Wednesday, October 8, 2008

MAISHA NA MAZINGIRA

Leo mwenzenu nimeamka vibaya, Kwani nimekasirika sana. Kisa ni kwamba nimekuwa nimefikiri muda mrefu ni vipi watu wanaweza kufanya hivi. Yaani siku zote hizi nilikuwa nimefungwa kabisa. Leo ndo naamka na nimekasirika mno. Mazingira, nani alisema watu wanaruhusiwa kumiliki maji au niseme nusu ya bahari. Watu wageni wanatoka huko na mihela yao na kuja nchi za wengine na kuamua yeye anamiliki nusu bahari. Kwa mfano Jangwani Seabreeze Resort, mtu anatoka huko Pakistani na kujengelea fensi ile wenye nchi wasiwe huru kwa nini? Na kwa nini wengine wanakubali kulipa pesa nyingi kwa sehemu ambayo Mungu ameifanya ili watu wote wafurahie maisha. Lakini sasa ni wachache tu wanafurahia. Kwa kweli naumia sana kuona wananchi hawana uhuru kwa sababu ya mtu ana pesa na katoka huko PAKISTANI. WATANZANIA TUSIWE HURU KATIKA NCHI YETU. Bado sielewi kwa nini? Je? wenzangu mnaelewa?

No comments: