Sunday, November 30, 2008

SALA YA MKE KUMWOMBEA MUMEWE

Napenda kufunga mwezi huu wa kumi na moja kwa sala hii;-

Ee Bwana , ni ajabu,
Jinsi fikra zangu zinavyomrudia kila mara
Huyu, mume wangu,
Mwenzi anayeshiriki maisha yangu kwa namna ya pekee.
Ninapofagia nyumba na mazingira yake,
Nataka kutengeneza nyumba nzuri kwa ajili yake.
Ninapopika chakula vizuri,
Napenda kumfurahisha.
Ninaponunua nguo mpya na kujaribu kuonekana mrembo,
Ni kwa ajili yake tena, Ee Bwana.

Na ninaweza kukuambia kwamba
Ninamwonea fahari,
Anafanya kazi kwa bidii ili kupata riziki yetu;
Ni mtu mwenye haki, mwadilifu,
Naye hujitahidi kutufurahisha.
Kwangu, yeye ni mpole na mwangalifu.
Hunijali na kuonyesha kweli kwamba anajali.
Hunifanya mimi nijiamini mwenyewe,
Anajua jinsi ya kuondoa hofu zangu,
Hunipatia usalama na upendo ambao nahitaji sana.

Ee Bwana, ninakuomba,
Umbariki na umlinde.
Katika safari zake, umfikishe salama.
Kazini mwake, umpe fanaka
N hapa, nyumbani petu naomba apate amani na heri.

Bwana, unisaidie mimi pia
Niweze kuwa yule mke anayehitaji.
Unifanye niwe mtu anayeweza kumwamini daima,
Mwanamke ambaye anaweza kumfurahia,
Niweze kumsaidia asahau matatizo yake,
Niweze kuondolea mbali hofu zake na kupunguza uchungu wake.

Bwana, Wewe ndiwe uliyenipa mume huyu,
Na katika yeye,
Umenipatia sehemu ya nafsi yako mwenyewe.
Ninakusifu kwa ajili yake, Ee Bwana.


Napenda kuwatakieni wote Jumapili Njema.

Friday, November 28, 2008

SALAMU KUTOKA SEMINARY YA PERAMIHO


Karibuni sana Peramiho kuna mengi ya kuangalia

HOSPITALI YA PERAMIHO


Ukipatwa na homa njoo hapa utapata matibabu mazuri tu. Pia nipo hapa uliza tu.

BOOKSHOP PERAMIHO


Ukifika Peramiho usikose kipitia hapa kujipatia vitabu na magazeti ya aina yote. Karibu sana (Kunyumba Kuperamiho) ugali na likolo la nanyungu sasa ndo msimu wake.

Wednesday, November 26, 2008

LEO TUANGALIE:- UGONJWA WA KIDOLE TUMBO/KIBOLE (APPENDIX) HUWAPATA ZAIDI VIJANA

Ugonjwa wa kidole tumbo inasemekana huwapata zaidi vijana kati ya miaka 10-25. Lakini pia wazee na vijana zaidi ya miaka 25 wanaweza kupata. Sio kawaida watoto chini ya miaka 2 kupatwa na ugonjwa huu.

Ulaya na Amerika magharibi kwa wastani moja ya kumo hupa ugonjwa huu. Lakini hapa Sweden idadi ya wapatao ugonjwa huu imepungua.

Katika uchunguzi/utafiti inaonyesha watoto ambao wanapata maziwa ya mama zaidi ya miezi saba wanaepuka kupata ugonjwa huu kuliko watoto wasionyonya maziwa ya mama.

Dalili zake:-

Ghafla,maumivu makali ya tumbo pembeni au juu ya kitovu, pia huahamia chini ya tumbo upande wa kulia na kuwa makali zaidi.


Wengine, baada ya muda hupata joto kali sana, hupoteza hamu ya chakula na hupata kichefuchefu. Wakati mwingine kutapika na kuhara pia.

kwa watoto wadogo na watu wazima dalili huwa vigumu kuonekana.

Tuesday, November 25, 2008

TUANGALIE VYOMBO VYA MICHEZO NA USAFIRI

MICHEZO YA PIKIPIKI

Michezo mingine ni kujitafutia kifo angalia hapa akianguka je?

GARI (SPORT CAR PORSCHE)


Sisemi sana ninyi mtasema

USAFIRI WA BAISKELI NI RAHISI ZAIDI

Karibuni wateja kukodisha baiskeli ni bei rahisi tu.

NI NINI KINAFANYA MAISHA YAWE NA FURAHA?

Hakuna kitu kitakacho weza kufanya maisha ya yako/yangu kuwa na furaha kama hatutakubali kujipokea mwenyewe na kupanga mfumo mzima wa maisha yetu. Wengi tunajikuta katika mahangaiko na mafarakano katika uhusiano iwe wa ndoa, au marafiki wa kawaida. Je? ume/tumesha wahi kukaa chini na kujadili kwa nini hili litokee, na je ni kweli kwamba katika haya yote hakuna jibu kwa matatizo haya.

Mpenzi msomaji katika kuchunguza hilo nimegundua kwamba tulio wengi hatuipi nafasi mioyo yetu kuchagua kile kilicho halali kwa matakwa yetu. Bali tunafuata mwelekeo wa mapendeleo yetu na tunaacha nafasi muhimu ya moyo kuupa nafasi ya kuchagua kilicho cha thamani zaidi ya furaha ya siku moja, ambao tuluo wengi tumekuwa tukililia au kuionea fahari. Hapa nina maana kwamba kama mwanamke ameahidiwa kuolewa basi atataka haja hiyo itekelezwe wakati hana uhakika wa kweli kama mpenzi wake anampenda kwa dhati.

Kuna misemo isemayo kwamba:- mwanamke anapotoa uamuzi wa kuolewa anafanya hivi akitegemea kwamba mwanamume anayeolewa naye atabadilika baada ya wao kuwa mke na mume; poleni sana wanawake tumepotea, dadili mwelekeo olewa na mtu mwenye mapenzi ya dhati na ambaye yupo tayari kutoa dhamiri yake kwa ajili yako.

Na kwa upande mwingine, Mwanamume anamwoa mwanamke na kumleta ndani ya nyumba akitegemea kuwa hatabadilika; Mungu ndiye ajuaye kuwa mwandamu ni kigeugeu, sasa atutendee nini ndipo tulidhike? Naamini wanawake wengi wanavumilia katika mahusiano ila wapo ambao nao ni wasumbufu, kwa sababu tu ya tamaa, na wengine hujikuta wanabadilika kwa kuwa maisha ni magumu ndani ya ndoa, na wengine umaskini, wanataka kupata chochote au kuiga ufahali wa wengine.

Swali linakuja je? unafikiri kukamatana ugoni na kuonyeshana kwenye vyombo vya habari kwamba nataka kumshikisha adabu ajifunze ni njia sahihi ya kutatua matatizo katika jamii kama watu hawata tumia njia ya kuiweka wazi mioyo yao kwa kile wanacho kipenda na kukitamani?

Ni changamoto kwamba kweli tulichokiamua pamoja na kukubaliana basi kiheshimiwe na kuthaminiwa kama kweli humpendi mwenzako sema tangu mwanzo liwe wazi tusitake maisha ya mtelemko kwa kuwa unayemwoa ana nafasi nzuri na wewe unavimba kichwa kwa sifa ya kazi yake na sio mapenzi ya kweli. Wewe utakuwa msaliti.

Maisha ya ndoa ni kuwa tayari kwa ajili ya mwingine wakati wa raha na shida, kwa furaha na amani bila majuto.

Monday, November 24, 2008

KATIKA MAISHA KUNA KUPENDWA NA KUCHUKIWA NA WATU

Kupenda/upendo ni kitu cha ajabu sana mara nyingi nimekuwa nimejiuliza kwa nini sisi binadamu tuna upendo tofaoti kwa kila mtu. Nikisema hivi nina maana kuna wakati mtu inaweza kutokea unampenda mtu kiasi kwamba huwezi kujizuia. Na cha ajabu mara nyingine uanaweza kumpenda mtu ambaye hujawahi kumwona ana kwa ana(uso kwa uso) na upendo ukawa wa nguvu kali sana.

Halafu sasa inaweza kuwa kinyume kabisa. Yaani watu tunaweza kuwa na chuki. Unaonana na mtu siku moja tu na utasikia simpendi kabisa jamaa huyu. Au hata kuangalia tu picha yake unapatwa na chuki. Nashangaa sana kwa uwezo kama huu ambao MUNGU amatupa na pia SHETANI anaingilia na kuharibu.Swali:- Hivi hii inatokana na nini?

Sunday, November 23, 2008

MDUNDUWALO/PERAMIHO 2005

2005 tukiwa Peramiho-Mdunduwalo. Hapo tulitaka kuruka na ungo. Huo hapo nyumba yetu ni ungo wa kupozea ugimbi (pombe)

RUHUWIKO/SONGEA 2007

Kaka zangu watono, baba na mdogo wangu mmoja wa kike. Hapo ni mwaka jana raha sana kuwa na familia kubwa.

Friday, November 21, 2008

HADITHI YA MWANA MPOTEVU

Hiii hadithi inanikumbusha mambo mengi sana sijui wenzangu mnasemaje?

Kulikuwa na baba mmoja aliyekuwa na watoto wawili wa kiume. Siku moja yule wa mwisho akamwambia baba yake : baba mimi sasa ni mkubwa naomba haki yangu nataka kuondoka kwenda mbali kutafuta maisha. Baba yake akampa pesa nyingi tu. Akaondoka akaenda zake na pesa zote.

Muda si mrefu akapata marafiki wengi tu. akawa anakula na kunywa nao pamoja na yeye ndiye aliyekuwa analipa kila kitu.

Lakini muda si mrefu pesa zote zikamwishia. Akawa hana kitu cha kula. Marafiki zake wote hawakumpa wala kumsaidia chochote isipokuwa walimtupa barabarani.

Siku moja akaondoka akaenda kwa mkulima mmoja na kusema ya kwamba anaomba chakula, aina yoyote ile, na halafu atafanya kazi kwake. Mkulima akamhurumia akampa chakula na akamwambia kazi yake ni kuchunga nguruwe wake.

Hata hiyo kijana bado alikuwa ana njaa. Akaanza kuwaza: kwa nini napata taabu hapa wakati baba yangu ana chakula kingi tu. Narudi nyumbani kwa baba tena. Nataka kufanya kazi kwa baba kuliko hapa.

Mara akaanza safari ya kurudi kwa baba yake. Na kusema baba, naomba radhi nimekosa. Ilibidi nisirudi na wala usinipokee tena hapa nyumbani kwako. Lakini baba kwa uchungu wa furaha akamkumbatia na kumpokea. Kwa furaha kubwa baba akamfanyia kijana wake sherehe kubwa kwa kufurahia kwa sababu kijana wake alikuwa amerudi tena kwake.

Kaka mtu akawa anarudi toka kazini(shambani) akakutana na babake asemaye. Mdogo wako amerudi tena nyumbani njoo tumsherehekee. Alipotea sasa amerudi tena.

Swali: Je? Hadithihii wewe inakufundisha nini?
Na je? ungekuwa wewe ni yule kaka mkubwa ungefanyaje?

Wednesday, November 19, 2008

MAISHA YA BINADAMU NI SAWA NA MAISHA YA KUKU


Mama na watoto wake tangu miezi tisa tumboni mpaka wanaanza darasa la kwanza wanamaliza na siku moja anabaki mama na baba tena peke yao kama walivyoanza maisha. Angalia hapo juu kila mama aendapo nao wapo. Mmh kazi kweli kweli.

MAISHA YA MAMA KUKU


Ebu angalieni hapa halafu fananisha na hapo juu. Maisha ya kuku hayaachani sana na ya binadamu. Kwani kuku ana bahati yeye anaatamia mayai wiki kama tatu hivi. Hapo tayari anatotoa vifaranga na atavitunza na kuvilinda na maadui wabaya kama vile mwewe na kadhalika. Baadaye wakiwa wakubwa anawadonoa hapo ndio kuwaambia SAMAHANI sasa muda umefika kwa ninyi kujitegemea.

Tuesday, November 18, 2008

SWEDEN NA MISITU YAKE

Ngoja leo tutembelee Sweden kuangalia mali asili(misitu)

Nitajaribu kutafsiri kwa kifupi tu yale mambo muhimu yaliyoandikwa hapo chini kwa kiswidi

Sweden ni nchi tajiri kwa misitu kati ya nchi zote duniani kama ukiangalia uhusiana baina ya maeneo ya misiti na uwingi wa watu. Kwa wastani kila mtu ana hekta 2,5 ya msitu.

Hekta milioni 41 hapa Sweden ni ardhi. Hekta milioni 23 ni misitu. Na zaidi ya nusu la eneo la nchi ni misitu.

