Thursday, March 29, 2012

POROJO YA LEO !!!

Bwana mmoja karudi nyumbani toka kazini amechoka ile mbaya, akaingia ndani na kujitupa kochini ili aangalie TV. Akamwambia mkewe:-
- Niletee bia, karibu inaanza .
-Mkewe akapumua na akampa bia.
- Baada ya dakika kumi na tano akasema :-
-Nipe bia nyingie maana karibu inaanza.
Mke wake akamwangalia kwa kuchoka choka lakini akampa bia nyingine:
Alipokuwa amemaliza ile bia baada ya dakika kadha akasema:-
- Nipe bia nyingie, kwani itaanza dakika yoyote ile.
-Mkewe akachukia na kumpigia kelele, akasema.
- Yaani huna kazi nyingine ya kufanya jioni hii, zaidi ya kukaa na kuangalia TV na kunywa bia?
Wewe huna lolote isipokuwa ni mvivu, mwanaharamu mkubwa.......
Yule bwana akapumua na kusema:-
-Sasa imeanza.......
Je wewe pia unajiuliza kama mimi ni nini kilichoanza?

5 comments: