Katika pitapita zangu kila siku nakutana na mengi sana katika blog nyingi na hivi karibuni nilikuwa nimepita hapa na nikakutana na WAZO la mwanablog mwenzetu nimelipenda wazo lake nami nikaona si mbaya kama nikaleweka hapa ili kueneza wazo lake.
---------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
WAZO LA LEO: Mila na desturi zipo, na tumezikuta kwa
wazee wetu, zipo nyingi, na nyingi hatuzijui tena kwa vile huenda hazikuwezekana
kutekelezeka. Lakini kuna mambo mengi mazuri tumeyapuuzia, na kwa kufanya hivyo
tumejikuta tukipata taabu sana,…nachukia kwa mfano wa kutafuta mchumba, kabla
mtu hajaoa au kuolewa, wazee wetu walikuwa wakihakikisha kuwa mke au mume wa
kuoa au kuolewa anatafutwa kwa kufanyika uchunguzi wa kina kwenye familia
anayotoka…ni ni hekima yake, ni kuwa kwa kumpata mume au mke bora ni kwa ajili
ya kizai bora, na matokeo yake ni kuwa na familia bora na hili litaweza kujenga
taifa lenye amani, hili tumelipuuza, na matokea yake ndio haya..
Pia wazee wetu walikuwa wakiangalia kuwa huyo anayeolewa au
kuoa, hana matatizo yoyote ya kiafya au ya kurithi, au tabia za kishirikina, au
tabia zozote mbaya…haya yalikuwepo na ukiyachunguza kwa makini utayaona kuwa
yalikuwa na faida zake, lakini huenda haya na mengine mengi hayapo tena
tumeyapuuza.
Wazo langu la leo. Zipo mila nzuri,
tuzifuate, na kama zipo mila potofu, tuziache, au tuziboreshe ziwe bora zaidi,
lakini tusisahau kabisa mila na desturi zetu zenye hekima ndani, na kukimbilia
mila na desturi za wenzetu,….kwanini tupuuze mila zetu, ….huo ndio utamaduni
wetu na anayeacha utamduni wake ni mtumwa.
NIWATAKIENI JUMANNE NJEMA NA KILA MTAKALOTENDA LIWE NJEMA...UJUMBE TUPENDANE....KAPULYA WENU