Showing posts with label binadamu. Show all posts
Showing posts with label binadamu. Show all posts

Thursday, January 19, 2017

SWALI LA LEO: SISI BINADAMU NI KITU GANI HASA?

Tunajitahidi sana katika kuvaa vizuri, kula vizuri, kujenga nyumba bora, kendesha magari makubwa na kufanya mengine ambayo yanaweza kuipa raha miili yetu na kutupatia  umaarufu ikibidi. Moja ya sababu za kufanya kwetu hivyo, ni ile imani yetu kwamba sisi ni miili yetu. Lakini ajabu ni kwamba, pamoja na kufanya hivyo, bado tunajikuta haturidhiki. Wengi hatujui kwamba, kutoridhika kwetu huko ni taarifa kwamba sisi ni kitu kingine, siyo miili hii tuliyonayo. Je, tumeshawahi kujiuliza sisi ni akina nani hasa? Kama bado, tumepata nafasi ya kujiuliza sasa na bila shaka tutapata jibu litakaloturidhisha.
Chanzo:- kitabu cha MAISHA NA MAFANIKIO

Friday, February 22, 2013

IJUMAA YA MWISHO YA MWEZI HUU WA PILI TUIMALIZE NA UJUMBE HUU:- KILA BINADAMU ANA MAPUNGUFU YAKE!!!

Sisi binadamu tumeumbwa na mapungufu, Hakuna aliyekamilika kila mmoja ni tofauti na mwingine. Kuanzia kimawazo, kimatendo pia kitabia. Na kwa kuwa kama tulivyo, hii ndio maana tuna hitaji pale jambo linapopinda, tuchukue jukumu na kujaribu kuliweka sawa na pia KUSAMEHEANA. Ila KUMSAMEHE mtu si jambo dogo maana kama kweli unamsamehe mtu basi umsamehe KIDHATI/TOKA ROHONI. Au hata kumpa yule mtu aliyekosea/uliyepishana naye mawazo nafasi ya pili/ajaribu tena. Sababu yeye ni banadamu kama wewe, yule, mimi na wao. NACHOTAKA KUSEMA HAPA:- KAMA UMEHITILAFINA NA MTU JARIBU KUONGEA NAYE ILI KUSHULUHISHA NA UTAOANA MAISHA YANAKWENDA SAFI. KWANI KUKAA NA KITU MOYONI HAISAIDII KITU. Binafsi kama kuna kitu nimemkosea mtu/nimemdanganya mtu basi NASEMA SAMAHANI SANA, SANA, SANA, SANA....kwani hata mie ni binadamu na nina mapungufu.NA NINGEOMBA TUANZE UPYA/SECOND CHANCE. IJUMAA NJEMA!!

Monday, January 28, 2013

KWANGU MIMI ILIKUWA NI KAMA NDOTO....!