Katka misitu hiyo zaidi ni misonobari na spruce(jamii ya misonobari)


Sverige består av 41 miljoner hektar land. 23 miljoner hektar är täckt av skog. På mer än halva landytan växer det alltså skog.
Skogarna består mest av tall och gran. Lövskogen är vanligare ju längre söderut i landet man kommer. I nordvästra Sverige ligger fjällkedjan med kalfjäll och fjällbjörkskog.
Sverige är ett av de skogsrikaste länderna i värden om man ser till förhållandet mellan areal skog och folkmängd. Vi har ungefär 2,5 hektar skog per person.



Sjöar och vatten drag9%= maziwa na mito 9%
Jordbruksmark 8% = Mashamba8%
Berg och fjäll = Milima 10%
Våtmarker 10%= Sehemu za majimaji(adimba) 10%
Produktiv skogsmark 51%= Sehemu nzuri za mavuno 51%
Övrigt 12%= Iliyobaki 12%


TAFSIRI YA HAPA CHINI

Kama ukijumlisha pamoja mimea yote kwenye miti utaona ya kwamba misitu hapa Sweden inachukua kwa wastani milioni 100 m3 kila mwaka. Pamoja na hivyo kila mwaka huvunwa kwa wastani milioni 85m3 . Pichi hiyo hapo chini inaonyesha jinsi miti inavyo kua.

Om man slår ihop tillväxten på alla träd ser man att skogen i Sverige växer med ungefär 100 miljoner m³ varje år. Samtidigt så avverkar vi omkring 85 miljoner m³ varje år. Det innebär att vi får större och större virkesvolym i landet. Idag har vi faktiskt dubbelt så stor virkesvolym som vi hade för hundra år sedan! Figuren här nedan visar virkesförrådets utveckling.








TAFSIRI YA HAPO JUU

Övriga privata ägare6%= Wamiliki wengineo binafsi 6%

Private enskilda ägare 51%= wamilikaji binafsi (kila mmoja) 51%

Private aktieblog 24%= Kampuni binafsi 24%

Övriga allmänna agare 1%= Wamiliki wengineo kwa ujumla 1%

Staten 18% = Serikali 18%

Sveriges landareal 41,1 milj. ha
Skogsmarksareal 22,7 milj. ha
Urskog ca 85 000 ha
Ädellövskog ca 150 000 ha
Tätortsnära skogar ca 300 000 ha
Kustnära skogar ca 450 000 ha
Virkesförråd 2 666 milj. m³sk
Årlig tillväxt ca 96,2 milj. m³sk
Årlig avverkning ca 70 milj. m³sk
Genomsnittlig volym av slutavverkningsträd från 0,20 m³sk i norra Sverige till 0,40 i de södra delarna av landet
Genomsnittlig volym vid slutavverkningar 203 m³sk/ha

Monday, November 17, 2008

MISITU NA WANYAMA WAKE HAPA SWEDEN HAPA NI AINA YA KONGONI(moose)




Mnyama huyu hapa Sweden ndiye mfalme wa msitu.

DUBU (Bear)




Kama mnavyooona hapa hii picha nimepiga mwenyewe kwani hapa ilikuwa karibu na siku zangu za mwisho. Nilikuwa mstuni natafuta uyoga, uroho wa uyoga. Lakini naona siku zangu zilikuwa bado.

MISITU YA SWEDEN NA WANYAMA WAKE

Sunday, November 16, 2008

AMRI KUMI ZA MUNGU

Leo ni jumapili nimeamka na nimeona afadhali nimkumbuke mungu kwa kuzikumbuka hizi amri.

1. Usiwe na miungu mingine ila mimi.

2. Usijifanyie sanamu ya kuchongo.

3. Usilitaje bure jina la BWANA , Mungu wako.

4. Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.

5. Waheshimu baba yako na mama yako upate heri na miaka mingi duniani

6. Usiue

7. Usizini

8. Usiibe

9. Usimshuhudie jirani yako uongo

10. Usitamani chochote alicho nacho jirani yako.

Je? Kwa mtazamo wako hizi amri zinatekelezwa kweli?

Saturday, November 15, 2008

TRACY CHAPMAN NA YASINTA NGONYANI



Je? mwasomaji mnakubaliana na watu wengine wanasema sisi tumefanana. Asiyewahi kusikiliza mziki wake basi sikiliza mimi nampenda huwa namsikiliza.

JE? HAPA NAPENDEZA?




