Tuesday, September 30, 2014

KAMA MNATAKA MALI!!!!


Nadhani wengi hasa mlio na umri wangu mnakumbuka kitabu hiki au vitabu hivi ya TUJIFUNZE LUGHA YETU. Leo nimekumbuka shairi hili...haya fuatana nami......

Karudi baba mmoja, toka safari ya mbali,
Kavimba yote mapaja, na kutetemeka mwili,
Watoto wake wakaja, ili kumtaka hali,
Wakataka na kauli, iwafae maishani.

Akatamka mgonjwa, ninaumwa kweli kweli,
Hata kama nikichanjwa, haitoki homa kali,
Roho naona yachinjwa, kifo kinanikabili,
Kama mwataka kauli, semeni niseme nini.

Yakawatoka kinywani, maneno yenye adili,
Baba yetu wa thamani, sisi tunataka mali,
Urithi tunatamani, mali yetu ya halali,
Sema iko wapi mali, itufae maishani.

Baba aliye kufani, akalibi lile swali,
Ninakufa maskini, baba yenu sina hali,
Neno moja lishikeni, kama mnataka mali,
Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

Wakazidi kumchimba, baba mwenye homa kali,
Baba yetu watufumba, hatujui fumbo hili,
Akili yetu nyembamba, haijajua methali,
Kama tunataka mali, tutapataje shambani?

Kwanza shirikianeni, nawapa hiyo kauli,
Fanyeni kazi shambani, mwisho mtapata mali,
Haya sasa burianai, kifo kimeniwasili,
Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

Alipokwisha kutaja, fumbo hili la akili,
Mauti nayo yakaja, roho ikaacha mwili,
Na watoto kwa umoja, wakakumbuika kauli,
Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

Fumbo wakatafakari, watoto wale wawili,
Wakakata na shauri, baada ya siku mbili,
Wote wakawa tayari, pori nene kukabili,
Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

Wakazipanda shambani, mbegu nyingi mbalimbali,
Tangu zile za mibuni, hata zitupazo wali,
Na mvua ikaja chini, wakaona na dalili,
Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

Shamba wakapalilia, bila kupata ajali,
Mavuno yakawajia, wakafaidi ugali,
Wote wakashangilia, usemi wakakubali,
Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

Wakawanunua ngómbe, majike kwa mafahali,
Wakapata na vikombe, mavazi na baiskeli,
Hawakuita pombe, sababu pombe si mali,
Kama mnataka mali, mtayapata shambani.

Wakaongeza mazao, na nyumba za matofali,
Pale penye shamba lao, wakaihubiri mali,
Walikiweka kibao, wakaandika kauli,
KAMA MNATAKA MALI, MTAYAPATA SHAMBANI.
NA HAPA NI MWISHO....!!!!

Sunday, September 28, 2014

NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI/DOMINIKA NJEMA!!!

Hivi ndivyo nilivyoonekana jumapili ya leo baada tu ya kutoka kanisani kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunilinda na kuniepusha na majaribu mengi na  mabaya. Napenda kuwaombea watu wote  wafu na wazima. UJUMBE WANGU WA LEO NI :- Kristo ni tumaini letu.

Saturday, September 27, 2014

ZILIPENDWA..NYUMBANI RUHUWIKO

Ilikuwa 2009 Ruhuwiko, tulifikiwa na wageni ambao ni watata viziwi toka shule ya watoto viziwi Ruhuwiko. Na siku hii kulikuwa na mvua kubwa sana na wote tukawa ndani . Bahati nzuri baraza ilikuwa kubwa sana... Ni viziwi lakini tulipata maswali mengi sana toka kwao...JUMAMOSI NJEMA KWA WOTE

Wednesday, September 24, 2014

PICHA YA WIKI!!!

NAWATAKIENI WOTE SIKU NA MAJUKUMU MEMA ...KUMBUKA SISI SOTE NI NDUNGU!!

Monday, September 22, 2014

JUMATATU YA LEO INATUPELEKA MPAKA SOKONI SONGEA

Yaani hapa ni aina zote za ..kuanzia dagaa, samaki wadogo mpaka mbelele chagu lako tu...Mimi nimetamani zaidi dagaa tena wala madafu na  samaki aina ya mbelele. Kwa chakula ulichokua nacho ni ngumu kukisahau..HAYA NAWATAKIENI WOTE MWANZO MWEMA WA JUMA !!

Friday, September 19, 2014

KWA NINI SALOMON ALIKUWA NA WAKE 700?/Why Solomon had 700 wives?

 
Katika matembezi yangu nimekutana na habari hii, nimeipata Jamii Forum. Haya karibu......

Juzi nilipokwenda dukani kununua liwa kwa ajili yakurembesha uso wangu. Muuzaji alinifungia liwa hiyo kwenye kipande cha karatasi ambacho kilikuwa na habari inayomhusu Nabii Suleiman AS.Huyu nabii anaelezwa kwamba alikuwa na utajiri mkubwa usiyo kifani, lakini pia alikuwa na busara na hekima haijapata kutokea hapa duniani. Alikuwa na nguvu sana na utajiri wake ulikuwa ni mkubwa usioweza kupimika.Lakini pamoja na kujaaliwa neema zote hizo lakini vyote hivyo havikuwa na maana yoyote kwake.
Inasemekana alikuwa ni mwanaume shababi mwenye siha nzuri. Pamoja na kuwa na wake 700 na nyumba ndogo zipatazo 300, lakini kamwe hakuna na amani moyoni mwake.
Je ni kitu gani alikosa nabii huyu?
1. Wake warembo alikuwa nao 700
2. Nyumba ndogo zilizojaaliwa neema za Allah zilikuwa
3. Hekalu kubwa lenye kila aina ya nakshi vikiwemo vito vya thamani
4. Utajiri mkubwa usio na mfano ulikuwa mikononi mwake
Alikuwa ana uwezo wa kupata starehe zote alizozitaka hapa duniani zikiwepo pombe za kila aina huku akiwa amezungukwa na wanawake warembo wa kila sampuli waliojaaliwa neema za Allah……. Mh!
Unaweza kushangaa, Je ni kitu gani amekikosa mtu huyu?

Naam, hebu angalia maisha ya vijana wa kiume wa nyakati hizi.
Wanahangaika sana kutafuta fedha, wanajenga mahekalu,wananunua magari ya kifahari, wanaoa wake warembo, wanakuwa na uwezo wa kula starehe sana tena za kila aina, watatafuta nyumba ndogo zisizo na hesabu,lakini bado hawatatosheka.

Pamoja na habari hiyo ya nabii Suleiman ambayo wengi wetu tunaifahamu vyema, lakini bado vijana wa kiume wameshindwa kung’amua kwamba hivi vitu vya nje, yaani Fedha, na fahari zote za dunia si chochote, na kamwe haviwezi kutuletea amani na ridhiko hata siku moja katika maisha yetu.


Kama Nabii Suleiman hakupata ridhiko kwa amali alizojaaliwa na Mwenyenzi Mungu seuze wao!


Ni kuhangaika tu kusiko na mashiko na kamwe fedha,mahekalu na wanawake wanene wanene wenye makalio makubwa na matiti yenye kututumka vifuani na sura za kuvutia si mali kitu, havitawafaa hata kwa miaka dahari.

Mtafuteni Mungu atawaongoza, acheni michepuko,tulieni na wake zetu.
NACHUKUA NAFASI HII NA KUWATAKIENI MWISHO MWEMA WA WIKI....KAPULYA

Wednesday, September 17, 2014

MAMA MJASILIAMALI AKIWA AMEBABA ZAMBARAU ANAKWENDA KUUZA!!!

Maisha ni kuyakubali na mwisho wa siku utaona mafanikio yake. Ila ukisema unataka mafanikio ya haraka hakika sijui kama yapo. Nimependa kuona watu/huyu mama anavyojituma. Mafanikio ni kujituma. NAWTAKIENI WOTE JUMATANO NJEMA NA KUMBUKENI TUPO PAMOJA.

Tuesday, September 16, 2014

NIMEKUMBUKA SANA KWETU LUNDO/NYASA

 
Hapa ni samaki wapo kwenye mtungo ndo wanatoka tu kuvuliwa...nadhani ni vituhi, ukipata na ugali wa muhogo hapo halafu na tembele au kisamvu eeeehhh bwana we basi tu. Haya kila la kheri kwa wote!!!

Saturday, September 13, 2014

NIMETAMANI HII...UTAMADUNI OYEEEEE!!!

Huki kiatu/sandali nimekifia kabisas yaani nimekipenda mno nitatafuta tu mpaka nikipate...JUMAMOSI NJEMA KWA WOTE!!

Friday, September 12, 2014

TUMALIZA WIKI KWA UJUMBE HUU UKIWA DUNIANI USIHUZUNIKE NA USIWE MNYONGE HATA KAMA UNA UMASKINI KIASI GANI!!!!

Ukiwa DUNIANI USIHUZUNIKE  na usiwe MNYONGE hata kama una UMASKINI kiasi gani, Mungu yuko pamoja nawe, na unatakiwa kizingatia haya;.

1. Usijilaumu kwa lolote lililokutokea.
2. Usihofu kuhusu hali uliyo nayo sasa.
3. Usijilinganishe na mtu yeyote duniani.
4. Usifikirie sana yaliyopita katika maisha yako
5. Kumbuka Mungu ndiye mpangaji wa kila linalokutokea.
6. Usiwaze sana kuhusu kesho waza kuhusu leo.
7. kukikosa ulicholikusudia yote ni mipango ya Mungu.
MUWE NA SIKU  PIA IJUMAA NJEMA NA MWISHO MWEMA WA JUMA.

Wednesday, September 10, 2014

NINA IMANI WENGI WETU TUNAKUMBUKA VIFAA HIVI....ZILIPENDWA-PICHA YA WIKI!!!

Bila redio kama hii ilikuwa hakuna kucheza disko,  bila pasi basi ni kuvaa shati la makunyanzi, bila kibatari/koroboi basi kulala kiza/giza na mwisho ni mpira huo ......

Monday, September 8, 2014

MWENZENU NIMETAMNI KWELI MLO HUU JIONI YA LEO...DUH MATE YANACHURUZIKA TU HAPA...

Sina jinsi nimebaki kutamani tu leo maana nimeishiwa unga ... halafu ebu angalia  hayo maharage mabichi ...ila inakosekana mboga majani maana mimi na mboga damudamu.....je wewe utakula nini jioni hii au sijui mchana  huu?

Saturday, September 6, 2014

UJUMBE TOKA MAISHA NA MAFANIKIO....

Nimeamka asubuhi hiii.... kama kawaida yangu huwa napitia barua pepe yangu...na leo nimekutana na ujumbe huu nimetumiwa na msomaji wa maisha na mafanikio. nikaona si mbaya nikiweka hapa ni kama ufuatavyo--------- karibu tujadili pamoja

Ni kwamba usipoteze muda  wako kuwa na watu/marafiki ambao hawana muda na wewe, yaani kila siku uwafuate wewe, kila siku ni wewe kuwapigia simu, kila siku ni wewe kuanzisha hadithi. Kama kweli wanakupenda na kukujali kama wasemavyo basi  watakutafuta, kwa vile wanajua wapi unapatikana, huna  haja ya kujipendekeza/kubembeleza, na wewe ni binadamu muhimu vilevile.
NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMAMOSI NJEMA. TUPO PAMOJA

Thursday, September 4, 2014

VAZI LA LEO GAUNI : NAONA IWE PICHA YA WIKI!!!!

 Ukiwa mfupi kuna kila njia ya kuwa mrefu kwa mfano hapa kusimama kwenye kiti:-) ujanja eehhh . Halafu sijui madada huya anataka kuruka pia.
 Hapa afadhali mdada katulia
Tabasamu kwa mbali.
Gauni hili nimenunua:- Indiska
 

UJUMBE WA LEO kutoka kwa Rais Kikwete "TUTATOA ELIMU YA MSINGI, SEKONDARI BURE"


Katika pitapita zangu jana nikakutana na hii habari/ujumbe kama ni kweli kwa kweli ni habari nzuri sana. Nikaona si vibaya nami nikiiweka hapa Maisha na Mafanikio...Nimeipada hapa haya karibuni tujadili kwa pamoja.
 
Rais Jakaya Kikwete amesema serikali inakusudia kufuta karo kwa wanafunzi wa shule za sekondari za serikali, ili kutoa fursa kwa watoto kusoma bure kuanzia elimu ya msingi, ikiwa ni jitihada za kuinua elimu na kuwapunguzia mzigo wazazi.

“Zipo sababu za msingi zinazosababisha wanafunzi wengi wa shule za sekondari kukatisha masomo yao, ikiwamo wazazi wao kushindwa kulipia karo za shule kutokana na changamoto mbalimbali zikiwamo za umasikini” alisema.
Rais Kikwete alisema kufutwa kwa ada hiyo utekelezaji wake upo mbioni ili kuhakikisha kila mtoto anapata elimu bure, hatua ambayo itasaidia kuinua kiwango cha elimu nchini.

Tuesday, September 2, 2014

KAPULYA SI MPENZI WA SCALFU NA KULIMA BUSTANI TU HAPANA ANAPENDA MIKOBA PIA!!!

 Nimeupenda mno mkoba huu rangi yake na jinzi ulivyokaa kaaa
Huu nilinunua nilipokuwa Estonia nako kazuri....Je wewe msomaji unapenda kukusanya nini labda bangili ???au shati? au labda viatu?:-)

Monday, September 1, 2014

MLO WA JANA JIONI.....KARIBUNI!!!!

Hivi ndivyo mlo wetu wa jana ulivyokuwa:- Wali, nyama ya ngómbe na kabichi na hiyo ni sahani yangu kiteremshia ni maji