Kwa nini ni rahisi kuwa na furaha?
Kwa nini uchungu ni mzito?
Kwa nini kuna furaha kidogo?
kwa nini kuna uchungu zaidi?
Au kwa sababu tunathamini/pendezwa na furaha wakati tunapofikiwa na furaha?
Au kwa vile tunayanyenyekea maisha?
Au kwa vile tunalazimika kucheka?
Au Labda kwa vile tunalazimika kulia?
SIKUNJEMA KWA WOTE
Showing posts with label uchungu. Show all posts
Showing posts with label uchungu. Show all posts
Thursday, April 30, 2009
Tuesday, April 14, 2009
MAISHA YA BINADAMU YANA UTAMU NA UCHUNGU WAKE
Maisha ni yenye ladha ya aina yake. Kwa upande mmoja maisha hayo ni yenye ladha ya utamu na upande mwingine yana ladha ya uchungu na ukakasi. Utamu au uchungu wa maisha hutokana na mambo kadha wa kadha ambayo hutokea maishani.
Maisha huwa na ladha ya utamu pale mtu anapokuwa mwenye siha njema, maelewano mema na wengine, mafanikio katika maisha, hali njema kiuchumi nk. Maisha hayohayo hubadili ladha yake pale mambo yanapokuwa magumu na kukuendea kombo. Ugumu huo wa maisha hutokea pale mtu anapokuwa katika afya mbaya,katika majonzi, msiba, mahusiano mabaya na wengine, kuwa katika mfadhaiko na kushindwa katika mambo mbalimbali ya maisha. Pia mambo mengine yanayosababisha ladha ya maisha kwa amani na upendo katika nchi, vita, hali ya ukimbizi nk.
Mambo kama hayo na mengine ya mtindo huo husababisha maisha kuonekana magumu kubadili ladha yake. Pia yanapomkabili mtu katika nafasi yake mtu huyo hushikwa na mfadhaiko na kusongwa nafsi yake hatimaye hupatwa na jakamoyo na kukata tamaa ya kuishi.
Katika ulimwengu tunaoishi kuna fujo tele. Fujo hizo husababisha ladha ya maisha kuchachuka. Ladha hiyo huyafanya maisha yaonekanane kuwa magumu na yenye kukatisha tamaa. Sasa hivi kuna vilio mbalimbali kutoka kona zote za dunia vitokanavyo na mwenendo wa maisha. Sio mara moja tunasikia redioni na kusoma katika magazeti juu ya kumomonyoka kwa maadili. Kuna maonevu mengi ambayo sasa yanaelekea kwenye kuhalalishwa kama sehemu ya maisha ya kisasa.Ubakaji leo hii umekuwa tu kama hadithi za kuburudisha. Utoaji wa mimba unaoendana bega kwa bega na utupaji wa watoto ni kama vitendewili vya kutengwa na kutegeliwa.
Dunia yetu imetawaliwa na vita na magomvi yasiyo kifani. Vita hivyo husababisha maafa, hali ya ukimbizi na shida nyingine za aina aina. Mfano mzuri ni vita vile vya Demokrasia ya Kongo ilivyosababisha lukuki ya wakimbizi. Tena yapo magonjwa ambayo hayana tiba na ambayo husababisha vifo visivyo na idadi kila siku. Magonjwa hayo huwafanya watu kukosa raha ya kuishi.
Tatizo sugu la madawa ya kulevya linazidi kuota mizizi, pamoja na vyombo vya dola kupiga vita dhidi ya mambo haya ya madawa ya kulevya, wahusika wameziba masikio, hawasikii na wala hawaelewi kitu. Kadiri wanavyozidi kutafuta mbinu za kupunguza au kuthibiti ndiyo kadiri hiyo hiyo biadhara inavyoshika kasi yake. Aidha, matukio ya vifo vya watu wanaojinyonga au kujiua wenyewe kutokana na mifadhaiko ya maisha waipatayo yanazidi siku hadi siku. Ukienda mjini, nako ongezeko la vichaa ni kubwa kiasi cha kutishia amani. Hali ya uchumi nayo huzidi kuwa ngumu siku hadi siku. Wenye uwezo wanazidi kujilimbikizia mali na makabwela wanazidi kudidimia. Rushwa tatizo sugu linazidi kupenyeza zaidi, watoa na wapokea rushwa ni wengi. Katika mtumbwa wa rushwa wako mameneja, madaktari, polisi, wakuu wa vyuo, makarani na hata wangoja malango, hapa ni baadhi tu. Bila rushwa huwezi kupata huduma. Haki iko wapi?
Mambo hayo na mengine mengi ya mtindo huo yanakatisha tamaa ya kuishi. Mtu wa kwanza kukatishwa tamaa ni kijana ambaye ndio kwanza anayaibukia maisha. Kijana anapoibukia maisha anakuwa na ndoto nyingi sana. Matarajio yake hutegemea namna gani ulimwengu utampokea. Lakini sasa anapokumbana na mambo ya aina hiyo ambayo yanakatisha tamaa, kijana anabadilika kabisa na kuwa kama vile hana akili nzuri. Hayo ni masumbuko, mateso, adha na kero kwa walio wengi. Siku za matumaini haziji bali bughudha nyingi zinazidi kila siku.!!!!!!
Maisha huwa na ladha ya utamu pale mtu anapokuwa mwenye siha njema, maelewano mema na wengine, mafanikio katika maisha, hali njema kiuchumi nk. Maisha hayohayo hubadili ladha yake pale mambo yanapokuwa magumu na kukuendea kombo. Ugumu huo wa maisha hutokea pale mtu anapokuwa katika afya mbaya,katika majonzi, msiba, mahusiano mabaya na wengine, kuwa katika mfadhaiko na kushindwa katika mambo mbalimbali ya maisha. Pia mambo mengine yanayosababisha ladha ya maisha kwa amani na upendo katika nchi, vita, hali ya ukimbizi nk.
Mambo kama hayo na mengine ya mtindo huo husababisha maisha kuonekana magumu kubadili ladha yake. Pia yanapomkabili mtu katika nafasi yake mtu huyo hushikwa na mfadhaiko na kusongwa nafsi yake hatimaye hupatwa na jakamoyo na kukata tamaa ya kuishi.
Katika ulimwengu tunaoishi kuna fujo tele. Fujo hizo husababisha ladha ya maisha kuchachuka. Ladha hiyo huyafanya maisha yaonekanane kuwa magumu na yenye kukatisha tamaa. Sasa hivi kuna vilio mbalimbali kutoka kona zote za dunia vitokanavyo na mwenendo wa maisha. Sio mara moja tunasikia redioni na kusoma katika magazeti juu ya kumomonyoka kwa maadili. Kuna maonevu mengi ambayo sasa yanaelekea kwenye kuhalalishwa kama sehemu ya maisha ya kisasa.Ubakaji leo hii umekuwa tu kama hadithi za kuburudisha. Utoaji wa mimba unaoendana bega kwa bega na utupaji wa watoto ni kama vitendewili vya kutengwa na kutegeliwa.
Dunia yetu imetawaliwa na vita na magomvi yasiyo kifani. Vita hivyo husababisha maafa, hali ya ukimbizi na shida nyingine za aina aina. Mfano mzuri ni vita vile vya Demokrasia ya Kongo ilivyosababisha lukuki ya wakimbizi. Tena yapo magonjwa ambayo hayana tiba na ambayo husababisha vifo visivyo na idadi kila siku. Magonjwa hayo huwafanya watu kukosa raha ya kuishi.
Tatizo sugu la madawa ya kulevya linazidi kuota mizizi, pamoja na vyombo vya dola kupiga vita dhidi ya mambo haya ya madawa ya kulevya, wahusika wameziba masikio, hawasikii na wala hawaelewi kitu. Kadiri wanavyozidi kutafuta mbinu za kupunguza au kuthibiti ndiyo kadiri hiyo hiyo biadhara inavyoshika kasi yake. Aidha, matukio ya vifo vya watu wanaojinyonga au kujiua wenyewe kutokana na mifadhaiko ya maisha waipatayo yanazidi siku hadi siku. Ukienda mjini, nako ongezeko la vichaa ni kubwa kiasi cha kutishia amani. Hali ya uchumi nayo huzidi kuwa ngumu siku hadi siku. Wenye uwezo wanazidi kujilimbikizia mali na makabwela wanazidi kudidimia. Rushwa tatizo sugu linazidi kupenyeza zaidi, watoa na wapokea rushwa ni wengi. Katika mtumbwa wa rushwa wako mameneja, madaktari, polisi, wakuu wa vyuo, makarani na hata wangoja malango, hapa ni baadhi tu. Bila rushwa huwezi kupata huduma. Haki iko wapi?
Mambo hayo na mengine mengi ya mtindo huo yanakatisha tamaa ya kuishi. Mtu wa kwanza kukatishwa tamaa ni kijana ambaye ndio kwanza anayaibukia maisha. Kijana anapoibukia maisha anakuwa na ndoto nyingi sana. Matarajio yake hutegemea namna gani ulimwengu utampokea. Lakini sasa anapokumbana na mambo ya aina hiyo ambayo yanakatisha tamaa, kijana anabadilika kabisa na kuwa kama vile hana akili nzuri. Hayo ni masumbuko, mateso, adha na kero kwa walio wengi. Siku za matumaini haziji bali bughudha nyingi zinazidi kila siku.!!!!!!
Saturday, December 6, 2008
KUMBUKUMBU YA MAREHEMU BIBI YANGU
Subscribe to:
Posts (Atom)