Jana wakati nipo kazini nilipata nafasi kidogo na kupita hapa kwenye kibaraza cha kaka yangu mzee wa Utambuzi. Nikakutana na kisa hiki hapa kwa kweli kilinigusa sana kiasi kwamba nimeona niweke hapa na wengine msome...haya karibuni.......
...............................................................................................................................................
Hadi leo naona kama ndoto.............!
(Picha haihusiani na habari hii.)
Nakumbuka ilikuwa ni mwaka 1991 wakati huo nikiwa nafanya kazi kwa mtu binafsi, Muasia mmoja. Nakumbuka katika mojawapo ya majukumu yangu, nililazimika kwenda Nairobi nchini Kenya. Nilikwenda huko kikazi na nililazimika kukaa kwa mwezi mmoja. Nilipomaliza kazi ile, niliamua kukaa kama siku tatu zaidi ili kujionea hali ya Kenya ilivyo. Nilizunguka jijini Nairobi na kwenda maeneo ya karibu kama vile Thika, Kinangop na miji mingine iliyo karibu na jiji hilo maarufu katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.
Siku moja wakati natoka kwenye matembezi yangu nje ya jiji hilo la Nairobi, nilikutana na mtu mmoja. Huyu bwana alikuwa anaonekana kuchoka sana, ama kwa kuumwa au kwa njaa. Nilikaa naye kiti kimoja kwenye Matatu, yaani daladala za Kenya. Huyu bwana alikuwa ananitazama mara kwa mara na kujitahidi kutaka kama kutabasamu, ingawa hakumudu sana.
Niliingiwa na huruma na kulazimika kumuuliza kama alikuwa yu mzima wa afya. Alisema anaumwa na hana hata senti tano ya kulipia matibabu yake. Nilimuuliza kama anao ndugu. Alisema hana na familia yake iko mashambani, ambapo haina kitu kabisa. “Nina watoto watatu mmoja amemaliza shule hana kazi na wawili wanasoma, lakini ni kwa mashaka sana, kwani mara nyingi hurudishwa nyumbani kutokana na kukosekana ada.” Aliniambia.
Ilibidi nimchukue yule bwana hadi hospitalini ambapo alichukuliwa vipimo. Aliambiwa arudi kesho yake kuchukua majibu yake. Tuliagana tukutane pale hospitalini kesho yake. Kwa kweli hakuamini kwamba, nilimfikisha hospitalini na kumlipia matibabu. Hakuweza hata kushukuru na nilielewa ni kwa sababu gani. Mshangao ulikuwa ni mkubwa sana kwa upande wake.
Kesho yake alipata majibu yake ambayo yalionyesha kwamba alikuwa na maji kwenye pafu moja pamoja na kifua kikuu. Ilibidi aandikiwe dawa. Hakuwa na fedha kabisa. Ilibidi nitoe fedha zote za matibabu yake. Ilikuwa kama silimia 20 ya pesa zote nilizozipata pale Nairobi kama posho. Lakini hiyo haikunisumbua. Nilikuwa najisikia vizuri kuona angeweza kupona.
Ilibidi niombe ruhusa ya siku saba zaidi ili nikae Nairobi kukagua hali ya yule jamaa. Wakati huo huo nilimwambia kwamba, kama anaweza kumwita mkewe akae naye pale mjini wakati anatibiwa ingekuwa vizuri. Nilimwambia ningemsaidia pesa kidogo za kumwezesha mkewe kukaa naye angalau kwa siku kadhaa. Alikubali na kumwita mkewe. Mkewe alipofika hakuamini kwamba niliweza kumsaidia mumewe vile. Yule mama alilia sana na aliniombea sana kwa kikwao, yaani Kikikuyu kwa majina ya mizimu yote. Nilijisikia furaha kwa namna mke wa jamaa alivyojisikia vizuri kuona mumewe amepata matibabu.
Niliondoka Nairobi siku ya tatu tangu mkewe kuja. Niliwaachia hela kiasi cha shilingi 14,000 za Kenya, ambazo nilimwambia yule mama zingemsaidia kufanyia shughuli yoyote ambayo ageona inafaa. Niliondoka bila hata kuwaachia anuani yangu wala simu yangu. Labda wao walitegemea ningewapa anuani yangu, lakini sikufanya hivyo. Mimi sikuona sababu ya kuwapa kwani, niliwasaidia kama binadamu ambao wanahitaji msaada wangu, siyo ili wanijue au tuwe marafiki.
Hivyo ndivyo nilivyo hata leo. Sijisifu kwa sababu sioni kuwa ni sifa, bali naona kila binadamu angetakiwa kuwa hivyo, ila basi tunazuiwa na choyo ya kufundishwa. Sikuwahi kusoma kuhusu masuala ya kusaidia na kupata furaha wala kumsikia mtu. Tabia hii nilitoka nayo kwetu, niliitoa kwa baba yangu ambaye, alikuwa mtu wa kusaidia sana bila kujali malipo. Hilo nalijua.
Mambo yangu yalienda vizuri hadi mwaka 1994. Mwaka huo nilipoteza kibarua change na hata shughuli zangu zikawa zimepoteza umaarufu kutokana na mabadiliko ya teknolojia. Ilibidi nianze kuhangaika. Kufikia mwaka 1996, nilikuwa hoi bin taabani kiuchumi. Watoto wangu watatu wakawa hawaendi tena shule, hakuna ada. Tulishindwa kulipa kodi ya nyumba, ambapo ilibidi tufukuzwe na kwenda kuishi kwa ndugu wa mke wangu. Huyu naye hatukukaa hata mwezi masimango yakaanza. Siwezi kumlaumu, kwani kusaidia siyo jambo rahisi, ingawa naamini ndipo mahali furaha ya binadamu ilipo.
Tulilazimika kuhama na kwenda kuishi Mtoni Kijichi. Huko hatukuwa tumepanga. Jamaa yangu mmoja alikuwa anajenga kule na alikuwa anataka mlinzi, ambapo nilimwambia ningefanya kazi hiyo. Hivyo tukawa tunaishi kwenye kibanda cha mtumishi. Lakini tulihisi nafuu. Hata hivyo watoto wote walisimama shule, kwani hata nauli ya kuwapa ili waende shule ilikuwa ni vigumu.

Wednesday, January 16, 2013

UJUMBE WA SIKU YA LEO!!

Watu wengi Binadamu wachache!! TUWE NA SIKU NJEMA!!!

Tuesday, October 23, 2012

WIKI HII NAONA ITAKUWA YA RUVUMA---TURUDI SONGEA TENA..


Wote tunajua MAJI ni muhimu kwa uhai wa binadamu ...kuwa na maji safi na salama kila mtu ana haki lakini si wote wanapata huduma hii...KILA LA KHERI

Tuesday, October 9, 2012

HII ITAKUWA PICHA YA MWAKA KWA KWELI ..!!!!

Inasemekana maziwa ni lishe bora kwa watu/hasa watoto lakini ndiyo hivi kweli? Salama hapa?
Ngoja nisikilia hizi chuchu nyingine ili wengine wasije wakachukua....Nimewahi kusikia kuwa ni hatari kunywa maziwa bila kuchemsha  yaani moja kwa moja kama mtoto huyu. Je ni kwa binadamu tu au?Maana Ndama hadhuriki..Kaaaazi kwelikweli hapa..sijui mama alikuwa wapi?

Thursday, September 20, 2012

KISA CHA KWELI !!!!


Nimetumiwa kisa hiki na msomaji wa Maisha na Mafanikio. Nikachukua muda na kusoma kwa kweli lazima niseme kisa hiki kimenigusa sana na nikaona kwamba msomaji huyu hajawa mchoyo kwangu kwanini mimi niwe mchoyo nimeona niweke hapa kibarazani ili wengi tujifunze maisha yalilivyo. KARIBUNI MUUNGANE NAMI.
................................................................................................................................................................
Ni siku nyingi kidogo, mwaka 1979, lakini ni tukio ambalo liliniuma sana. Ilikuwa vigumu sana kulisahau na lilinifanya nijiulize, inakuwaje Mungu anakuwa mkatili kiasi kile. Lakini bila shaka ilikuwa ni wakati ule wa ufahamu mdogo. Hivi sasa ninafahamu mengi na hasa baada ya kujifunza maarifa haya ya utambuzi.

Ilikuwa ni mwaka 1979 nikiwa nasafiri kutokea Dar es salaam kwenda Arusha. Sijui ilikuwaje, lakini ilitokea. Tuliondoka Dar es salaam saa 12.30 jioni. Wakati ule mabasi yalikuwa yakisafiri jioni na usiku, sio kama siku hizi.

Nilikuwa ninakwenda Arusha kwenye usaili kwa ajili ya ajira, nikiwa ndio kwanza nimemaliza kidato cha nne. Niliajiriwa moja kwa moja serikalini, kwani siku zile ajira zilikuwa ni za kumwaga. Hata hivyo sikuridhishwa na kazi niliyokuwa nafanya, hivyo niliomba kazi kwenye kampuni moja kule Arusha na niliitwa kwa usaili.

Tulifika mji unaoitwa Korogwe ambao wakati ule ulikuwa ndio mji maarufu kwa hoteli zake katika barabara yote ya Segera hadi Moshi na Arusha. Tulipofika Korogwe basi letu lilisimama kwa ajili ya abiria kupata chakula. Niliingia kwenye hoteli moja ambayo nakumbuka hadi leo kwamba ilikuwa ikiitwa Bamboo. Niliagiza chakula na kula haraka kutokana na muda mfupi wa kula uliotolewa na wenye basi la TTBS ambalo ndilo nililosafiri nalo.

Wakati wa kulipa ndipo niliposhangaa na kuogopa. Niliingiza mkono mifukoni na kukuta kwamba sikuwa na hela. Nilianza kubabaika na mwenye hoteli alisema hawezi kukubali ujinga huo, "Abiria wengine wahuni bwana, anakula na kujifanya kaibiwa, ukikubaliana nao kila siku hasara tu" Mwenye hoteli alisema kwa kudhamiria hasa.

Kulizuka zogo kubwa, huku mwenye hoteli akisema ni lazima anipeleke polisi. Ni kweli alimtuma mmoja wa watumishi wake kwenda kituo cha polisi ili nishughulikiwe……

Hapo Hotelini kulikuwa na bwana mmoja aliyekuwa amekaa pembeni na mkewe na watoto wao wakila. Yule bwana alipoona vile alimtuma mhudumu mmoja aniite. Niliondoka pale kaunta nilipokuwa nabembeleza na kuja kwa yule bwana.

Alikuwa ni kijana mtu mzima kidogo, mwenye miaka kama 50 hivi. Nilimsalimia na aliitikia, nilimsalimia mkewe pia. Yule bwana aliniuliza kisa cha vurugu ile na nilimsimulia. Aliniuliza sasa huko Arusha ningeishi vipi wakati wa usaili wakati nimeibiwa fedha zote na ningerudi vipi Dar. Nilimwambia nilikuwa napanga namna ya kurudi Dar, kama huko polisi ningeaminika.

Kama mzaha vile yule bwana aliniambia kuwa angenipa fedha za kutumia huko Arusha na nikirudi Dar nimrudishie fedha zake. Nakumbuka alinipa shilingi 90 kwa ahadi kwamba nikirudi Dar nimpelekee fedha zake ofisini kwake. Alinielekeza ofisini kwake, mtaa wa Nkuruma na kuniambia kuwa ameamua kunisaidia kwa sababu kila binadamu anahitaji msaada wa mwingine na maisha haya ni mzunguko. Nilimshukuru na kuondoka kukimbilia basini. Basi lilikuwa linanisubiri mimi tu. Nilipanda ndani ya basi na abiria wengine walinipa pole. Tuliondoka Korogwe, lakini haikuchukua muda basi letu lilipata tatizo la pancha ya gurudumu moja la mbele. Ilibidi tuegeshe pembeni ili litengenezwe. Baada ya matengenezo, tuliondoka kuendelea na safari yetu.

Karibu na mji wa Same kwenye saa saba usiku, basi letu lilisimama ghafla. Abiria walisimama ndani ya basi na kulizuka aina ya kusukumana. Huko nje kulikuwa na ajali. Abiria tulishuka haraka na wengine huko chini walishaanza kupiga mayowe, hasa wanawake. Niliposhuka niliona gari ndogo nyeusi ikiwa imebondeka sana na hapo kando kulikuwa na maiti wawili.

Nilijua ni maiti kwa sababu walikuwa wamefunikwa gubigubi. Halafu kulikuwa na katoto kalikokuwa kanalia sana kakiwa kamefungwa kanga kichwani. Tumwahishe huyu mtoto hapo Same hospitali ameumia, ingawa sio sana. Nilikatazama kale katoto ka kiume kenye umri wa miaka kama mitatu. Kalikuwa kameumie kwenye paji la uso, lakini kalikuwa hai. Bila shaka wale walikuwa ni wazazi wake, kalikuwa yatima tayari. Machozi yalinitoka.

Baada ya kupata msaada na askari wa usalama barabarani kuchukua maiti wale tulipanda basini kuendelea na safari yetu. Kale katoto kalichukuliwa na jamaa fulani waliokuwa na Land Rover ya serikali kukimbizwa hospitalini. Ndani ya Basi mazungumzo yalikuwa ni kuhusu ajali ile tu, hadi tunafika Arusha. Tulichelewa sana kufika Arusha kwani tulifika kwenye saa tano asubuhi, badala ya saa mbili .

Nililala kwenye hoteli rahisi na kufanya usaili kesho yake. Ni hiyo kesho, baada ya usaili niliponunua gazeti ambapo nilipata mshtuko mkubwa ajabu. Kumbe wale watu wawili waliokufa kwenye ajali ile ya Same walikuwa ni yule bwana aliyenisaidia hela na mkewe. Yule mtoto wao ndiye aliyeokoka. Niligundua hilo baada ya kusoma jina lake na jina la kampuni aliponiambia nimpelekee fedha zake nikirudi Dar, pamoja na picha yake, mke na mtoto. Nililia sana, kama mtoto.

Nillishindwa kujua ni kwa nini afe. Nilijiuliza ni nani sasa angemlea mtoto yule? Yalikuwa ni maswali yasiyo na majibu na pengine maswali ya kijinga pia.
Nilijua kwamba nilikuwa na deni, deni la shilingi tisini. Kwa wakati ule shilingi tisini zilikuwa ni sawa na shilingi laki moja za sasa.
Kwa mara ya kwanza sasa nilijiuliza ni kwa nini marehemu yule aliniamini nakuamua kunipa fedha zile. Sikupata jibu.

Nilikata kipande kile cha gazeti la kingereza kilichokuwa na habari ile. Nilichukuwa kipande hicho na kukiweka kwenye Diary yangu. Deni, Ningelipa vipi deni la watu? Nilijikuta nikipiga magoti na kuomba mungu anipe uwezo wa kuja kulilipa deni la mtu yule mwema kwa njia yoyote. 'Mungu naomba uje uniwezeshe kulilipa deni la marehemu kwa sura na namna ujuavyo wewe. Nataka kulilipa deni hili ili nami niwe nimemfanyia jambo marehemu,' niliomba. Nilirejea Dar siku hiyo hiyo.Kwa sababu ya mambo mengi na hasa baada ya matokeo ya usaili ule kuwa mbaya kwangu, nilijikuta nikiwa na mambo mengi na kusahau haraka sana kuhusu mtu yule aliyenisaidia mbaye ni marehemu. Nilifanikiwa hata hivyo kupata nafasi ya kusoma Chuo cha Saruji na baadae chuo cha ufundi na hatimaye nilibahatika kwenda nchini Uingereza. Mwaka 1991 nilianza shughuli zangu.

Ilikuwa ni mwaka 1995 nikiwa ofisini kwangu pale lilipokuwa jengo Nasaco ambalo liliungua mwaka 1996, ambapo lilijengwa upya na kubadilishwa jina na kuitwa Water Front. Nikiwa nafanya kazi zangu niliambiwa na sekratari wangu kwamba kulikuwa na kijana aliyekuwa anataka kuniona. Nilimuuliza ni kijana gani, akasema hamjui. Nilimwambia amruhusu aingie. Kijana huyo aliingia ofisini. Alikuwa ni kijana mdogo wa umri miaka kama 17 au 18 hivi, mweupe mrefu kidogo. Alikuwa amevaa bora liende , yaani hovyohovyo huku afya yake ikiwa hairidhishi sana.

Nilimkaribisha ilimradi basi tu, kwani niliona atanipotezea bure muda wangu. Ni lazima niwe mkweli kwamba sikuwa mtu mwenye huruma sana na nilikuwa naamini sana katika watu wenye pesa au majina. Nilimuuliza, “nikusaidie nini kijana na ukifanya haraka nitashukuru maana nina kikao baada ya muda mfupi”. Nilisema na sikuwa na kikao chochote , lakini nilitaka tu aondoke haraka.

“Samahani mzee, nilikuwa na shida…..nimefukuzwa shule na sina tena mtu wakunisaidia kwa sababu …..nime….niko ….kidato cha pili na hivyo tu natafuta tu kama atatokea mtu……..
Nilimkatisha. “Sikiliza kijana. Kama huna jambo lingine la kusema, ni bora ukaniacha nifanye kazi. Hivi unafikiri kama nikiamua kumsaidia kila mtu aliyefukuzwa shule si nitarudi kwetu kwa miguu! Nenda Wizara ya Elimu waambie……Kwanza wazazi wako wanafanya kitu gani, kwa nini washindwe …..Kwa nini walikupeleka shule ya kulipia kama hawana uwezo, wanataka sifa?”

“Hapana wazazi wangu walikufa na ninasoma shule ya serikali. Nimekosa mahitaji ya msingi na nauli ya kwendea shule. Nasoma shule ya Kwiro, Morogoro. Shangazi ndiye anayenisomesha, naye ana kansa na hivi sasa hata kazi hafanyi….,” Alianza kulia. Huruma fulani ilinijia na nilijiambia, kama ni nauli tu na matumizi, kwa nini nisiwe mwema, angalau kwa mara moja tu. “Baba na mama walifariki lini?” Niliuliza nikijua kwamba, watakuwa wamekufa kwa ukimwi, maana kipindi kile ndipo fasheni ya ukimwi ilipoanza, ambapo kila anayekufa huhesabiwa kwamba kafa kwa ukimwi.

“Walikufa kwa ajali nilipokuwa mdogo sana, nilipokuwa na miaka mitatu. Ndio shangazi yangu akanichukua na kunilea hadi sasa anakufa kwa kansa.” Yule kijana alilia zaidi. Naomba nikwambie wewe msomaji unayesoma hapa kwamba, kuna nguvu fulani na sasa naamini kwamba ziko nyingi ambazo huwa zinaongoza maisha yetu bila sisi kujua.

