Showing posts with label vyakula. Show all posts
Showing posts with label vyakula. Show all posts

Tuesday, April 10, 2018

VYAKULA VYA USWAHILINI VINAVYOSAHAULIKA

Naanza kuwaza hili jambo iweje tusahau vyakula kama hivi vilivyotukuza, au ndo kama vile tunavyopenda mavazi ya kigeni na sasa ipo kwenye vyakula pia?

Friday, March 9, 2018

PALE UPATAPO WASAA WA KUPUMZIKA BASI PUMZIKA KWANI NI MUHIMU KATIKA MAISHA YA MWANADAMU

Hapa yaonekana kuna kitu alikuwa akishangaa  au sijui hakuwa na njaa?
CHAKULA AKIPENDACHO KAPULYA KULIKO VYOTE HAPA DUNIANI NI SAMAKI
BAADA YA KAZI YA WIKI NZIMA SIO MBAYA KUJOPONGEZA KIDOGO. NAWATAKIENI WOTE MWISHO MWEMA WA WIKI HII NA IWE YA FURAHA NA AMANI ITAWALE KATIKA KAYA ZENU.

Wednesday, August 2, 2017

HIVI NDIVYO VYAKULA AVIPENDAVYO KAPULYA WENU

Ugali wa ulezi na nyama ya kuku, na sio ugali tu ugali na mlima wake juu ukiisha huu ni lazima usingizi mnono utapatikana iwe mchana au usiku:-)
Samaki waliokaangwa kwa ustadi haswaaaa
Au tu chips MIHOGO...nimekula sana mlo huu wakati nipo chuo kwanza naupenda pia ilikuwa bei rahisi  na unashibisha . Ukipata na kachumbali yako mmmhhh utajiuma kidole au pia ulimi:-) Haya niwatakieni mlo mwema siku ya leo chochote utakachokula kiwe kitamu.....PANAPO MAJALIWA

Friday, March 4, 2016

IJUMAA YA LEO TUPO KATIKA SOKO LA NAMTUMBO NJE KIDOGO YA MJI WA SONGEA

Hebu angalia hapa vyakula vyetu vya asili yaani hata kuangalia tu unashiba... umeona eehh. Nyanya, Tangawizi na vyakula vingine kwa wingiiii...Mmmmhhh ngoja NIWATAKIENI IJUMAA NJEMA. PANAPO MAJALIWA TUTAONANA.

Tuesday, December 3, 2013

JUMANNE YA LEO TUTEMBEE KWETU LITUMBANDYÓSI /NYUMBANI NI NYUMBANI!!!

 Hapa ni sokoni petu ukitaka dagaa, viazi vitamu, samaki nk.utapata bila matatizo:-) 
 Na hapa usipotaka dagaa au samaki basi waweza kujipatia kiti moto ...
Na hapa ndo unga tayari umeshasagwa kwa hiyo hakuna shida. Isipokuwa  ni  kuandaa chakula tu sasa....Nimeutamani huu unga basi tu...NAWATAKIENI JUMANNE NJEMA..

Monday, May 20, 2013

TUANZE JUMATATU HII KWA KUTEMBEEA MAENEO YA SOKO KUU LA SONGEA,,,HAPA ILIKUWA MWEZI WA KWANZA 2013....KARIBU!!!

 Hapa ni baadhi ya duka maalumu kwa kanga tu..tukiwa katika msako wa kununua kanga..si umeona zilivyo nyingi. Tulipata shida sana kuchagua. Hili ni baadhi ya kitu dhaifu kwangu..kuchagua.....
 Ndani ya soko kuu ...hapa ni sehemu ya kupata mchele
Huwezi kununua mchele tu Nyanya, Vitunguu na mapochopocho mengine ni lazima pia..

Saturday, April 6, 2013

JUMAMOSI YA LEO NINGEPENDA MLO WANGU UNGEKUWA HIVI...NAOTA NDOTO...

 
 

Nimeamka na kuanza kufikiri huu ungekuwa mlo wangu wa siku ya leo chai kwa maandazi au vitumbua...
 ....chai ya rangi bila sukari
 ...au labda chai kwa Vitumbua na chapati...
Na hapa ungekuwa mlo wangu wa mchana huu sambusa....Sambusa tamu sana ila inabidi uwe na muda haswaaa..
na kumalizia siku kwa ugali kwa samaki na kachumbali kidogo---
kumalizia na glasi ya maji...mmmhhh hivi ndivyo ningependa siku yangu ya leo ningekula lakini sasa sitaweza ....nakula kwa macho. baadhi ya picha nimezipata hapa. JUMAMOSI NJEMA.

Wednesday, September 3, 2008