Hapa mwenzenu nilikuwa Saudi Arabia, wanawake wote wanavaa hivi kazi kweli kweli

Friday, November 14, 2008

BAADHI YA METHALI NA MAFUNDISHO KUTOKA KATIKA VITABU VYA WANGONI

1) Methali:- Kweli ikidhihirika uongo hujitenga.


Fundisho:- Kesema ukweli kunatusaidia katika kuweza kuishi na watu vizuri bila
kuelemewa na soni na kujifichaficha ambayo ni madhara ya kusema
uwongo.

2) Methali:- Mkataa pema pabaya panamwita

Fundisho:- Usikubali kufunga ndoa na mtu usiyemfahamu barabara.


3) Methali:- Majuto ni mjukuu

Fundisho:- Kila tunapofanya mipango ya mambo makubwa tuchukue tahadhari yote ili
kukwepa matokeo mabaya.


4) Methali:- Anayejua joto la jiwe ni mjusi
Fundisho:- Tusilete vitu majumbani mwetu bila kujali athari zinazoweza kutupata
sisi wenyewe au jirani zetu kutokana na vitu hivyo.


5) Methali:- Kila ngoma ina wimbo wake
Fundisho:- Wazazi tusiyapuuze matatizo ya watoto wetu hata kama wamekuwa ni watu
wazima. Tuwape misaada au ushauri.


6) Methali:- Aliyekataa ukoo alikuwa mchawi.
Fundisho:- Dumisha ukoo kwani ndugu atakufaa siku ya dhiki.


7) Methali:- Mwenda usiku amesifiwa kulipokucha
Fundisho:- Wewe usumdharau mtu kwa kuwa huielewi shughuli anayofanya kwa sababu
penngine shughuli yake italeta mafanikio na wenzako watamsifu.


8) Methali:- Mwanamume sio ndevu.
Fundisho:- Kila mwanamume anao uwezo. Kwa hiyo ni wajibu kwa wanaume wote kushika
moyo wa kiume.


9) Methali:- Mdomo ukila oua haitaki.
Fundisho:- Watu wengine hawafurahii mafanikio ya wenzao.



10) Methali:- Hasira ya mkizi furaha ya mvuvi.
Fundisho:- Unapokuwa na hasira usifanye jambo lenye umuhimu mkubwa ili kukwepa
kulifanya vibaya.

Wednesday, November 12, 2008

WENGI WANASEMA HIZI NI RANGI ZA WANARASTA




Je? ni kweli ni rangi za wanarasta kwani binafsi pia ni rangi zangu. Nisaidieni basi.Kazi kweli kweli.

MISS JAMAICA 2007+RASTA




Hapa ni dada Yvonne Gayle 2007 alikuwa Miss Jamaica. Swali langu: je? hizo rasta ni za kweli? au? angalieni vizuri.

Tuesday, November 11, 2008

KATIKA MAISHA NI VIZURI KUWAFARIJI MWENYE MATATIZO

Huu ni ushauri wangu mimi kwa wewe iliye na rafiki aliye na matatizo:-

1) Kama rafiki yako ana matatizo usiogope kumwuuliza hali yake kwa ujumla hata kama hali yake inaonekana si nzuri. Kama una matatizo halafu watu/marafiki wanakuuliza U HALI GANI utajisikia amani yaani kuna watu ambao wanakujali haupo peke yako.

Wakati mwingine kunatokea mambo ambayo si kweli na watu wanafikiri kuwa tayari yule mwenye matatizo amepata msaada mtu wa kuongea naye, wakati kumbe wewe upo peke yako kwa hiyo kuuliza ni muhimu sana.

2) Piga simu au nenda ili kujua mpatwa matatizo ana hali gani. Pia pika chakula, nenda kwake na mle pamoja. Wakati matatizo yanapotokea, inakuwa ngumu kuelezea vitu ulivyozoea kufanya kila siku. Kama una watoto inakuwa ngumu zaidi kuwatunza wakati upo kwenye matatizo/majonzi.

3) Onyesha upendo wako, bila kuonekana ni usumbufu kwa mpatwa matatizo, uwe nusu nusu. Usizidishe au usipunguze. HAPO NDIPO UTAWEZA.

Monday, November 10, 2008

MIRIAM MAKEBA AMETUACHA




Ni majonzi makubwa sana kwa dunia nzima lakini hasa Afrika/kusini. Kwa kuondokewa na mwanamke shujaa na Mwimbaji Miriam Makabe alikuwa Italia kusini.Jana usiku alipatwa na homa ghafla alikuwa kule kwa ajili ya kuimba. Miriam Makeba amekufa akiwa na miaka 76.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi AMINA.

