MADONGA/MATUNDA YA ASILI
Nimeamka nikiwa na hamu kweli ya matunda haya ya asili, nimekumbuka nilipokuwa mdogo ukienda mstuni kuokota kuni basi huko nyumbani wasahau maana chakula tayari kilikuwepo. Matunda haya yanakuwa kwanza kijana, na baadaye yanakuwa njano unapasua na ndani yake kuna mbegu. Mbegu hizo zina nyama nyingi tu basi unazimungúnyamungúnya kama vile pipi na mbegu unatema...weeeeeeeeeeeee ni matamu na sijayala miaka mingiiiiiiiiiiii nimetamani kwelikweli...kama vile LIKUNGU....Kuna mwingine amewahi kula matunda haya????