Sunday, March 21, 2010

Nawatakieni Jumapili njema wote na neno Upendo!!!

Ufanyacho upendo:-

Upendo kidogo ni kama jua, ambalo ni rafiki yetu wa daima. Hufukuza baridi, kuimarisha mazao yetu na kuyaivisha. Hivyo ndivyo ufanyavyo upendo; kama jua. Katika kupendana, yule mwenye kupendwa hibadilika. Anabadilishwa kutoka hali ya mashaka, wasiwasi, hofu, upweke na kutoamini; anakuwa mtu mwingine kabisa. Mwanzoni alikuwa mwenye hofu na mashaka, sasa ni mwenye kujiamini na kuthubutu kutenda. Badala ya uchungu na upweke, imekuwa furaha na heri. Ni kama nyoka abadilishaye ngozi yake ya zamani kwa wakati fulani, na kubaki na ngozi mpya. Kwa upendo aliopata mtu huyu amefanywa kuwa mpa.

Mara nyingi twasikia watu wakisema , "Huyu mvulana anampendaje msichana huyu?" au " nini cha kuvutia alicho nacho Bwana huyu?" Haina maana kuuliza kwa nini twampenda mtu mwingine. Kama ni mapendo kweli, hatumpendi mtu kwa kuwa ana vitu fulani vya kuvutia wala hatumpendi ingawa ana kasoro, bala tunampenda mtu aliye ndani ya yote haya.

Na kwa kweli tunaweza kupata maana kamili ya upendo kutoka kwa Mungu peke uyake ambaye Neno lake latuambia

upendo: huvumiliam hufadhili,
Upendo: hauhusudu,
Upendo: hautabakari, haujivuni,
Upendo: haukosi kuwa na adabu, hautafuti mambo yake,
Upendo: hauoni uchungu, hauhesabu mabaya
Upendo: haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli
Upendo: huvumilia yote, huamini yote, hutumaini yote, na hustahimili yote
(1 Wakorintho 13: 4-7)
NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI/DOMINIKA HII YA 12 YA MWAKA HUU. MWENYEZI MUNGU AWA NANYI WOTE. AMINA



6 comments:

Mija Shija Sayi said...

Yasinta neno la leo lina nguvu. Asante, asante sana.

MARKUS MPANGALA said...

ASANTE SANA

Simon Kitururu said...

Jumapili njema kwako pia!

PASSION4FASHION.TZ said...

Asante sana na kwako pia.

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

mhmm

Yasinta Ngonyani said...

Da mija! Asante:-)

Markus! Ahsante wewe pia

Simon! Ahsante

Passion4fashin.tz ! shukrani

Kamala! mhmmm Vipi?