Tuesday, March 20, 2018

KUMBUKUMBU.....NIMEIPENDA HII PICHA NA NIMEONA IWE PCHA YA WIKI HII

UJUMBE:- JANA NI HISTORIA. KESHO NI MIUJIZA  NA LEO NI ZAWADI.
NAPENDA KUWATAKIENI SIKU YA LEO IWE NJEMA SANA, FURAHA NA AMANIPIA. KAPULYA WENU....

2 comments:

ray njau said...

Jitihada ya Kutafuta Furaha

MIAKA michache iliyopita, watu nchini Marekani, Ufaransa, Uingereza, na Ujerumani waliulizwa, “Ni nini kinachohitajiwa ili kuwa na furaha?” Kati ya wale waliohojiwa, asilimia 89 walisema kwamba ni lazima uwe na afya nzuri; asilimia 79 wakataja ndoa au uhusiano mzuri; asilimia 62 wakataja thawabu ya kuwa mzazi; nao asilimia 51 wakasema kwamba ni lazima mtu awe na kazi nzuri ili awe na furaha. Na hata ingawa kwa kawaida watu wengi wanafundishwa kwamba pesa haziwezi kuleta furaha ya kudumu, asilimia 47 ya wale waliohojiwa walisadiki kwamba zinaweza. Lakini ukweli wa mambo unaonyesha nini?

Kwanza, ona uhusiano unaodhaniwa kuwepo kati ya pesa na furaha. Uchunguzi uliofanyiwa watu mia moja walio matajiri zaidi nchini Marekani ulionyesha kwamba matajiri hao hawakuwa na furaha zaidi kuliko watu wa kawaida. Isitoshe, ingawa watu wengi nchini Marekani wameongeza mali yao maradufu katika miongo mitatu iliyopita, wataalamu wa magonjwa ya akili wanasema kwamba furaha ya watu hao haijaongezeka. Hata ripoti moja inasema: “Katika kipindi hichohicho, idadi ya watu wanaoshuka moyo imeongezeka. Idadi ya matineja wanaojiua imeongezeka mara tatu, nayo idadi ya wale wanaotalikiana imeongezeka maradufu.” Katika nchi 50 hivi, watafiti waliochunguza uhusiano uliopo kati ya pesa na furaha walikata kauli kwamba pesa haziwezi kununua furaha.

Kisha, mambo kama vile afya nzuri, ndoa yenye furaha, na kazi nzuri ni muhimu kadiri gani ili kuwa na furaha? Kwa kweli, ikiwa mambo hayo yanahitajiwa kabisa ili kuwa na furaha, vipi yale mamilioni ya watu ambao hawana afya nzuri na wale wote ambao ndoa zao hazina furaha? Namna gani wenzi wa ndoa ambao hawana watoto, na pia wanaume na wanawake wote ambao hawana kazi nzuri? Je, watu hao wote wanaishi maisha yasiyo na furaha? Na je, wale ambao sasa wanadhaniwa kuwa na furaha kwa sababu ya afya nzuri na ndoa nzuri watapoteza furaha kama hali zao zitabadilika?

Je, Tunatafuta Furaha Mahali Panapofaa?

Kila mtu anataka kuwa na furaha. Hilo halishangazi kwa sababu Muumba wa wanadamu anatajwa kuwa “Mungu mwenye furaha,” naye mwanadamu aliumbwa kwa mfano wake. (1 Timotheo 1:11; Mwanzo 1:26, 27) Hivyo, ni jambo la kawaida kwa wanadamu kutafuta furaha. Hata hivyo, wengi huona kwamba kuidumisha ni sawa na kushikilia mchanga—zote huponyoka kwa urahisi.

Hata hivyo, je, watu fulani hujitahidi kupita kiasi ili kupata furaha? Mwanafalsafa wa masuala ya kijamii Eric Hoffer alifikiri hivyo. Alisema: “Kutafuta furaha ndiyo sababu kuu ya ukosefu wa furaha.” Bila shaka, hiyo ni kweli tukiitafuta furaha mahali pasipofaa. Tukifanya hivyo, bila shaka tutakata tamaa na kufadhaika. Hatutapata furaha kwa kujaribu kuwa matajiri; kujitahidi kuwa mashuhuri; kufuatia miradi ya kisiasa, ya kijamii, au ya kiuchumi; au kuishi tu maisha ya ubinafsi na kutosheleza tu tamaa zetu papo kwa hapo. Si ajabu kwamba wengine wamekubaliana na maoni yenye kupingana ya mwandishi mmoja aliyesema hivi: “Kama tu tungeacha kujitahidi kuwa na furaha tungekuwa na furaha ya kiasi fulani”!

Ni muhimu kuona kwamba uchunguzi uliotajwa mwanzoni mwa makala hii pia ulionyesha kwamba watu 4 kati ya 10 walihisi kwamba furaha hutokana na kuwafanyia wengine mema na kuwasaidia. Na mtu 1 kati ya 4 alikazia kwamba imani na usadikisho wa kidini ni muhimu sana ili kuwa na furaha. Bila shaka, tunapaswa kuchunguza kwa makini ni nini kinachohitajiwa ili kuwa na furaha kikweli.(Chanzo:www.jw.org/sw)

Yasinta Ngonyani said...

Mimi nafikiri ni muhimu kutafuta furaha sio pesa...makala hii ipo jikoni itakuja wiki ijayo....Ahsante sana kwa maoni yako