Friday, December 14, 2012

BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIA KUTOKUWA HEWANI KWA MUDA ..NAKWENDA KULA LIKOLO LA NANYUNGU:-)NYUMBANII NI NYUMBANI!!!

Hali ya hewa ndivyo ilivyo leo  DAKIKI/DAKIKA MBILI ZILIZOPITA...yaani mtu unaonekana mnene kama vile tembo kwa ajili ya kuvaa mingua mingi ili usisikie baridi. Nina furaha kuachana na hali hii kwa muda .. nisemapo hivi ni kwamba BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIA INATAKA KUSEMA HAITAKUWA HEWANI KWA MUDA KUTOKANA NA MAMA WA MAISHA NA MAFANIKIO ATAKUWA SAFARINI. Nachukua nafasi hii kuwatakieni wote CHRTITMAS NJEMA NA PIA MWAKA MPYA NA PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA HAPO MWAKANI 2013.
Labda tu Remmy Ongala afichue wapi nakwenda..... na kipande hiki cha mziki..

Narudi nyumbani eeeeh nakwenda kula likolo la nanyungu....wangoni wote myumwike..nyumbaniiiiiii

Wednesday, December 12, 2012

NIMEUPENDA UBUNIFU HII ...AKILI NI MALI KILA MTU ANA ZAKE/USITUPE VIZIBO VYA BIA/SODA NI MALI!!!

Mwaka jana nilipita Mikumi katika maduka waozayo mambo ya urembo na vitu vingine..Nilishikwa na mshangaO baada ya kuona hizi heleni zilizotengenezwa na vizibo vya sodana bia (visoda). Nilipenda sana ubonifu wao na binti yangu akaniambia twaweza pia kufanya kazi hiyo kwa mikono yetu. Lakini, kumbe si kazi rahisi. Nawasifu watu waliofanya kazi hii kwa mikono yao. kunywa soda au bia yako na vizibi ( visoda ) usitupe ni mali... NAWATAKIENI WOTE SIKU HII YA JUMATANO IWE NJEMA SANA NI SIKU MAALUMU MAANA NI TAREHE 12-12-12..KILA LA KHERI!!!

Tuesday, December 11, 2012

KUMBUKUMBU .....TANZANIA!!!!!

 Shamba la katani ...ni Morogoro karibu na mlima wa Uluguru


Twiga wa Serengeti
Ngorongoro Crater

Sunday, December 9, 2012

JUMAPILI YA LEO NI JUMAPILI AMBAYO IMEANGUKIA SIKU AMBAYO TULIPATA UHURU 9/12/1961...


Nami nimea si wimbo huu wa maombi unafaa sana kwa siku ya leo. NACHUKUA NAFASI HII NA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI NJEMA NA PIA SIKU HII KWA UJUMLA

Friday, December 7, 2012

SALAMU/UJUMBE KUTOKA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO IJUMAA YA LEO NI:-

Kila CHOZI ni ishara ya MAUMIVU. Kila ukimya ni ishara ya UPWEKE, kila TABASAMU ni ishara ya FURAHA, lakini kila ujumbe ni ishara ya kum-mis/kumtamani mtu. NAWATAKIENI WOTE MTAOPITA HAPA  ASUBUHI ,MCHANA, JIONI AU NISEME TU IJUMAA NJEMA.....KAPULYA!!!!

TUANZE MWISHO WA JUMA HILI NA WIMBO HUU MALAIKA NAKUPENDA NA MIRIAM MAKEBA....


NAPENDA KUWATAKIENI WOTE MWISHO MWEMA WA JUMA NA MATUMAINI YANGU TUPO PAMOJA...KAMA UTAKUWA UNAENDESHA WALE WENYE THERUJI ENDESHENI TARATIBU MAANA KUNA AJILI NYINGI ZIMETOKEA MPAKA SASA..IJUMAA NJEMA....

Nilipoendelea kutafuta zaidi wimbo huu wa MALAIKA...nikakutana na hawa nadhani ni wachina nao wanaimba ebu wasikilize ukipata muda....

Kweli kiswahili sasa kinaenea dunia nzima....haya kila la kheri!!!!

Thursday, December 6, 2012

JINSI WATOTO WA KIKE WANAVYOJIFUNZA MAISHA ...

....mtoto umleavyo ndivyo akuavyo..ila kuna wakati katika jamii yetu huwa tunazidisha kidogo..mtoto anakuwa kama mtu mzima kabisa. Kwa maana hiyo anakosa ule muda wa kuwa mtoto. Ila tumejifunza mengi na tumekuwa kwa kiutu uzimauzima si kama sasa..au wenzangu mliopitia maisha haya mnasemaje?..Duh!  siku zinakimbia tayari leo ni Alhamisi ya tarehe 6/12/2012..KILA LA KHERI WANDUGU!!!!

Wednesday, December 5, 2012

MCHANA WA LEO NINGEPATA MLO KAMA HUU NINGEFURAHI SANA LAKINI SASA ITANIBIDI NILE KWA MACHO....

Ni ugali kwa mlenda uliochanganywa kwawa majani ya maboga na ambayo bamia. Halafu  bakuli la (ma)tembele la kuchemshwa kwa nyanya na kitunguu. Bila kusahau pilipili shamba.
Hakika hapa ni utamu, na tena ule wa asili kabisa ,yamu yamu yamu....NAWATAKIENI WOTE SIKU /JUMATANO NJEMA SANA.

Tuesday, December 4, 2012

NIMEUPENDA UJUMBE HUU:-)

Nimeupenda ujumbe huu kwa kweli ...nahisi nawe unayesoma umeupenda pia basi ngoja niwatakieni wote mtakaosoma siku njema.PAMOJA DAIMA...

Monday, December 3, 2012

HIVI NDIVYO HALI YA HEWA ILIVYOKUWA FINLAND LEO!!!

Hali ya leo Finland...hapa kwetu bado haijaangua kihivyo ila kuna baridi kali sana kiasi kwamba ile kutoka tu nje pua inasinyaa kabisa....Mwaka huu itakuwa kali kwelikweli...JIONI NJEMA KWA WOTE.....

MWANAFUNZI ABAKWA MPAKA ANAPOTEZA FAHAMU MKOANI RUVUMA!!!

JESHI LA POLISI mkoa wa Ruvuma limefanikiwa kumtia mbaroni Daud Ndunguru (19) wa mtaa wa Hoahoa uliopo Mbinga mjini na linaendelea kumsaka na mwingine jina lake ambaye halikufahamika mara moja linaendelea kumsaka kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wa kike wa umri wa miaka 12 (jina lake limehifadhiwa) anayesoma darasa la nne katika moja ya shule za msingi zilizopo Mbinga mjini na kumsababishia maumivu makali na kupoteza fahamu.

Habari zilizopatikana jana mjini hapa ambazo zimethibitishwa na kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Deusdedit Msimeki zimeeleza kuwa tukio hilo lilitokea desemba 2 mwaka huu huko katika mtaa wa Kihaha nje kidogo ya Mbinga mjini ambako mwanafunzi wa kike inadaiwa alibakwa na watu wawili akiwemo Daud Ndunguru ambaye alikamatwa muda mfupi baada ya kumfanyia kitendo cha kinyama msichana huyo na mwenzake ambaye jina lake halikuweza kufahamika alikimbia na kutokomea kusikojulikana.

Habari zaidi za tukio hilo zimefafanua zaidi kuwa watu hao wawili akiwemo Ndunguru majira ya saa 4:30 usiku walimvizia njiani msichana huyo na kumlazimisha atoe nguo alizokuwa amevaa na kisha kumfanyia kitendo cha ubakaji jambo ambalo limesababisha msichana huyo kupata maumivu makali sehemu za siri na kusababisha kupoteza fahamu.

Hata hivyo kamanda Msimeki alisema kuwa kufuatia kuwepo kw purukushani hizo majirani watoka na kwenda kwenye eneo la tukio ambako walifanikiwa kumkamata Ndunguru na mwenzake alikimbia huku msichana huyo akiwa amepoteza fahamu na walimchukua na kwenda nae kituo cha polisi cha kati cha polisi ambapo walichukua hati ya polisi ya matibabu (PF3) na kwenda nae hospitali ya serikali ya wilaya ya Mbinga ambako amelazwa na anaendelea kupata matibabu na hali yake inaendelea vizuri.
Kamanda Msimeki alisema kuwa mtuhumiwa Ndunguru anatarajiwa kufikishwa mahakamani pindi upelelezi wa tukio hilo utakapo kamilika na jeshi la polishi mkoani Ruvuma linaendelea kumsaka mtuhumiwa mwingine wa tukio hilo anayedaiwa kukimbia na kutokomea kusikojulikana baada ya kumfanyia kitendo cha kinyama msichana huyo
Habari hii nimeipata hapa

Saturday, December 1, 2012

SIKU YA LEO NIMEKUMBUKA LUNDO MBAMBA BAY 2007

Hapa kutoka kushoto ni kaka yangu wa mwisho Philoteo, katikati ni mjomba wangu mwl. John Bosco Ngonyani anajulikana zaidi kwa jina la JB na mwisho ni mwenyewe Kapulya. Siku hii ilikuwa siku ya furaha sana katika maisha yangu kwani nilikuwa sijaonana na mjomba wangu mpendwa karibu mika ishirini ...Muwe na  WAKATI MZURI PIA JUMAMOSI NJEMA YA MWEZI HUU WA KUMI NA MBILI AMBAYO NI YA KWANZA  NA KESHO NDO TUNAANZA KUSUBIRI ULE UJIO /KUZALIWA WA/KWA BWANA YESU KRISTU.

Neno La Leo: Fikiri Kuwa, Sayari Tunayoishi ( Dunia) Ni Jehenamu Ya Sayari Nyingine..​.!

Ndugu zangu,

Kwamba kuna viumbe kwenye sayari nyingine wenye kukesha wakiomba kwenye nyumba zao za ibada, kuwa Mungu wao awaepushe na balaa la kuwaleta kwenye sayari dunia. Dunia iliyo zaidi ya tambala bovu. Dunia iliyojaa wanadamu wenye roho za wivu, kinyongo, inda, husda na nyinginezo. Wanadamu wenye kutakiana mabaya badala ya mema.

Na mfano ni huyu aliyeomba sana kwa Mungu ashushiwe rehma. Siku moja akashukiwa na malaika. Akaambiwa, kuwa Mungu amepokea maombi yake. Kwamba anamtaka mwanadamu huyu achague jambo moja ili ashushiwe. Na akishachagua moja, basi, Mungu atampa jirani yake mara mbili ya kitu alichochagua.

Mwanadamu yule akamwambia malaika; " Basi, niache kwanza nitafakari". Baada ya kutafakari kwa muda,mwanadamu yule akatamka; " Namwomba Mungu anipe chongo!" Kwamba kwa vile alimwonea kinyongo jirani yake apate mara mbili ya atakachokipata, mwanadamu yule aliona ni heri Mungu amtoboe jicho lake moja, awe chongo, na jirani yake atobolewe mawili, awe kipofu!

Naam, fikiri kuwa sayari tunayoishi yaweza ni jehenamu ya sayari nyingine. Kumbuka, nimesema fikiri, hivyo basi fikiri kwa bidii...yaweza kukusaidia kupata jibu la kwanini nchi yetu ni masikini, na watu wake pia.

Na hilo ni Neno La Leo.

Maggid Mjengwa
Iringa.
0788 111 765
Nimetumiwa na http://mjengwablog.com.