Kitu fulani kilinipiga akilini paaa! Nilijikuta namuuliza yuel kijana. “Kwa nini umeamua kuja kwangu, ni nani alikuelekeza hapa na wazazi wako walikufa mwaka gani na wapi?”
Yule kijana alisema, “Nimeona nijaribu tu kwa mtu yeyote ambaye anaweza kunisaidia, na ndio nimejikuta nikiingia hapa, sijui……..sikutumwa na mtu. Wazazi wangu walikufa mwaka 1979 huko Same na mimi wanasema nilikuwa kwenye ajali, nikaokoka. Niliumia tu hapa.” Alishika kwenye kovu juu ya paji lake la uso.

Nilihisi kitu fulani kikipanda tumboni na kuja kifuani halafi niliona kama vile nimebanwa na kushindwa kupumua. “Baba yako alikuwa anaitwa nani?” “Alikuwa anaitwa Siame….Cosmas Siame….” Niliinuka ghafla hadi yule kijana alishtuka . Nilikwenda kwenye kabati langu mle ofisini na kuchakura kwenye droo moja na kutoka na diary. Mikono ikinitetemeka, nilitoa kipande cha gazeti ndani ya diary hiyo, nilichokuwa nimekihifadhi.

“Ndio alikuwa anaitwa Cosmas Siame. Huyu ni mtoto wake, ni yule mtoto aliyenusurika.” Nilinong’ona. Nilijikuta nikipiga magoti na kusali. “Mungu, wewe ni mweza na hakuna kinachokushinda. Nimeamini baba kwamba kila jema tunalofanya ni akiba yetu ya kesho na kesho hiyo huanzia hapa duniani.” Halafu nillinyamaza na kulia sana. Nililia kwa furaha na ugunduzi wa nguvu zinazomgusa binadamu kwa kila analofanya.

Nilisimama nikiwa nimesawajika kabisa. Nilihisi kuwa mtu mwingine kabisa. Nilimfuata yule kijana na kumkumbatia huku nikiwa bado ninalia. “Mimi ni baba yako mdogo, ndiye nitakyekulea sasa. Ni zamu yangu sasa kukulea hadi mwisho” Naye alilia bila kujua sababu na alikuwa amechanganyikiwa kabisa. Nilirudi kwenye kiti na kumsimulia kilichotokea miaka 17 iliyopita.

Tuliondoka hapo na kwenda kumwona shangazi yake Ubungo, eneo la maziwa ambako alikuwa amepanga chumba. Kutokana na hali yake nilimhamishia kwangu, baada ya kumsimulia kilichotokea. Huyo dada yake Cosmas alifurahi sana hadi akashindwa kuzungumza kwa saa nzima. Alifariki hata hivyo mwaka mmoja baadae, lakini akiwa ameridhika sana.

Kijana Siame alisoma na kumaliza Chuo Kikuu na hivi sasa yuko nchini Australia anakofanya kazi. Ukweli ni kwamba ni mwanangu kabisa sasa. Naamini huko waliko Mbinguni wazazi wake wanafurahia kile walichokipanda miaka mingisana nyuma. Lakini nami najiuliza bado. Ilikuwaje Cosmas akanipa msaada ule? Halafu najiuliza ni kitu gani kilimvuta mwanae Siame hadi ofisini kwangu akizipita ofisi nyingine zote? Nataka nikuambie, usiwe mbishi sana bila sababu, kuna nguvu za ziada zinazoongoza matokeo maishani mwetu…………

*************MWISHO*********

Wednesday, September 19, 2012

SHUKRANI ZANGU...



Chacha wambura Ng´wanambiti
Katika maisha, watu wengi hufikiri watu wa karibu yaani ni familia tu. Leo nimehakikisha kitu ambacho sitaweza kusahau maishani mwangu. Watu/mtu anachukua muda wake na kufanya kitu ambacho wengi hawangefanya. Huyu kaka sijawahi kuonana naye lakini kama alivyosema hapa kwake hakika ni wachache sana wanafanya hivi. Mwenyezi Mungu na akubariki na akuzidishie upendo. Ahsante sana.

Thursday, September 13, 2012

UJUMBE WA LEO:- HUU NDIYO UPENDO!!!

Ufafanuzi mmoja kuhusu upendo ni, ‘uhusiano mchangamfu na wakibinafsi au shauku yenye kina, kupendezwa sana na mtu mwingine.’
Ni sifa ambayo huchochea watu wafanye mambo yanayowanufaisha wengine, nyakati nyingine wakifanya hivyo kwa kujidhabihu sana. Kulingana naufafanuzi wa Biblia, upendo wahusisha akili na moyo.
Akili, au uwezo wa kufikiri, hutimiza fungu fulani kwasababu mtu anayependa hufanya hivyo akitambua kwamba yeye pamoja na wanadamu wengine anaowapenda, wana udhaifu na vilevile sifa zenye kuvutia.

Uwezo wa kufikiri wahusika hata zaidi kwa kuwa kuna wale ambao Mkristo huwapenda—nyakati nyingine, hata ingawa nyutu zao hazimpendezi—kwa kuwa kutokana na kuisoma Biblia anajua kwamba Mungu anataka afanye hivyo.
Hata hivyo, kwa asili upendo hutoka moyoni. Upendo halisi kama uonyeshwavyo katika Biblia hautegemei tu uwezo wa kufikiri. Wahusisha unyofu mwingi na kujitoa kabisa kihisia-moyo.

Ni nadra sana kwa watu ambao ni wenye ubinafsi kudumisha uhusiano wenye upendo wa kweli kwasababu mtu anayependa huwa tayari kutanguliza masilahi ya mwingine.
Maneno ya Yesu “kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko kulivyo katika kupokea” ni ya kweli hasa wakati wa kutoa kunapokuwa tendo la upendo.Upendo ni kifungo chenye nguvu. Mara nyingi upendo hutia ndani urafiki, lakini vifungo vya upendo ni vyenye nguvu zaidi ya vifungo vya urafiki.

Uhusiano wa kimahaba kati ya mume na mke wake nyakati nyingine husemwa kuwa upendo; hata hivyo, upendo ambao Biblia hututia moyo tusitawishe hudumu kuliko uvutio wa kimwili.
Mume na mke wanapopendana kwelikweli, huendelea kuwa pamoja hata isipowezekana tena kuwa na uhusiano wa kimwili kwa sababu ya udhaifu unaosababishwa na uzee au kwa sababu mmoja wao hajiwezi.
UPENDO DAIMA!!!

Thursday, September 6, 2012

WANADAMU NA TABIA ZETU/CHUKI ZETU....KUSENGENYANA/KUSEMANA HADI MAOFISINI...

Jana nilikuwa naangalia kipindi fulani na hapo ndipo nilipokumbuka. Ya kwamba watu wengi wanasema akina mama/wanawake ni watu ambao wanapenda sana kusemana/kusengenyana. Hapana si wanawake tu nimeona mwenyewe kwa macho yangu na kusikia kwa masikio yangu. Yaani mtu anakuwa rafiki yako na unaongea naye, na unacheke naye na unamwamini kabisa lakini kumbe sio unavyofikiri wewe. Na watu wengi wamekuwa wakigombana/gombanishwa kwa kitu ambacho si cha kweli na mwisho kuishia kuwa madui wakubwa. Kwa nini kusema ya wenzio na yako nani atasema.? Na kwa nini kama tuna nguvu  basi tuchukue jembe na kwenda kulima kuliko kutumia muda na kusema wengine? Na kwa nini mpaka kumsema mwingine? Ni afadhali kuchukua jukumu na kumwambia/kumuuliza tu. Kuliko kusengenya sengenya ...
Ngoja mr. Nice amalizie  kwa TABIA GANI .....

UNAPOMSEMA MWENZAKO JIFIKIRIE MWENYEWE KUWA JE? KAMA NINGESEMWA MIMI NINGEJISIKIAJE?

Thursday, August 9, 2012

FIKRA/WAZO LA LEO:- UTOFAUTI WA BINADAMU JINSI ULIVYO!!


Nimekuwa nikifikiri sana jinsi binadamu tulivyo tofauti. Sio kimaumbile tu LA HASHA. Bali  ni kiMATENDO, kiMAWAZO/kiFIKRA na  kiTABIA. Kwa mfano: Kuwa na ile tabia ya UMIMI/kijionea huruma, yaani mtu anajua amefanya kosa, lakini hata hivyo anaona wewe aliyekutendea unamwonea tu.Anataka uwe upande wake.
Halafu hii ya kuwa na HASIRA ZA HARAKA ambazo watu wengi inakuwa ngumu kusamehe hata kitu kiwe kidogo kwako kinakuwa kikubwa. Sababu kubwa wanakuwa wameumizwa sana na yule aliyemuumiza mwenzake anaona si umizo/maumivu. Lakini kuna wengine ni wepesi sana kusamehe hata iweje sasa sijui wanasamehe kweli au?
SWALI LANGU ambalo nimekuwa nikijiuliza kila siku:- Je? kama wote tungekuwa hivyo dunia hii ingekuwa? Na Je? kundi lipi ni jema?

Wednesday, June 13, 2012

WANAUME KATIKA MAPENZI NI KAMA MASOKWE...!

Ndugu zangu wapendwa leo ni JUMATANO YA KIPENGELE CHA MARUDIO YA MAMBO /MAKALA,PICHA MBALIMBALI. Nale katika pitapita nimekutana na hii na si kwingine tena ni kwa  kaka yangu wa hiari Kaluse. KARIBUNI!!!!
Katika utafiti uliofanywa na akina Kruger na wenzake kwa wanyama jamii ya Sokwe, ilibainika kwamba kulikuwa na vifo vingi vya Sokwe madume wenye umri wa miaka 13. Hali hii ilitokana na sababu kwamba, kwa kawaida katika umri huo, Sokwe madume huwa wamefikia umri wa kupanda na kufanya mapenzi na hivyo huanza kushindana wenyewe kwa wenyewe wakigombea majike na hata kwa lengo la kudumisha hadhi yao miongoni mwa Sokwe wengine.
Katika hatua hii Sokwe hao hufikia mahali pa kupigana na hata kuuana kwa lengo la kujipatia wapenzi na kudumisha hadhi zao. Hali hii haiko kwa sokwe peke yao, bali hata kwa wanyama wengine pamoja na ndege wa aina mbalimbali.


Hata hivyo, pamoja na ukweli huo binadamu naye hajanusurika hata kidogo na purukushani za aina hiyo. Labda kinachomtofautisha binadamu na wanyama hao ni namna wanavyokabiliana na mashindano hayo. Lakini ukweli unabaki palepale kwamba, hata akichagua njia ya aina gani ili kushindana na binadamu wenzake, bado matokeo ya mwisho yatafanana na yale ya wanyama, yaani kifo.
Imeonekana wazi kwamba binadamu wa kiume ndiye mwenye mwelekeo mkubwa wa kupenda purukushani na kuhatarisha maisha yake. Ingawa binadamu huyu wa kiume au mwanaume hahitaji kupigana mweleka na mwanaume mwenzake ili kumpata mwanamke, lakini harakati zake ni zaidi ya kupigana mweleka.

Hata hivyo katika mazingira mengine, mieleka hupiganwa sana katika sura ya mieleka halisi au katika sura nyingine za ushindani wa kutafuta ushindi katika kumpata mwanamke. Wengi tunajua kuhusu habari za kuuawa kwa wanaume kutokana na vurugu za kugombea wanawake.

Tabia hii ya wanaume ya kuhatarisha maisha si ya leo, bali ni ya tangu kale. Huenda huko nyuma baadhi ya wanaume walitumia silaha kwa lengo la kuwadhulumu ama kuwauwa wanaume wenzao ili hatimaye waweze kuwamiliki wanawake wanaowapenda.
Kwa kawaida, wanaume hushindana wao kwa wao kwa lengo la kumiliki rasilimali na kuhifadhi au kudumisha hadhi na heshima yao ndani ya jamii wanamoishi.


Huu ndio ukweli wenyewe ambao hautofautiani hata chembe na ule wa Sokwe. Ukweli ni kwamba mwanaume anapokuwa na uwezo wa kumiliki rasilimali adimu kama vile fedha na anapoweza kusimika kwa uhakika heshima na hadhi yake, ndani ya jamii iliyomzunguka, mambo hayo humpatia thamani kubwa na kumrahisishia kazi ya kumpata mwanamke anayemtaka.
Au tu tumaliziae na ujumbe huu kutoka kwa CHOX FT ALIKIBA - TUSIGOMBANE

MUNGU AKIPENDA TUTAONANA TENA JUMATANO IJAYO NA RUDIO JINGINE. KWA SASA NASEMA JUMATANO NJEMA!!!

Tuesday, April 3, 2012

NIMEYAPENDA MENENO HAYA:- UBINADAMU KAZI!!!

Hapa ni mimi, nikiwa pamoja na wifi yangu na mwanae...ni mwaka jana. Hapa ni stendi KUU ya SONGEA tulikuwa tukiwasindikiza walikuwa wakirudi kwao Mbinga. Nimependezwa na maneno haya kwenye T-shirt ya Wifi. UBINADAMU KAZI.... ...KILA LA KHERI.

Friday, February 24, 2012

UJUMBE WA LEO:- KILA BINADAMU ANA MAPUNGUFU YAKE!!!

Sisi binadamu tumeubwa na mapungufu, Hakuna aliyekamilika kila mmoja ni tofauti na mwingine. Kuanzia kimawazo, kimatendo pia kitabia. Na kwa kuwa kama tulivyo, hii ndio maana tuna hitaji pale jambo linapopinda, tuchukue jukumu na kujaribu kuliweka sawa na pia KUSAMEHEANA. Ila KUMSAMEHE mtu si jambo dogo maana kama kweli unamsamehe mtu basi umsamehe KIDHATI/TOKA ROHONI. Au hata kumpa yule mtu aliyekosea/uliyepishana naye mawazo nafasi ya pili/ajaribu tena. Sababu yeye ni banadamu kama wewe, yule, mimi na wao. NACHOTAKA KUSEMA:- KAMA UMEHITILAFINA NA MTU JARIBU KUONGEA NAYE ILI KUSHULUHISHA NA UTAOANA MAISHA YANAKWENDA SAFI. KWANI KUKAA NA KITU MOYONI HAISAIDII KITU. Binafsi kama kuna kitu nimemkosea mtu/nimemdanganya mtu basi NASEMA SAMAHANI SANA kwani hata mie ni binadamu na nina mapungufu.NA NINGEOMBA TUANZE UPYA/SECOND CHANCE. IJUMAA NJEMA!!

Thursday, January 12, 2012

MAJI YA KWENYE MTUNGI NI MATAMU JAMANI!

Maji ya mtu ni matamu sana hasa kama unatumia kata au kikombe cha bati kama uonavyo hapo kwenye picha. Mtungi huu una historia yake:- Ni Hivi mwaka jana nilipokuwa Matema beach, pale kuna soko kubwa la vyombo vya aina mbalimbali vya udongo wa mfinyanzi. Nami nikaona ngoja niende nikasafishe macho. Kwa bahati nzuri nikaona mtungi huu nikaununua. Nakuambieni penye nia pana njia. Niliupakata mtungi huu kuanzia Matema Beach mpaka Songea/Ruhuwiko. Halafu kabla hatujafika nyumbani Ruhuwiko tukasimamishwa na Polisi pale Bombambili kwa wale wanaojua umbali wa kutoka Bombambili mpaka Songea mjini /Ruhuwiko. Tukamsalimu, mnajua alitaka nini, baada ya kuangalia ndani ya gari? MTUNGI HUU! Duh! hapo nikasema simpi ngó, naye akasema nitawatoza kwa spidi ila mkinipa mtungi nitawaacha nami nikamjibu, sawa tu..kwa vile nilijua hatukuwa katika mwendo wa spidi. Akashindwa na tukaendelea na safari. Hii ni historia fupi ya MTUNGI HUU.
Hapo juu nimesema maji ya mtungi ni matamu kwa kunywa kwa kutumia KATA. Kwa wale wasiojua kata ni nini . Katika picha hii hapa mnamwona Stella Manyanya akijaribu kunywa maji kwa kutumia KATA. Hivi ndivyo ilivyokuwa hapo zamani ni utamaduni wetu.

Thursday, April 14, 2011

AJALI YA RESTIELI

Restieli.

Gari lao lililohusika na ajili hiyo.

Mama na baba Restieli.

