Watoto uwaleavyo ndivyo wakuavyo hapa wakiwa wanacheza bao mchangani....zaidi mchezo huu huchezwa na watoto wakiume....au vijana pia akina baba. Wengi wetu nadhani twaukumbuka mchezo huu...ni mchezo lakini hapo kunamambo wanajifunza kama vile hesabu nk.
Na hapani watoto wa kike wakicheza mchezo wa mdako... nilipenda sana mchezo huu....maharage yalikuwa yanaungua kila mara :-)
Watoto wengi hasa wa kiume walipenda sana kucheza huu mchezo kama baiskeli au gari vile ni ringi la baiskel ...hapa watakiwa kuwa na balansi...
Usipojifunza mapishi tangu udogo itakuwa shida...ni mchezo lakini ndiyo kujifunza huko.....zamani watoto walikuwa wakijifunza vitu vingi sana na kupata maarifa ...lakini sasa mmmhhh wapo mitandaoni tu....

