Showing posts with label mjadala. Show all posts
Showing posts with label mjadala. Show all posts

Wednesday, November 30, 2011

SWALI LILILONIKERA KWA MIAKA MINGI!!!

Nimeshindwa kuvumilia mwenzenu, kwani hili jambo/swali limekuwa likinikera miaka sasa.

Ni hivi:- Hivi kwanini mwanamke mjane anweza kuishi peke yake mudamrefu au hata milele bila kuolewa tena na mwanamume mwingine? Maana ukiangalia asilimia kubwa ya wanaume wajane huwa hawaishi muda mrefu peke yao huwaa wanaoa tena.

Nina mfano mmoja, bibi yangu mzaa mama:- Babu alifariki mwaka 1980 na bibi amekuwa mjane mpaka Mwenyezi Mungu alipomchukua 2005. Na mafano mwingine nilionao ni baba mmoja nimfamuye mkewe alifariki 2004 na yeye 2006 tayari alipata mwanamke mwingine na kufunfa naye ndoa 2008.
Je?Hapa ndo kusema wanawake wanawapenda zaidi waume zao/wana uchungu zaidi kuliko wanaume?
NAOMBA TUJADILI KWA PAMOJA SWALA HILI JAMANI... KAPULYA WENU!!!!!

Thursday, March 12, 2009

MJADALA WA LEO:- KWA NINI WATU TUTOE RUSHWA

Kichwa kinaniuma sana kila nikifikiria hili jambo la rushwa. Najua mtasema nimesahau mambo yanavyokuwa nchini mwangu. Labda NDIYO:- Ni hivi juzi tu nimetoka nyumbani Tanzania. Kusema kweli nilishikwa na butwaa, kwanza kabisa ni hivi baba yangu amestaafu mwaka juzi 2007. Amepata kiinua mgongo chake, na baada ya hapo inabidi apate (mafao) pesa kiasi fulani kila baada ya miezi mitatu. Lakini mpaka leo hizi za kila baada ya miezi mitatu hajapata. Kila akifuatilia kwenye maofisi yanayohusika wanamwambia njoo kesho au anayehusika hayupo. Yaani hapo wanachotaka babangu awape ya SODA kidogo wakati anataka HAKI yake. Je? hii ni haki kuwasumbua watu/wazee walioitumikia serikali?

Bado sijamaliza:- Jingine ni kwamba mimi ni mgonjwa nahitaji matibabu. Cha kushangaza unaambiwa nipe ya kula mchana. Kwa nini mimi nimpe ya chakula wakati yeye analipwa mshahara. Ndiyo, labda ana mshahara mdogo. Maa sasa inaonekana usipokuwa na refa basi huwezi kufanikisha kitu.

Swali:- Kwa nini inakuwa hivi? na kwa nini isiwe kinyume?

Wednesday, September 24, 2008

MJADALA WA LEO

Hili swali limekuwa likinikereketa sana miaka yote ambayo nimeishi hapa duniani kwa hiyo sasa naomba mwenzangu tujadiliana au mnipe jibu.

SWALI NDIO HILI:- Je? Kuna sheria Tanzania isemayo kama msichana akipata mimba asiendelee na masomo?