Thursday, May 1, 2008

Mei 1, 2008 Elimu

Hili jambo limekuwa likinikereketa sana akilini mwangu. ELIMU je? ni nani ana haki ya kupata elimu hapa duniani. Kwa mfano afrika yetu,wazazi wengi wanasema hakuna haja ya kusomesha watoto/mtoto wa kike kwani wanaogopa watapoteza bure pesa kumsomesha mtoto wakati wanajua baada ya muda atarudi nyumbani tu. Lakini kitu ambach mimi bado sijaelewa kwa nini hao wasichana wanaokatishwa masomo baada ya kulea mtoto wake asiendelee na masomo? kwani kwa akili yangu sioni kama kuna tatizo wao wasiendelee na masomo yaani yote ya shule ya msingi na pia sekondary. Au kwa nini basi kusiwe na shule maalum kwa wale wasichana waliopata watoto. Kwani inasemekana kuwa Elimu ni ufunguo wa maisha , Sasa je? kama sisi wasichana hatupati elimu tutakuaje na ufunguo wa maisha?

Na; Yasinta Ngonyani

No comments: