Showing posts with label matogoro. Show all posts
Showing posts with label matogoro. Show all posts

Monday, November 12, 2012

TURUDI TENA SONGEA KWETU:-UVUNAJI WA MITI KATIKA MILIMA YA MATOGORO KWASABABISHA KUKAUSHA MTO RUVUMA!!!

Na Daniel Mbega, Songea
 MVUA zilikuwa zikimtendea haki Josephat Komba, mkulima katika kijiji cha Ndilima Litembo wilayani Songea, wakati pepo za kusi zilipovuma vyema na hivyo shamba lake la mpunga kupata maji ya kutosha yaliyompa mavuno mengi. Lakini hana uhakika kama atapata bahati kama hiyo msimu ujao.
“Zamani, hatukuwa na mashaka kuhusu hali ya hewa,” anasema Komba, akiwa shambani kwake kilometa kadhaa kutoka Songea mjini. “Lakini hivi sasa, tatizo ni kubwa mno.”
Komba anaitazama Milima Matogoro kwa masikitiko, na kujiuliza kama mabadiliko hayo ya hali ya hewa yameletwa na Mungu au wanadamu.
“Tumesikia mara kadhaa kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa, lakini nikwambie ukweli, miaka ya nyuma milima hii unayoiona hapa ndiyo ilikuwa mkombozi wetu. Tuliitegemea sana kwa ajili ya kuleta mvua, sasa hatujui kama ni laana ya Mungu au ni binadamu ndio tunaosababisha majanga haya,” anasema.
Komba anasema, zamani walikuwa wakipanda kwa wakati na mvua zilinyesha katika kipindi kile kile. “Lakini tangu walipoanza kufyeka miti kwenye milima hii, kila kitu kimebadilika. Nadhani wameikasirisha miungu.”
Misimu kadhaa iliyopita, mvua zikaanza kuadimika. Mara kadhaa mpunga wake ulikomaa bila unyevu; karibu theluthi ya mimea yake ilikauka kwa ukame na hata Mto Ruvuma ambao amekuwa akiutegemea umekuwa hauna maji ya kutosha hata nyakati za masika.
Mabadiliko hayo ya ajabu ya hali ya hewa ndiyo ambayo wanasayansi wa mazingira wanaamini kuwa ni madhara ya mabadiliko ya hali ya hewa. Wakati mwingine kunaweza kuwa na ukame, lakini msimu mwingine mvua zinaweza kuwa nyingi kiasi cha kuleta mafuriko hivyo kushindwa kulima.
Komba analalamika kwamba, uchomaji wa moto kwenye msitu wa milima hiyo ni sababu nyingine inayoondoa hali ya asili ya milima hiyo ya Matogoro na hivyo kuleta wasiwasi mkubwa kwamba mito mikuu kama Ruvuma, Luhira na Luwegu itatoweka katika miaka michache ijayo.
Sehemu kubwa ya msitu wa Milima ya Matogoro imebakia vipara kutokana na uvunaji wa miti ya kigeni (exotic trees) kama Misindano (Pines) na Mikaratusi (Eucalyptus) ambayo wataalamu wa hifadhi ya vyanzo vya maji wanasema inayonya maji mengi.
Mhandisi Jaffari Yahaya wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Manispaa ya Songea (SOUWASA) anasema kwamba kuwepo kwa ukosefu wa maji wakati wa kiangazi katika Manispaa ya Songea kunachangiwa kwa kiasi kikubwa na aina ya miti ambayo ipo katika misitu ya milima Matogoro ambayo hunyonya maji kwa kiwango kikubwa kwa kipindi cha mwaka
Soma zaidi hapa

Saturday, September 13, 2008

JUMAPILI NJEMA

Hili ni kanisa langu ambalo wakati naishi Songea (mahenge) nilikuwa kila jumapili nakwenda kumshukuru mungu hapa. Ni Kanisa la Matogoro.






Na hapa ni kanisa ambalo nilipata Kipaimara wakati naishi ubenani. Ni kanisa la Maweso. Jumapili njema tena kwa wote.