Kama mnakumbuka niliwahi kuweka ushuhuda wa binti mmoja aitwae Restieli Moses Mbwambo akieleza kisa chake cha kuungua na mafuta akiwa mdogo (ukitaka kujikumbusha waweza kubofya hapa). Juzi nimepata taarifa kuwa familia ya binti huyo akiwemo mwenyewe Restieli, walipata ajali katika maeneo ya Lembeni mkoani Kilimanjaro.



Ajali hiyo ilihusisha gari lao dogo aina ya Toyota RAV 4 waliyokuwa akisafiria kutoka Upareni kurejea Moshi hapo mnamo siku ya Jumanne ya tarehe 5/04/2011. Ajali hiyo ilitokea baada ya tairi la mbele la gari hilo kupasuka na hivyo kupinduka mara kadhaa. Habari nilizozipata ni kwamba wote walisalimika katika ajali hiyo isipokuwa walipata majeraha kadhaa mwilini ambapo walitibiwa na kuruhusiwa.



Mleta habari amebainisha kwamba kutokana na ajali hiyo gari lao limeharibika vibaya, na ukiliangalia hutaamini kama waliokuwa ndani ya gari hilo wote wamepona.



Blog ya Maisha na Mafanikio inapenda kuchukua nafasi hii kuwapa pole wote walionusurika katika ajali hiyo, na ninaamini Mungu ataendelea kuwalinda.

Wednesday, April 13, 2011

Tafakari ya leo:- Umpendaye ndiye?

Moyo wa mtu ni kichaka na watamanianao huonekana wengi bali wapendanao ni wachache na hawajulikani. Hebu fikiria leo Mungu akisema kila moja asimame na ampendaye Je? Wewe utasimama na nani? Na huyu umdhaniaye ukimkuta amesimama na ampendaye utafanyaje? Haaaaaa…..!! Unacheka?

Friday, March 11, 2011

MAISHA/MILA,UTAMADUNI NA DESTURI:- SIKU YANGU ILIVYAKUWA LEO....MAZISHI!!!

Sijui nianzia wapi??
Ok ni hivi:- Jana Alhamisi nilikuwa kazini, na baada ya kazi kama kawaida ya watu wote huwa wana hangaika na mihangaiko au kuridi nyumbani na kupumzika. Kwa hiyo nami nilifanya hivyo jana nilikuwa na mihangaiko yangu na baadaye nikarudi nyumbani. Ile kuingia tu ndani nikakumbana na mlio wa simu, kuangalia sioni jina yaani limefichwa, hata hivyo sikusita nikapokea.

Oh! Kumbe wewe Mariana, ndiyo mimi Yasinta, hali yako? Salama tu......tukaendelea maneno mawili matatu...Oh, nilisahau Mariana ni rafiki yangu anatoka Angola. Basi pale tukawa tunapeana habari za hapa na pale na mara akaniambia kuwa rafiki yetu mwingine kutoka Serbien kafiwa na mamamkwe wake na mazishi ni kesho yaani leo.

Hapo nikawa hoi, ingwa huyo mama mkwe wa rafiki yetu Saida sijawahi kumwona hata siku moja. Nikashikwa na uchungu sana. Kwa hiyo nikakata shauri kwenda kwenye mazishi yake ambayo yalikuwa leo. Mamamkwe wa Saida anaitwa Maria amefariki akiwa na miaka 82.

Tulikuwa na misa na baadaye tukaunganika na kumsindikiza mamamkwe Maria kwa safari yake ya mwisho. Kulikuwa na watu 23 na Padre 24. Nasikitika sana kuwa sijaweza kupiga picha nilisahau kamera yangu nyumbani. Mamamkwe Maria na Ustarehe kwa Amani Peponi Amina!!

Monday, November 1, 2010

HUU NDIO WEMA!

Jirani kala nini?

Huu ndio wema! Unapotenda wema usitegemee fadhila. Unapokuwa na marafiki, ndugu, na jamaa wa karibu, watendee wema bila kudhamiria kupata fadhila kutoka kwao. Ninapoongelea wema na kutoa ninamkumbuka mama Theresa wa Calcutta ambaye kwa umri na maisha yake angelikuwa Bilionea lakini kwa kujitolea kwake alikufa masikini, lakini akiwa ni tajiri wa nafsi. Nina maana alikufa akiwa na ridhiko, kwani kazi aliyotaka kuifanya aliifanya tena kwa kufaulu. Je wewe hufurahii kuwa kama yeye?
Kumbuka amri kuu isemayo “mpende jirani yako kama unavyojipenda” Je unapokula na kusaza huwa unajiuliza kuwa jirani kala nini?

Tafakari……… hii aliandika mdogo wangu wa hiari Koero Mkundi.

Friday, October 22, 2010

WANYAMA NAO WANAFIKIRI NA KUFANYA MAJARIBIO KAMA SISI BINADAMU!!

Hapa vipi???
Sijui hapa niseme huyu farasi ni mjinga au? unakubaliana wanyama wapo karibu sana na sisi binadamu? Nakumbuka nilipokuwa mdogo nilikuwa nacheza na rafiki yangu Pona tulikuwa tukipangua mbula/mabuni na mchezo huo umenipa kilema kwenye kidole changu, kwa ajili ya kufanya majaribio kama huyo Farasi. Sijui atatukaje hapo?



Nadhani kama huyu Chura hapa juu wengi leo ni mwisho wa juma na kazi mpaka jumatatu tena kwa hiyo itakuwa ni kupumzika tu. Haya nawatakieni IJUMAA NJEMA SANA!!!!