Bhantu" na kutokana na neno hilo kumekuja kujulikana kundi linaloitwa WABANTU. Kundi hili mara zote limetambulikana kwa lugha wanayozungumza ya KIBANTU. Hivyo, Wanyamwezi, Wakimbu hadi Wabemba walioko Zambia ni kundi kubwa la wabantu kufuatia lugha wanazozungumza.
Taarifa zingine kuhusu chimbuko la wasukuma kutoka kwenye mtandao wa internet…kwenye anwani hii.www.mwanzacommunity.com.org
Katika picha mwenye koti jeusi ndiye mzee mwenye miaka 114 ajulikanaye kama Mzee mtalimbo. Ni mganga wa kienyeji ana wake 7 watoto 14 na wajukuu 82. Mtoto wake wa kwanza ana mika 72.
Hii ni nyumba ya mzee mtalimbo ndani pia ni maazi ya nyuki ambao ni mali yake.
Subscribe to:
Posts (Atom)

