Dunia hii sasa ni hatari kweli. Mtu na akili zake kabisa anathubutu kumfanyia unyama mtoto wa mwenzie. Kiasi cha kumpa mimba na kuzaa mtoto mapema. Kabla ya wakati wake wa kuzaa haujafika. Inaonekana huku tunakoelekea sasa ni hatari tupu au ni kweli labda ni mwisho wa dunia.
Showing posts with label mimba. Show all posts
Showing posts with label mimba. Show all posts
Thursday, October 8, 2009
Wednesday, September 16, 2009
WANAFUNZI WA KIKE WAPATAO MIMBA KABLA YA KUMALIZA SHULE WARUHUSIWA KUFANYA MTIHANI
Nimezoea sana kusikiliza habari za BBC, kwa hiyo wakati nasikiliza habari hii, nikaona sio mbaya kama nikiiweka hapa kibarazani kwangu ili wengi msome na tuweze kujadiliana.
Idadi ya wanafunzi wa kike wanaoacha shule kwa sababu ya mimba isiotarajiwa inazidi kupanda
IDADI ya wasichana wanaokatisha masomo yao na kuacha shule wilayani Kericho, kwa sababu ya kupachikwa mimba wasiotarajia imewashangaza maafisa wa Elimu na wadau wengine.
Katika kisa ambacho kimezua mjadala mkubwa juu ya Elimu na mimba miongoni mwa wanafunzi wa kike, imeibuka kuwa toka kwa idadi ya wasichana 25 waliojiunga katika kidato cha kwanza katika shule moja katika eneo hilo, 24 waliacha shule baada ya kutwikwa mimba.
Katika makala ya wiki hii tunahoji nini kinachopelekea hali kama hii ya mimba za mapema miongoni mwa wanafunzi???? Mwalimu mkuu alizungumzia umbali wa shule kuoka kwa makao ya wanafunzi ambao wanalazimika kupitia katika misitu ya chai jambo amabalo linawaweka katika hatari ya mahusiano ya kimapenzi na hata ubakaji.
Mwalimu huyo mkuu alisema ni jambo la kushangaza sana. Aliongezea kuwa idadi ya waichana katika shule hio sasa ni ishirini pekee. Wengi wa wasichana waliokuwa wakifanya vyema katika masomo wameacha shule baada ya wanafunzi wenzao na baadhi ya wafanyakazi katika mashamba ya chai kuwatwika mimba.
Elimu ya watoto wa kike inaendelea kuwa ndoto isioweza kutimika katika eneo hili la Afrika. Wasichana wengi wanadanganywa na wanaume na kujitosa katika tabia na mahusiano ya kingono yanayopelekea mimba isiotarajiwa. Jambo ambalo huwafanya wasichana hawa kuacha shule na kuanza maisha ya uzazi wakiwa wao wenyewe bado wachanga.
Wengine wanakumbwa na vizingiti vya kitamaduni kama vile tohara ya wanawake, ndoa za mapema, kazi za nyumbani, magonjwa na umasikini. Kumekuwa na mjadala iwapo kuratibishwa kwa masomo ya afya ya uzazi katika silabasi za shule kutaksaidia kudhibiti mimba isiotarajiwa na magonjwa ya zinaa miongoni mwa wanafunzi.
Inchini Tanzania serikali, kwa mara ya kwanza, imewaruhusu wale waliopata mimba wakiwa shuleni kufanya mitihani. Hapo awali wanafunzi waja wazito walikuwa wakikatazwa kufanya hivyo.
Je, nini mchango wako kuhusu yote haya??????
Habari zaidi sikiliza hapa katika kipengele cha kimasomaso. http://www.bbc.co.uk/swahili/
Idadi ya wanafunzi wa kike wanaoacha shule kwa sababu ya mimba isiotarajiwa inazidi kupanda
IDADI ya wasichana wanaokatisha masomo yao na kuacha shule wilayani Kericho, kwa sababu ya kupachikwa mimba wasiotarajia imewashangaza maafisa wa Elimu na wadau wengine.
Katika kisa ambacho kimezua mjadala mkubwa juu ya Elimu na mimba miongoni mwa wanafunzi wa kike, imeibuka kuwa toka kwa idadi ya wasichana 25 waliojiunga katika kidato cha kwanza katika shule moja katika eneo hilo, 24 waliacha shule baada ya kutwikwa mimba.
Katika makala ya wiki hii tunahoji nini kinachopelekea hali kama hii ya mimba za mapema miongoni mwa wanafunzi???? Mwalimu mkuu alizungumzia umbali wa shule kuoka kwa makao ya wanafunzi ambao wanalazimika kupitia katika misitu ya chai jambo amabalo linawaweka katika hatari ya mahusiano ya kimapenzi na hata ubakaji.
Mwalimu huyo mkuu alisema ni jambo la kushangaza sana. Aliongezea kuwa idadi ya waichana katika shule hio sasa ni ishirini pekee. Wengi wa wasichana waliokuwa wakifanya vyema katika masomo wameacha shule baada ya wanafunzi wenzao na baadhi ya wafanyakazi katika mashamba ya chai kuwatwika mimba.
Elimu ya watoto wa kike inaendelea kuwa ndoto isioweza kutimika katika eneo hili la Afrika. Wasichana wengi wanadanganywa na wanaume na kujitosa katika tabia na mahusiano ya kingono yanayopelekea mimba isiotarajiwa. Jambo ambalo huwafanya wasichana hawa kuacha shule na kuanza maisha ya uzazi wakiwa wao wenyewe bado wachanga.
Wengine wanakumbwa na vizingiti vya kitamaduni kama vile tohara ya wanawake, ndoa za mapema, kazi za nyumbani, magonjwa na umasikini. Kumekuwa na mjadala iwapo kuratibishwa kwa masomo ya afya ya uzazi katika silabasi za shule kutaksaidia kudhibiti mimba isiotarajiwa na magonjwa ya zinaa miongoni mwa wanafunzi.
Inchini Tanzania serikali, kwa mara ya kwanza, imewaruhusu wale waliopata mimba wakiwa shuleni kufanya mitihani. Hapo awali wanafunzi waja wazito walikuwa wakikatazwa kufanya hivyo.
Je, nini mchango wako kuhusu yote haya??????
Habari zaidi sikiliza hapa katika kipengele cha kimasomaso. http://www.bbc.co.uk/swahili/
Wednesday, September 24, 2008
MJADALA WA LEO
Hili swali limekuwa likinikereketa sana miaka yote ambayo nimeishi hapa duniani kwa hiyo sasa naomba mwenzangu tujadiliana au mnipe jibu.
SWALI NDIO HILI:- Je? Kuna sheria Tanzania isemayo kama msichana akipata mimba asiendelee na masomo?
SWALI NDIO HILI:- Je? Kuna sheria Tanzania isemayo kama msichana akipata mimba asiendelee na masomo?
Subscribe to:
Posts (Atom)
