Sunday, February 28, 2016

NI JUMAPILI YA TATU YA KWARESMA:- UJUMBE... MSHUKURU MUNGU KWA KILA JAMBO....

Mungu akikuacha katika hali fulani:-
Basi mshukuru wala usilalamike. Kwani yeye ndiye akujuaye zaidi. Pia usidhani kama maisha yamekamilika kwa mtu yeyote.
Kuna mwenye nyumba lakini hana gari, kuna mwenye gari lakini hana watoto, kuna mwenye watoto lakini hana pesa, kuna mwenye pesa lakini hana afya, kuna mwenye afya lakini hana kazi na kuna mwenye vyote lakini hana AMANI wala FURAHA. MSHUKURU MUNGU KWA KILA JAMBO.  Nami naanza kwa kusema AHSANTE MUNGU KWA KILA JAMBO.

No comments: