Showing posts with label asante. Show all posts
Showing posts with label asante. Show all posts

Thursday, June 16, 2011

Thankfulne​ss

Be thankful my dear,
Always learn to thank them.

People will ignore you,
Be happy when thanking them.

When people do hurt you,
Make sure you thank them.

They'll then satisfy you,
Don't forget to thank them.

Love has to disappoint you,
Be happy and thank it.

And when people do admire you,
It's when you always thank them.

Then, after reading this poem,
Happily say, THANK YOU!
SHAIRI HILI NIMETUMIWA NA MTANI WANGU MSHAIRI MTANGA nikaona si vibaya kama nikiweka hapa ili nanyi mpate chochote. AHSANTE!!

Tuesday, April 5, 2011

NIMEMKUMBUKA KWELI MDOGO WANGU ASIFIWE LEO

Yasinta na Asifiwe 2009 mwezi wa pili
Leo nimeamka nikimuwaza kweli mdogo wangu Asifiwe nusu nichukue simu na kumpigia ili tuchape hadithi zetu kama tulivyozoea. Nikawa nasikia kama vile ananiita dada, dada, nami nikawa namwita jina lake na mara nikakukumbuka shairi hili aliloandika mtani wangu Fadhy ukitaka kusoma mashairi yake zaidi basi ingia Fadhili ya diwani Shairi lenyewe linasema hivi:-
Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani

Asifiwe! Asifiwe! sauti zetu sikia,


Asifiwe! Asifiwe! kweli unatusikia?


Asifiwe! Asifiwe! mbona hujaitikia?


Asifiwe umekwenda, dunia 'meikimbia,


Wajua tulikupenda, ila Mungu kazidia,


Mauti yamekutenda, wewe umetangulia,


Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.


Umetwachia majonzi, hakika twakulilia,


Tumejawa na simanzi, hatuwezi elezea,


Mdogo wetu mpenzi, uchungu 'metuachia,


Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.


Ulijawa na adabu, nao ukarimu pia,


Kwa wako utaratibu, ni nuru imepotea,


Umekwenda kama bubu, kwa heri hukutwambia,


Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.


Wewe mtu mwuungwana, kwa njema yako tabia,


Tulikupenda kwa sana, nd'o maana twaumia,


Mfano wako hakuna, kwa pengo kulizibia,


Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.


Kuondoka kwatuliza, kila tukifikiria,


Twatamani tungeweza, kifo tungekizuia,


Mwaka huu kumaliza, nayo inayof'atia,


Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.


Lakini sisi ni nani, Mungu tukamwamulia?


Tukamwuliza kwa nini, wewe amekuchukua?


Mwamuzi ndiye Manani, aloiumba dunia,


Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.


Pengo halitozibika, wewe ulotuachia,


Daima 'takukumbuka, wema'wo kusimulia,


Tukimwomba Rabuka, mwanga kukuangazia,


Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.


Upumzike salama, kwa Mola twakuombea,


Akupe pahala pema, nuru kukuangazia,


Asifiwe mtu mwema, buriani twakwambia,


Pumzika kwa amani, Asifiwe Ngonyani.


Shairi hili nimeliandika maalumu kwa marehemu Asifiwe Ngonyani, mdogo wa kike wa dada yetu, rafiki yetu na mwanablog mwenzetu Yasinta Ngonyani. Asifiwe alipatwa na mauti Jumatano 23.03.2011. Asifiwe umetuacha kimwili tu, kiroho tungali pamoja nawe. Tunakuombea pumziko salama la milele. Amina. AHSANTE SANA MTANI FADHY KWA SHAIRI HILI!!