Showing posts with label umoja ni nguvu. Show all posts
Showing posts with label umoja ni nguvu. Show all posts

Monday, February 4, 2019

TUANZE MWEZI HUU WA PILI KWA PICHA HII:-UMOJA NI NGUVU

 Kuna wengi watakumbuka hii kazi ya kutwanga  sio hapo zamani tu hadi sasa hasa vijijini bado wana enzi utamaduni huu. Lakini jamii ya sasa sijui kama kuna anayejua kinu   na mwichi ni nini...najivunia kuwa mmoja ninayeuenzi utamaduni huu pia hata kizazi changu. NAWATAKIENI MWEZI MPYA HUU UWE MWEMA.


Wednesday, May 28, 2014

UMOJA NI NGUVU !!!

 Ni raha pale wote mnaposaidiana kazi  sio kumwachia mmoja tu. Hapa akina mama na watoto wanamenya karanga ingawa wengine wanapeleka mdomoni lakini wamejumuika kuifanya kazi...inavyoonekana ni karanga kwa ajili ya mbegu au labda kuunga mboga....Raha sana kushirikiana.....
....na hapa vijana hawapo nyumba wanasaidia kazi za nyumbani hapa wanakoboa mahindi. Wananikumbusha enzi hizi tulivyokuwa tukikoboa mahindi au kutwanga mihogo na kaka zangu. Nani anasema kazi ya kutwanga au kukoboa ni ya akina dada/mama tu?  Nimependa sana hii Je na wewe umependa?:-)

Wednesday, December 10, 2008

MKOKOTENI+USAFIRI+UMOJA+MBOLEA =MAISHA

Ngoja tuache mambo ya kukaa chini na kusoma vitabu vya hadithi. Sasa ni wakati wa kilimo kwa, mbolea zinahitajika. Na huu ndio usafiri wetu hapa Ruhuwiko. Kuna majembe mengi tu kwa hiyo msiona aibu. KARIBUNI