Thursday, August 3, 2017

LEO TUANGALIE :- SIFA ZA MTAMA NA VIRUTUBISHO VYAKE!


Sifa za mtama:- Mtama una virutubisho muhimu vinavyotakiwa katika mwili wa binadamu. Tafiti zinaonyesha kuwa mtama una kiasi cha wanga, nishati, nyuzi nyuzi, na mafuta karibu au sawa na mahindi au nafaka nyingine.

Mtama una madini aina ya chuma na chokaa kwa wingi kuliko mahindi au nafaka nyingine. Una protini kwa wingi kuliko mahindi, mchele au ngano. Mafuta yake hayanarehamu, Una vitamin B complex,vitamin C  na vitamin E kwa wingi. Mtama una madini ya zinc, phosphorus, potassium, na manganese kwa wingi kuliko nafaka nyingine.

Mtama una vimelea viitwavyo phenolica mbavyo ni mhimu sana kwa mwili kujikinga na saratani, Mtama hauna gluten  hivyo ni  salama kutumiwa na watu wenye matatizo au ugonjwa  wa Celiac.
Muhimu: Sukari yake huyeyuka taratibu sana mwilini hivyo mtama ni chakula kinachofaa kuliwa na watu wenye magonjwa kama kisukari.
HII NIMETUMIWA NA RAFIKI  NIKAONA NI SOMO ZURI KWA WENGI ....AHSANTENI.

No comments: