Tuesday, April 30, 2013

SHUKRANI KWA WOTE MLIOSHIRIKI NASI KATIKA KIPAIMARA CHA BINTI YETU..AMBAYO NI SEHEMU/HATUA YA MAISHA KATIKA MAISHA/KUISHI!!!!

Nachukua nafasi hii na kuwashukuruni wote mliohudhuria siku hii ya kipaimara cha binti yetu iwapo kiukaribu au kwa umbali..Mwenyezi Mungu awazidishie Upendo. Kwa vile Mwanakipaimara anajua kiswahili amesoma maoni ameniagiza kusema AHSANTE SANA kwa kuwa naye kwa siku hii maarufu katika hatua za maisha...AHSANTENI..NA MUWE NA JUMANNE NJEMA..KAPULYA NA FAMILIA.

Sunday, April 28, 2013

JUMAPILI YA LEO NI MAARUFU BINTI YETU CAMILLA ANAPATA KIPAIMARA..HONGERA..

picha ya pamoja baada ya kupata kipaimara Da ´Camilla  hapo katikatika na nywele nyeusi
 
nipo na rafiki
watu walivyofurika

baadhi ya wageni waliokujha kumpongeza Camilla
baadhi ya msosi

 
baada ya misa , sasa hapa nu nyumbani

keki ya karoti
 
kufungua zawadi
Jumapili hii imekuwa ndefu na nyenya baraka nyingi sana katika nyumba yetu ...TUNAMSHUKURU MUNGU KWA SIKU HII...nimeona niwe pamoja nanyi katika siku hii njema, AHSANTE MUNGU....NA HONGERA SANA BINTI CAMILLA

Saturday, April 27, 2013

JUMAMOSI YA LEO TUANGALIE VITENDAWILI VYETU...KITENDAWILI.....

Kwanza nina swali moja hivi kwa nini tunasema KITENDAWILI....na wengine wanajibu...TEGA..???? HAYA KITENDWILI...
1. Huyu mwanamume, huyu mwanamke, hwakutani...
2, Mtoto wangu ninapomtuma mmoja, wanarudi wengi.
3. unga wa kuanika usiku, mchana hakuna.
4. Shamba langu kubwa, ulezi nivunao kiganja kimoja
5. mtu mwenyewe mdogo, watoto wengi.

JUMAMOSI NJEMA KWA WOTE....NASUBIRI MAJIBU:-)

Thursday, April 25, 2013

TANZANIA INA MAKABILA MENGI NA KILA KABILA LINA MTINDO WAKE WA KUENEZA UTAMADUNI WAKE .HAPA NI NGOMA YA Traditional dance, Kisesa...


Haya jamani ilikuwa zamani kidogo na hizi ngoma zetu za asili..karibuni tucheze...mimi nafikiri ni WASUKUMA HAO ..JE WEWE MWENZANGU UNASEMAJE? MUWE NA WAKATI MMOJA

Wednesday, April 24, 2013

KATIKA MAISHA KUNA KUPENDWA NA KUCHUKIWA NA WATU ....!!! UPENDO!!!

Kupenda/upendo ni kitu cha ajabu sana mara nyingi nimekuwa nimejiuliza kwa nini sisi binadamu tuna upendo tofauti kwa kila mtu. Nikisema hivi nina maana kuna wakati mtu inaweza kutokea unampenda mtu kiasi kwamba huwezi kujizuia. Na cha ajabu mara nyingine uanaweza kumpenda mtu ambaye hujawahi kumwona ana kwa ana(uso kwa uso) na upendo ukawa wa nguvu kali sana.
Halafu sasa inaweza kuwa kinyume kabisa. Yaani watu tunaweza kuwa na chuki. Unaonana na mtu siku moja tu na utasikia simpendi kabisa jamaa huyu. Au hata kuangalia tu picha yake unapatwa na chuki. Nashangaa sana kwa uwezo kama huu ambao MUNGU amatupa na pia SHETANI anaingilia na kuharibu.Swali:- Hivi hii inatokana na nini?
Leo nimeona niimbe mwenyewe ila samahani hamtaisikia sauti yangu:
Upendo, upendo, upendo ni amri ya bwana, Yesu alisema pendaneni, pendaneni kama nilivyowapenda. Nanyi pia, nanyi pia mpendane palipo na upendo Mungu yupo nasi tupendane tupendanex2.
NAWATAKIENI WOTE UPENDO NA AMANI KATIKA KILA MFANYACHO...KAPULYA

 

Tuesday, April 23, 2013

KUNA NJIA NYINGI YA KUITANGAZA BENDERA YETU YA TANZANIA...

Nimependa magauni haya nafikiri safati ijayo nami nitashona maana duh nimepeata hamu kweli--kama tusemavyo ni rangi nzuri na kila moja ina maana yake..tukianzia na..
1. Nyeusi- Huonyesha watu wa Jamuhuri ya Tanzania.
2. Kijani - Huonyesha mimea na ardhi ya Tanzania
3. Njano - Huonyesha utajiri wa mali ya asili.
4. Bluu - Huonyesha bahari inayoziunganisha sehemu za Jamuhuri ya Muungano
Haya ni maelezo  ya Bendera yetu ya Jamuhuri ya Tanzania....Si mnakumbuka tulijifunza darasa la tatu-nne vile au?......Nawatakieni wote JUMANNE NJEMA!!!!

Monday, April 22, 2013

SIMBA WEUPE WA PORI LA LIPARAMBA WILAYANI MBINGA MKOANI RUVUMA....!!!

Juzi nilikuwa naangalia habari ya wanyama pori ambayo ilikuwa kuhusu simba waupe huko Afrika ya kusini,,,Mara nikakumbuka ya kwamba Simba waupe wanapatikana pia katika pori la wanyama la Liparamba wilayani Mbinga mkoani Ruvuma. Ina semekana Wanyama katika pori hii kila mwaka wanahamia kutoka nchini Msumbiji kuingia Tanzania. JE WEWE MWENZANGU UMEWAHI KUONA SIMBA MWEUPE???

Sunday, April 21, 2013

JUMAPILI NJEMA KWA WOTE WATAOPITA HAPA...MAISHA NA MAFANIKIO

IMANI YA BWANA IWE NANYI...NA UPENDO PIA BARAKA ZITAWALE NYUMBANI MWENU.

Saturday, April 20, 2013

JUMAMOSI ...UJUMBE WANGU NI HUU....

Ukiwa DUNIANI USIHUZUNIKE na usiwe MNYONGE hata kama una UMASKINI kiasi gani. Mungu yuko pamoja nawe na unatakiwa kuzingatia haya:-
1. Usijilaumu kwa lolote lililokutokea
2. Usihofu kuhusu hali uliyo nayo sasa.
3. Usijilinganishe na mtu yeyote duniani.
4. 5. kumbuka Mungu ndie mpangaji wa kila linalokutokea.
6. Usiwaze sana kuhusu kesho waza kuhusu leo.
7. Kukikosa ulichokikusudia yote ni mipango ya Mungu.
MUWE NA SIKU/JUMAMOSI  NJEMA

Thursday, April 18, 2013

KWA MARA NYINGINE TUANGALIE JAMBO HILI :-MTOTO/KIJANA AFUNGA NDOA NA MAMA YAKE MZAZI BAADA YA BABA YAKE KUFARIKI -SONGEA!!!

Katika pitapita nimekutana na hii mimi na Tanzania ...nikakumbuka hii nikaona niweka hapa  maisha na mafanikio... haya hebu wasikilize maelezo yao pia wanajamii wengine...

Sijui hapa itakuwa laani au ni ukosefu wa akili...inasikitisha sana kwa kweli....Jioni njema kwa wote mtakaopita hapa..Bibi kaongea na kingoni bwana :-)

unaikumbuka hii???- KUAMINI KUWA WAMEKAMILIKA NI KUJIDANGANYA BURE!


unaikumbuka hii? ebu soma tena ni vizuri kukumbuka  zilipendwa....karibu

Wiki iliyopita na wiki hii nimekumbuka sana nyumbani, nadhani ni kwa sababu wiki iliyopita tarehe 17 ilikuwa ni tarehe ambao mama yangu alifariki na wiki hii 23/5 imetimia miezi miwili tangu Mdogo wangu alifariki. Kwa kweli nam-miss sana mama yangu pia mdogo wangu.

Nakumbuka ilikuwa kila nikienda likizo, nilikuwa natumia muda mwingi kuwa jikoni na mama yangu nikizungumza naye simulizi za kale za enzi ya utoto wangu.

Ni simulizi ambazo kwa kweli kila nizikumbukapo huwa natamani yale maisha yajirudie kwani kuna mengi ya kufurahisha na ya kuhuzunisha ambayo kwangu mimi nimejifunza mengi kwako.

Lakini lipo jambo moja ambalo nimelikumbuka, ambalo kwa kweli huwa linanifikirisha sana. Jambo lenyewe ni kuhusiana na baadhi ya marafiki zangu kule nyumbani.

Kusema kweli ule ukaribu niliokuwa nao na baadhi ya marafiki zangu umepungua kiasi cha kukatisha tamaa.

Sababu kubwa ni kutokana na kile walichodai kwa nimewatupa kutokana na kutowasaidia kupata wachumba wa Kizungu. Yupo rafiki yangu mmoja mbaye yeye aliwahi kunitamkia wazi kuwa mimi ni mbinafsi kwa kuwa ni mara nyingi ameniomba nimtafutie mchumba wa Kizungu kwa kuwa ninaishi huku ughaibuni lakini nimeshindwa kumtafutia.

Nakumbuka nilimweleza ukweli kuwa siwezi kumsaidia juu ya jambo hilo kwa sababu liko nje ya uwezo wangu, lakini kutokana na labda tuite ufinyu wa kufikiri, nilimpoteza rafiki huyu kwa sababu ya kushindwa kumtafutia mchumba wa kizungu……..yaani kaaaazi kweli kweli.

Hata hivyo nilijiuliza swali moja, kuwa hivi hakuna wanaume huko nyumbani mpaka mtu aamue kutafuta mchumba wa Kizungu? Je ni mapenzi au ni Uzungu unaotafutwa hapo?

Lakini kwa upande mwingine sikumshangaa sana kwa sababu kwa huko nyumbani ipo silka ya baadhi ya watu ambao wanaamini kwamba kuoa au kuolewa na Mzungu ni jambo la kujivunia sana. Huwa nimezoea kauli za baadhi ya watu kule nymbani kila niendapo likizo wakisema, ‘siyo mwenzako yule, kaolewa na Mzungu’ .

Yaani mpaka leo hii bado kuna baadhi ya watu wanaamini kuwa kuoa au kuolewa na mzungu ni jambo la kifahari na la kujivunia. Kinachotafutwa sio mapenzi tena ni huo uzungu..

Kuna baadhi ya watu wamefikia hatua ya kuamini kuwa sisi waafrika ni duni na wenzetu weupe ni bora na waliokamilika.

Lakini nadhani makosa hayo hayakuanza leo, yameanzia mbali sana. Kwani kizazi na kizazi tumekuwa tukiaminishwa kuwa wazungu ni bora zaidi yetu sisi.

Kwa mfano, mtu kufanya mambo yake kwa umakini na anayefuata muda huyo ataitwa ni mzungu, au mtu asiyependa majungu, uzinzi, uasherati na umbeya naye ataitwa kuwa ni mzungu. Nakumbuka wakati nikisoma kule nyumbani, ilikuwa kama kuna mwalimu ambaye ni mwadilifu kwa wanafunzi na anayewajali, utawasikia wanafunzi wakisema, ‘yule mwalimu ni mzungu’

Yaani kipimo cha kufanya mambo kwa uadilifu na kuwajali wengine kimekuwa kikihusishwa na uzungu, mpaka imefikia mahali kila mtu anatamani kuolewa au kuoa mzungu wakiamini kuwa hao wamekamilika.

Hata huko makazini napo watu wanaochapa kazi kwa uadilifu wanafananishwa na wazungu. Wakati mwingine huwa nacheka kwa sababu naamini hao wanaoamini kwamba mtu kuwa mzungu anakuwa amekamilika ni wazi kwamba hawawafahamu watu hao.

Kwamba kuwa mzungu ni kutokuwa na tabia mbaya, kama uvivu, udokozi, kutojali muda, kusengenya, umbeya, wivu, au kijicho, uzinzi, uasherati, ushoga na tabia zote mbaya tunazozijua hapa duniani, nikujidanganya bure.

Nasema kuamini hivyo ni kujidanganya, kwa sababu kwa wale wanaoishi huku ughaibuni au wale wanaofanya kazi na hawa wenzetu huko nyumbani, watakuwa ni mashahidi wangu.

Kama mlikuwa hamjui ni kwamba hawa wenzetu nakubali kuwa wapo waadilifu na wenye tabia nzuri, lakini pia wapo wenye tabia za ajabu kama uvivu, udokozi, kutojali muda, kusengenya, umbeya, wivu, au kijicho, kutojiamini, uzinzi, uasherati, ushoga na tabia zote mbaya tunazozijua hapa duniani.

Ule udhaifu tulio nao pia wenzetu hawa wanao tena wenzetu hawa wamepitiliza. Ila kutokana na kudanganywa na TV na hizo kauli za wazee wetu tumejikuta tukiamini kitu ambacho hakipo.

Mie wakati mwingine huwa nashangaa pale ninapokutana na baaadhi ya Watanzania wenzangu ambao wanaishi au wamewahi kuishi huku ughaibuni wanapozungumza kwa kubana pua kama hawa wenzetu. Wanashindwa kujua kwamba ile ni lafudhi ambayo inatokana na lugha yao. Ni kama pale unapokutana na Mmakonde, Mngoni au Msukuma au Mpare anapoongea Kiswahili kwa lafudhi ya lugha yao.

Mbona wenzetu kwa mfano Wanaijeria au Wakenya wanaongea kwa lafudhi ya lugha zao. Ni rahisi sana kumtambua Mkenya au Mnaijeria kutokana na lafudhi yake pale anapoongea Kiingereza, tofauti na sisi ambapo Tunajitahidi kubana pua mpaka tunajisahau hata pale tunapoongea Kiswahili.
Na ndio maana kuna baadhi ya wanawake huko nyumbani na hata huku ughaibuni wamefikia hatua sasa wanaukataa uafrika na kuanza kujichubua kwa mikorogo ili kuutafuta weupe.

Kuna wakati nilipokuwa huko nyumbani nilishangaa kuwaona baadhi ya wasichana ambao nawajua kabisa rangi zao kuwa ni weusi kama mimi lakini wamekuwa weupe mpaka wanatisha! Tabu yote hiyo ni ya nini?

Tumefikia hatua sasa kila jambo linalofanywa na hawa wezetu tunaiga, na ndio sababu siku hizi tabia kama za ushoga, usagaji na tabia nyingine chafu tunazozishuhudia huku zimetamalaki huko nyumbani.

Sisi kama Watanzania tunazo tabia nzuri ambazo hawa wenzetu wanazitamani sana tofauti na tunavyodhani. Kwa mfano, sisi ni kawaida mtu kuamka na kupita nyumba mbili tatu na kuwajulia majirani zake hali, au kuingia nyumba yoyote na kama akikuta chakula akala bila wasiwasi.

Kwa upande wa Misiba au harusi watu wamekuwa wakichangiana na kusaidiana kwa hali na mali, yaani tumekuwa na ushirikiano wa hali ya juu tofauti na wenzetu hawa.

Kuwa mzungu haimaanishai kuwa mwadilifu wala kuwa na tabia nzuri, bali tabia nzuri inatokana na tabia ya mtu na malezi kwa ujumla wake, hakuna mahusiano yaliyopo kati ya uadilifu, tabia nzuri na uzungu. Nasisitiza kuwa hakuna kitu kama hicho, ni kujidanganya bure.

Inashangaza kuona kwamba, badala ya kujivunia tabia hizi nzuri tulizo nazo ambazo hata hivyo wenzetu wanazitamani, tunatamani za kwao ambazo nyingi ni mbaya na zenye kuumiza.
Tubadilike………………

Wednesday, April 17, 2013

BIBI KIDUDE AMEFARIKI DUNIA MAPEMA ALFAJIRI LEO..UTAKUKUMBUKWA DAIMA!!

Hapa ni Bi Kiduka katika uhai wake akipiga ngoma..
Upumzike kwa amani utakumbukwa daima.

Tuesday, April 16, 2013

KANGA YA VIKOMBE VYA CHAI...NIMEIPENDA HII KANGA!!!!!

Maandishi yanasema ISIKUHADAE RANGI TAMU YA CHAI NI SUKARI...Hivi ni kweli?

Monday, April 15, 2013

EBU LEO TUANGALIA BAADHI YA MAKUNDI MBALIMBALI YA WATU HAPA DUNIANI...

Katika hii dunia kuna watu wa aina mbalimbali...
kundi la kwanza: Kuna watu wanajua lakini hawajui kwamba wanajua. Hawa wanaitwa wasahaulifu na sisi tunatakiwa tuwakumbushe.

kundi la pili:- Kundi hili ni kwamba wengine ni maskini wa Mungu hawajui lakini Mungu amewabariki wanajua kwamba hawajui . Hao ni wajinga na sisi inabidi tuwaelimishe.

kundi la tatu:- Hawa wengine wao wanajua na wanajua kwamba wanajua. hawa waelevu nasi tunahitaji kujifunza toka kwao kwa vile wao ni waelevu.

Na kundi la nne: Wengine hawajui na wao hawajui kwamba hawajui wabishi. Hawa ni wapumbavu ..hawa inabidi tuachane nao kabisa. Mhhhh..najiuliza sijui ni kundi gani nipo???
JUMATATU NJEMA KWA WOTE...

Sunday, April 14, 2013

JUMAPILI NJEMA KWA NA AMANI ITAWALE NDANI YA NYUMBA ZENU....

Wote mnapendwa sana ...na tuzidi kupendana..JUMAPILI NJEMA SANA....

Friday, April 12, 2013

LEO TULIKUWA TUKIMSINDIKIZA DADA YETU MPENDWA MARIANA KATIKA SAFARI YAKE/MAKAO YAKE YA MILELE....

Kama nilivyowataarifu hapa basi leo imekuwa siku ya mwisho kumsindikiza dada yetu, Mama yetu na rafiki yet mpendwa Mariana katika makao yake ya milele..................................................................


HAPA NDIPO ATAKAPOLALA DADA MARIANA
 PAMOJA NA MWANAE MANUELA
Siku ya leo imekuwa siku ndefu na ya masikitiko kwa familia, ndugu jamaa na marafiki na imekuwa siku ya kujifunza mengi kwangu, kutoka kwa da´mkubwa Mariana kwa kweli. Ama kweli wote watendao mema huwa wanatutangulia kwanza. Katika maisha yangu hapa nimewahi kwenda  kwenya misiba/mazishi mingi/mengi sana lakini huu leo hapana. Watu walifurika kuliko kawaida kiasi kwamba nikajiona nipo kwangu Afrika. Na kanisa lilikuwa halitoshi kabisa. Kweli ukitenda mema utarudishiwa hapa hapa duniani. Watu walifumuka pande zote. Au niseme hivi kwa kifupi dada huyu hakuna neno la kutosheleza maelezo yake kwa kweli,,,,alijali sana wengine na mpaka kujisahau mwenyewe. NITAKUKUMBUKA DAIMA. MWENYEZI MUNGU NA AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI. AMINA

Wednesday, April 10, 2013

PICHA YA WIKI:- WANAWAKE WANAWEZA HATA KABLA HAWAJAWEZESHWA.....

Hapa nimejiuliza mara kumi kumi hivi anawezaje  huyu mama....maana kuendesha baiskeli unahitaji balansi na kuubeba huyo mzigo pia halafu mtoto mgongoni na mtoto nyuma ya baiskeli naye kabeba mtoto ...mmmmhhh hapa kazi  kwelikweli....Lakini kweli hii ni haki kweli/Uungwana kweli??? KILA LA KHERI !!!

KUNA ANAYEJUA HABARI ZA MWALIMU MATONDO MASANGU NZULILIMA????

Nimekuwa mara nyingi nikijiuliza mwalimu Matondo yupo wapi na halafu juzi tu nimeulöizwa na mkereketwa mwingiau niseme mwal. Mhango  kama najua habari na ndugu yetu huyu. Kwa kweli sijui kabisa na sasa naona kichwa kimetawala mno..Je? kuna anayejua habari/kitu chochote kuhusu ndugu yetu huyo? Maana ukiangalia hapa  inaoshesha ni muda sana aliweka kitu...

Tuesday, April 9, 2013

PALE WATU WANAPOJIULIZA KWA NINI WANGONI WANA VIBONGO/MAJINA YA UKOO KAMA WANYAMA????

Dhumuni la leo ni kutaka kumjibibu dada msaidizi katika mada hii swali lake lilikuwa kama lifuatavya hapa chini
Mija Shija Sayi said...Yasinta umependezaje?
Hebu naomba utusaidie wadau wako kwamba, ni kwanini wangoni majina yao mengi wamechukua kwa wanyama?
Ngonyani, Mapunda.. n.k, Je kuna historia yoyote? Kaka S mtaalamu wa mambo ya Tamaduni,swali hili unaweza tusaidia pia..
Asanteni..
------------------------------------------------------------------------------------------------------------
nami nitajaribu kujibu kama ifuatavyo....
Wangoni wanajulikana sana kwa kuwa na mvibongo/majina ya wanyama wa pori, na hata wanyama wa nyumbani ama majina ya miti au hata ya nyasi. hii ilianzia pale ukoo wa mwanzo ulitoka wapi, wangoni wana majina ambayo yanaelezea kile wanachokifanya, jinsi walivyokuwa hapo kale nk- Walipoanza kutembea na kupiga vita na watu wengine ndo hapo wakaongezea  na majina ya wanyama, ndege na ya miti. kwa mfano:- Cawe, Gama, Kapungu, Komba, Kunguru, Mbawala, Nyati, Nguruwe, Ngonyani, Soko, Nyoka na Tembo.....na mengine mengi sitaweza kuyataja yote maana ni mengi mno..

Saturday, April 6, 2013

JUMAMOSI YA LEO NINGEPENDA MLO WANGU UNGEKUWA HIVI...NAOTA NDOTO...

 
 

Nimeamka na kuanza kufikiri huu ungekuwa mlo wangu wa siku ya leo chai kwa maandazi au vitumbua...
 ....chai ya rangi bila sukari
 ...au labda chai kwa Vitumbua na chapati...
Na hapa ungekuwa mlo wangu wa mchana huu sambusa....Sambusa tamu sana ila inabidi uwe na muda haswaaa..
na kumalizia siku kwa ugali kwa samaki na kachumbali kidogo---
kumalizia na glasi ya maji...mmmhhh hivi ndivyo ningependa siku yangu ya leo ningekula lakini sasa sitaweza ....nakula kwa macho. baadhi ya picha nimezipata hapa. JUMAMOSI NJEMA.

Friday, April 5, 2013

NIMEKUMBUKA KWELI NYUMBANI LEO NIKAANZA KUSIKILIZA NGOMA ZETU ZA ASILI..HII NI NGOMA BETA YA WANGONI

NAWATAKIENI WOTE JIONI HII YA IJUMAA YA TAREHE 5/4 IWE NJEMA NA YENYE UPENDO,,,,

IJUMAA NJEMA...NA UJUMBE HUU!!!

Napenda kuwatakieni wote IJUMAA njema sana..kama una nafasi hata dakika tano chukua hizo na msalimu rafiki yako umpendaye na hata tu kumtumia ujumbe. WOTE MNAPENDWA SANA...

Thursday, April 4, 2013

TUSISAHAU METHALI ZETU....!!!!!

1. Watu tunawadhania ni marafiki, mara nyingine ni maadui.. Mpelelezi si rafiki.
2. Mtu akitaka kupata cheo, awe na heshima kwa wakubwa.
3. Kama ukipata mali kwa kazi yako, weka akiba kwa siku za uzee.
4. Ufuate mashauri na maneno ya watu wenye akili.
5. Mtu ana maneno mazuri na matamu, lakini nia yake ni mbaya.
6. Ukiwa mgeni katika nchi, uelekee kadiri watu walivyo.
7. Wakiwa wakubwa wawili, watapata ugomvi, hawawezi kukaa pamoja.
8. Mtu akitangaza habari ya uongo, ni vigumu kusahihisha maneno yake.
9. mtu anaweza kukuchekelea kwa mdomo, lakini katika moyo ana mawazo mengine.
10. Ujitahidi mwenyewe na Mungu atakusaidia.
TUTAENDELEA KUKUMBUSHANA KILA WIKI ILI TUSISAHAU..NA KAMA KUNA MMOJA ANA NYINGINE ANAWEZA KUONGEZEE TU...SIKU NJEMA SANA PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA...KAPULYA

Tuesday, April 2, 2013

WANAMITINDO NA WAREMBO WA WIKI ..JE? UNAWAJUA HAWA WADADA??

Hawa ni kati warembo,wanamrindo waliokuweka katika  COVENTRY WOMEN  Kwa picha na mambo mengine zaidi bonyeza KACHIKI. Ahsanteni wote...

Monday, April 1, 2013

MWEZI WA NNE(APRILI) NI MWEZI KUKUMBUKWA NA MUHIMU KWA HISTORIA YA NCHI YETU

Kwa watanzania wengi ambao wanafuatailia historia na kukumbuka masuala muhimu ya nchi hii mwezi huu una mambo muhimu ya kukumbukwa kutokana na matukio makuu yasiyopungua manne.
Kama ifuatavyo hapa chini.
Ø Baba wa Taifa hayati mwalimu Nyerere alizaliwa mwezi hu wa nne 13/04/19922.
Ø Muungano kati ya iliyokuwa Tanganyika na Zanzibar kuzaliwa kwa Tanzania Ulizaliwa mwezi wa nne 26/04/1964.
Ø Rais wa kwanza wa Zanzibar hayati shekh Abeid Aman Karume aliuwawa mwezi huu wa Nne tarehe 07/04/1972
Ø Aliyekuwa Waziri mkuu wa tatu wa Tanzania Hayati Edward Moringe Sokoine alifariki mwezi hu wa nne tarehe 12/04/1984.
Ø Na kwa mwaka 2013,unaongeza tukio lingine la kuanza utaratibu mpya wa kujadili na kupitisha bajeti ya Serikali kuanzia tarehe 9/4/2013.
Ø Mwaka 2014 utakuwa na tukio muhimu na nyeti litaongezeka katika mwezi huu kutokana na kuendelea kwa mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya ya Tanzania ambayo inatarajiwa kuzinduliwa tarehe 26/04/2014,wakati muungano utakapokuwa unatimiza miaka 50.
Kutokana na matukio manne ya awali tunatakiwa kuwaenzi mzee wetu hayati Abeid Karume, Julius K Nyerere na Edward M. Sokoine ,kuna umuhimu kwa Watanzania kupewa au kukumbushwa kuhusu historia ya Viongozi hawa na tukio la muungano, viongozi hao wana michango ya aina yake katika historia ya nchi hii na kutokana na hilo tunatakiwa kujiuliza nini kama jamii tunaweza kujifunza na kuiga kutoka kwao kwa faida ya kizazi hiki na kijacho.

07/04/1972-KUUWA KWA HAYATI KARUME KWA KUPIGWA RISASI.
Mambo ya kukumbukwa aliyasimamia hayati karume.
Hayati karume aliweza kuwaongoza wazanzibar kuwaondoa watawala wa kisultani
Historia inatuonyesha kuwa karume alikuwa baharia/mvuvi. Karume alisoma mpaka darasa la nne. Kwa kusoma na kuishi darasa la nne na pia kwa kuwa baharia inamaanisha kuwa kiongozi bora na jasiri hakuhitaji kwenda shule kubwa,Uongozi ni kipaji/kujitolea na kujituma. Kiongozi anatakiwa kuongozwa na Uzalendo na siyo ubinafsi kama ilivyo kwa viongozi wengi.

Karume kutokana na kuongozwa na kanuni ya maadili ya asili aliweza kufanya maamuzi ya kijasiri bila ya kujifikiria yeye kwanza pale alipokubali kuunganisha Zanzibar na Tanganyika na kuzaliwa Tanzania,Inasadikiwa kuwa kabla ya Tanganyika kuungana na Zanzibar Mwalimu hayati JK Nyerere alitaka tuungane na Kenya Kenyatta akakataa. Kwa kukubali kwake kuungana na Tanganyika alipoteza sifa ya Ukuu wa Nchi na kuwa Makamu wa Rais kitu ambacho kama hakuwa anaongozwa na uzalendo asingekubali pamoja na kuwa kulikuwa na sababu zingine za kiusalama na za kuharakisha uhuru wa nchi zingine za kiafrika bado kwa uamuzi wake anaingia katika viongozi waliotanguliza uzalendo kwanza kabla ya ubinafsi.

Kutokana na kukubali kwake kuungana na Tanganyika Muungano huu umekuwa wa kuigwa na unaendelea kudumu pamoja na kasoro za hapa na pale. Kuna nchi nyingi za Afrika zilijaribu kuungana lakini kutokana na ubinafsi wa viongozi wa nchi hizo muungano wao haukudumu mfano Senegambia muungano kati Senegal na Gambia.

Karume alikuwa mtu wa vitendo kiongozi anayeonyesha kwa mifano halisi na hai ya kuwatumika wananchi alianzisha wazo la kujenga nyumba za kuishi watu wa maisha ya kawaida Michenzani.

Karume pia aliweza kutoa maamuzi ambayo yanaweza kufananishwa na mzazi katika familia kwa kumteua Dkt Salim A.Salim kuwa balozi mdogo wa Tanzania nchini Misri akiwa na umri wa miaka 22,ambapo katika hali ya kawaida Dkt Salim alikuwa anaonekana mchanga na mdogo na kwa mazoea ya viongozi hata katika ngazi ya familia angeweza kusema huyo ni Taifa la kesho au kiongozi wa kesho. Kwa kumteua Dkt Salimu karume alidhihirisha kuwa ni kiongozi ambaye anaamini kuwa hata vijana wanaweza kusimamia majukumu katika ngazi mbalimbali pale watakapokabidhiwa madaraka hayo kwa nia njema. Kudhihirisha kuwa chaguo lake halikuwa la kubahatisha Dkt Salim alipanda hadi kufikia kutaka kuwa katibu mkuu wa Umoja wa mataifa kama kusingekuwa na mizengwe ya mataifa makubwa. Ikubukwe kuwa dkt Salim ni mmoja kati ya makatibu wakuu wa uliokuwa umoja wa nchi huru za Afrika OAU kwa sasa AU ambaye ametumikia cheo cha ukatibu Mkuu kwa muda mrefu..

Hayati karume anatufundisha kuwa wazazi na viongozi wanatakiwa kuwaamini na kuwajengea moyo wa kujiamini na kujitumia vijana watoto wao ili waweze kusimamia na kutekeleza masuala mbalimbali. Fundisho kubwa tunalolipata kutokana na suala la KARUME kumteua Dkt salim kwa umri wa miaka 22,kuwa kuna umuhimu wa kuwaandaa vijana kuwa viongozi na wasimamizi katika ngazi ya kuanzia katika familia. Mfano tunatakiwa kuhakikisha kuwa tunawashirikisha vijana katika masuala ya utunzaji wa mali na rasimali katika ngazi ya familia na jamii.

Karume ametuachia changamoto kubwa ya kuifanyia kazi katika masuala yanayohusiana na pale tunapotakiwa kufanya maamuzi yanayohusiana na masilahi ya umma na kwa manufaa ya walio wengi. Swali wewe kama kiongozi unajilinganishaje na Mzee huyu ambaye hatuko naye kimwili lakini ambaye anaonekana bado yu hai na ataendelea kuwa hai.

Unajengaje uzima wa milele wa jina lako katika ngazi ya familia na jamii kama viongozi waliotangulia mbele ya haki?

TAREHE 12/04/2008
SOKOINE.
Historia inaonyesha kuwa Sokoine alikuwa ni waziri Mkuu wa tatu wa Tanzania alitanguliwa Nyerere,Kawawa. Alikuwa waziri Mkuu kwa vipindi viwili 1977-1981 na 1982-1984.
Sokoine alikuwa jasiri na alifanya kwa vitendo/alithubutu na aliweza. Kwa kifupi Sokoine alikuwa ana mtazamo wa kufanya kwa mkabala wa kuweza.

Kutokana na ujasiri aliweza kuthubutu na kutenda,Sokoine aliweza kuthubutu na kumshawishi mwalimu nyerere kupunguza baraza la mawaziri wakati huu baraza la mawaziri lilikuwa na mawaziri wapatao 26,alilipunguza na kuwa na mawaziri 13.

Sokoine ndiye muasisi wa kitu kinachoitwa daladala katika miaka ya 1980 lilikuwa shirika la usafiri Dar lilielemewa na idadi ya wakazi jijini Dar na kushindwa kuhimili wimbi hilo sokoine akaamuru kuanzishwa kwa usafiri wa watu binafsi ikumbukwe kuwa wakati huo suala la makapuni na biashara binafsi hazikuwa zinaruhusiwa daladala za mwanzo kabisa zilikuwa canter na zilijulikana kwa jina maarufu (Chai maharage) kutokana na kuwa na viti vya mbao mabenchi ambayo yalikuwa yanatumika sana katika migahawa na ambayo watu wa kipato cha chini hasa kwa jiji la Dar asubuhi walikuwa wanapata kifungua kinywa chai kuchanganya na maharage na maandazi au kitumbua na mkate.

Sokoine ndiye muasisi wa sheria ya nguvu kazi ambayo iliwezesha nchi hii kuwa na uzalishaji wa chakula cha kutosha kutokana na kuisimamia sheria hiyo ya nguvu kazi,Chanzo cha kijiji maarufu cha GEZA ULOLE.
Sokoine kam kiongozi wa kusimamia shughuli za Serikali aliongoza na kusimamia vita dhidi ya wahujumu uchumi (Tunaweza kusema yeye ndiye muasisi wa kweli wa kupiga vita hiki kitu kinachoitwa ufisadi.) pamoja na kuwa katika vita hiyo imeacha makovu lakini funzo tunalolipata ni kuwa Sokoine alijitolea kuwahudumia wanyonge wananchi waliowengi ambao kutokana na matokeo ya vita ya kagera makovu na machungu ya vita hiyo ilisababisha uchumi wa nchi kuyumba na baadhi ya wafanyabiashara kuitumia nafasi hiyo kwa manufaa yao kwa kuamua kuficha bidhaa muhimu ili ziuzwe kwa bei ya kulangua ( Kuliibuka biashara ya ulanguzi kurusha/Sukari, sabuni, hata sigara kwa wanaokumbuka vizuri kipindi cha miaka ya 1980) Vijana wengi wa wakati huo waliacha kusoma(shule za Msingi na sekondari) na kujiingiza katika biashara ya ulanguzi kurusha vitu muhimu ili kujitajirisha. Katika vita hiyo ya wahujumu uchumi Tanzania kwa mara ya kwanza iliweza kushuhudia wafanyabiashara wanatupa mali zao ikiwemo fedha kutokana na jinsi Sokoine alivyosimamia zoezi hilo. Historia inaonyesha kuwa wafanyabiashara wengi wanaongozwa na ubinafsi na kwa maana hiyo hawako tayari kupoteza hata senti tano,lakini waliweza kutupa mali zao.

Tunatakiwa kumkumbuka SOKOINE kwa kuangalia na kusoma yale yote aliyataka kuyafanyia kazi. Mfano hata wazo la kuwa na Usafiri wa treni Dar, (Maarufu treni ya Mwakyembe) ni moja ya masuala aliyokua anafikiria k uyafanyia kazi

SOKOINE KAMA KIONGOZI
Aliongoza kwa maslahi ya wengi wananchi aliokuwa anawatumikia
Alikuwa na sifa ya UJASIRI,KUJITUMA KUWAJIBIKA kwa vitendo.
Wewe kama kiongozi wa kisiasa au mtumishi wa umma unajipima vipi na Hayati SOKOINE jikague ili uone kama unaweza kuvaa viatu vya marehemu sokoine hata kama au kukubana?

13/04/1922-KUMBUKUMBU YA KUZALIWA KWA HAYATI BABA WA TAIFA.
Historia inatuambia kuwa mwl alizaliwa mwaka 1922 kijiji butiama katika wilaya ya musoma Mkoani mara,alianza shule akiwa na miaka 11,baada ya kuwa mchungaji wa mifugo hasa ng
ombe. Mwalim alisoma shule ya msingi inayoitwa mwishenge na baada ye kuendelea na masomo ya sekondari katika shule ya sekondari Tabora ,mahali alikoanza kuonyesha au kujipambanua kuwa yeye ana sifa za kuwa kiongozi kwa kuwa kiongozi wa serikali ya wanafunzi na alikuwa anasifa ya kutetea wanafunzi wake, sifa nyingine alikuwa na mtazamo wa kimapinduzi/ukombozi hasa katika michango yake aliyokuwa anaitoa katika debeti (Mijadala iliyokuwa inaendeshwa katika shule enzi hizo ambayo ilikuwa inahusisha na kuchambua mada mbalimbali hasa katika masomo ya historia na kiingereza.

Mwalimu aliendelea na harakati za masuala ya ukombozi hata alipokuwa katika chuo Makerere nchi Uganda.
Baada ya kumaliza masomo ya chuo kikuu mwalimu aliaajiriwa kama mwalimu katika shule ya sekondari pugu na kuendelea na harakati za ukombozi kwa kushiriki katika kuasisi uanzishaji wa chama cha Tanu Mwaka 1954 kutoka TAA. Ili kuonyesha kuwa mwalimu alikuwa amejipambanua kuwa ni mwalimu na mwalimu ni kioo cha jamii alikubali kuacha kazi ya ualimu na kuendelea na masuala ya ukombozi wa watanganyika (Kuthamini maslahi ya wengi na siyo ubinafsi). Mwalimu wakati anajikita katika masuala ya siasa ili kupigania uhuru alikuwa na miaka 32 tu,umri ambao katika hali ya kawaida katika miaka ya sasa hivi unachukuliwa kama kijana hajakomaa kuwa katika masuala ya uongozi wa kitaifa wakati si kweli.

Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ni nani katika historia ya Tanzania,Afrika na Dunia kwa ujumla?
Mfano:-  Mwl.  Nyerere alikuwa kama taasisi ya kutuwezesha kupata viongozi kwa mfumo aliuenzi-Mwinyi na Mkapa ni matokeo ya mwalimu kuwa kama taasisi.
Mwalimu alikuwa kiongozi anayeongozwa na UTU na kujali maslahi ya wengi,alikuwa Muasisi na kukubali DSM kuwa makao makuu ya kamati ukombuzi wa Nchi za kusini mwa Afrika na yeye kuwa kiongozi wa Nch zilizokuwa mstari wa mbele katika mapambano ya ukombozi wa Nchi za kusini mwa Afrika, Msumbiji, Angola, Namimbia, Zimbabwe na Afrika ya Kusini.
Mwalimu alikuwa kiongozi wa wanyonge kumbuka mwalimu alikuwa Mwenyekiti wa kamati ya SOUTH SOUTH Commision,Kamati iliyoundwa na Nchi zinazoendelea kuangalia na kupendekeza mfumo wa Uchumi mara baada ya kwisha kwa vita baridi iliyokuwa inaongozwa na Nchi za Urusi na Marekani.

Pamoja na mapungufu yake kama binaadmau bado anabaki kuwa kiongozii wa mfano aliyepata kutokea katika Nchi yetu, Bara la Afrika na Dunia.
Mwalimu anatuonyesha kuwa Uongozi ni suala la kujitolea kwa maslahi ya walio wengi na si suala la kujinufaisha. Kiongozi unatakiwa kuwa na msimamo thabiti na usio yumba,kumbuka mwalimu alipewa jina la utani la HAAMBILIKI kutokana na kusimamia katika kile anachoamini.
Mwalimu alikuwa kiongozi mwenye maono,SIASA YA UJAMAA NA KUJITEGEMEA,pamoja na mapungufu yaliyojitokeza katika utekelezaji wa siasa ya Ujamaa na kujitegemea ,suala la kujitegemea katika familia na kama taifa halina mjadala, na kuamini kuwa binaadamu wote ni sawa kwa maana katika hali ya kawaida sisi binaadamu thamani yetu ni huo UBINAADAMU na si kile unachomiliki.

 26/04/1964 NI SIKU YA MUUNGANO WA ILIYOKUWA TANGANYIKA NA VISIWA VYA UGUNJA NA PEMBA(ZANZIBAR NA KUZAA TANZANIA)
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar pamoja na sababu nyingi zinazotolewa za masuala ya kiulinzi na usalama na undugu wa asili kutokana na watu wa kutoka Tanganyika wengi kulowea katika visiwa vya ugunja na pemba kufanya kazi za manamba katika mashamba ya mikarafuu,kazi za ulinzi na uvuvi. Sababu kubwa ni kutaka kurudisha udungu huo na pia kuhakikisha kuwa wazo la kuwa na Afrika moja linatimia kwa kuunganisha nchi na kanda na baadae kuwa na muungano wa Afrika ambao utakuwa umejengwa kwa misingi ya kueleweka miongoni mwa mataifa ya Afrika na ikumbukwe kuwa huu ndio ulikuwa mtazamo wa baba wa taifa katika suala la kuwa na muungano wa Nchi za Afrika kwa lengo la kuwa na Sauti ya pamoja katika masuala mbalimabali ya kiuchumi kijamii,kisiasa na kiutamaduni. Nini kimetokea na nini kinaendelea ni suala la kulijadili na kuliangalia kwa mapana bila ya kuwa na mtazamo wa nani anapata nini na nani anakosa nini. Je muungano huo unaweza kuwa soma kwetu katika kufikiria mustakabali wetu kama Taifa na hasa katika kipindi hiki cha viguvugu la katiba mpya. Wewe unasemaje.
Vipi suala la muungano katika familia zetu linadumishwa au ndo kila siku migogoro. Tujadili kwa pamoja.