Friday, November 7, 2008

KWA NINI JINA WAZUNGU,WAAFRIKA NA CHOTARA?

Baada ya uchaguzi huu wa USA, Nimejifunza mambo mengi kweli watu tuna mawazo tofauti labda naweza kusema UBAGUZI.

Wazungu akizaa na wazungu kinachotokea ni mzungu
mwafrika akizaa na mwafrika kinachotokea ni mwafrika
mzungu akizaa na mwafrika ni mzungu, chotara au mwafrika?
Na nusu mzungu/mwafrika akizaa na mwafrika je tutaita nini?
au akizaa na mzungu mtoto ataitwa nini? Mzungu, chotara au mwafrika. Au kama asilimia 99 mzungu na asilimia 1 mwafrika huyu ataitwa mzungu, mwafrika au chotara?
Swali.- Kweli Obama ni mzungu au mwafrika? na je? watoto wao tutawaitaje? kwa sababu wote mke wa Obama na Obama ni Chotara au nimekosea?

Kwa nini majina yote haya tuache ubaguzi ndugu zangu kwani wote ni binadamu na wote ni mungu ndiye aliyetuumba na damu zetu wote ni nyekundu.

Thursday, November 6, 2008

SAMAKI+MBOGA+CHAKULA



Na bila kituweo huwezi kula ugali. Haya ndugu zangu karibuni ugali na samaki wa kupaka.

KUSONGA UGALI+ CHAKULA




Sio kuandaa tu na kuacha, hapana sasa ni ile kazi ya kuandaa ugali mwenyewe.

KUTWANGA MIHOGO +CHAKULA




Hii kazi ndugu zanguni ni kazi muhimu sana. Hasa wakati ule mimi au sisi wengine tuluipokuwa wadogo. Bila hivyo huwezi kula kwani hizi mashine za kusaga hazikuwepo miaka ile ya -70, 80 na 90. Kwa hiyo picha hii imenikumbusha mbali sana wakati wa utoto wangu.Asante Lundu Nyasa kwa picha. nimechukua bila kuomba

Wednesday, November 5, 2008

TATIZO NI LIPI?

Mpaka watu wawe na roho mbaya ya:-

Usafirishaji haramu wa watu/biashara ya watu(Human Trafficking) ni nini?
Usafirishaji na biashara haramu ya watu (Human Trafficking) ni nini?

Usafirishaji na biashara haramu ya watu (human trafficking) ni uhamisho wa mtu kutoka kwenye jumuiya yake na kwenda sehemu nyingine ndani au nje ya nchi kwa ahadi za uongo, matokeo yake ni kunyonywa kunyanyaswa, na kutumikishwa kwa kupindukia bila ya ujira kwa faida ya mtu mwengine, hii hujulikana kama utumwa mamboleo na ni moja ya matishio makubwa ya haki za binadamu. Ingawa usafirishaji na biashara haramu ya watu (human trafficking) huwatokea wanaume, wanawake na watoto, lakini inaonekana wanawake na watoto ndio wanaoathirika zaidi.


Usafirishaji na biashara haramu ya watu hutokea duniani kote na unyonyaji wa watu hutofautiana kati ya nchi na nchi (watoto kutoka Togo wanatumikishwa na kunyanyaswa katika mashamba ya kakoa Ghana, Wasichana wa Colombia wanalazimishwa ukahaba Japan n.k.)

Usafirishaji haramu wa watu/biashara ya watu katika Tanzania

Hali ya Usafirishaji na biashara haramu ya watu Tanzania.

Usafirishaji na biashara haramu ya watu (human trafficking) hutokea ndani ya Tanzania na kimataifa. Watu huletwa Tanzania kutoka Kenya, Uganda, Malawi na Burundi. Usafirishaji na biashara haramu ya watu unaoonekana kutapakaa sana ni ule wa ndani kwa ndani ya nchi unaolenga kuwanyonya watoto katika kazi za ndani.
Tanzania pia inatumiwa kama nchi ya kupitishia wahanga wa usafirishaji na biashara haramu ya watu toka nchi za pembe ya Afrika(Ethiopia, Somalia) wanaopelekwa Afrika kusini: Kuna wimbi la wahamiaji haramu wanaoingia
Tanzania ambao serikali ya Tanzania inahisi miongoni mwao wapo wahanga wa usafirishaji na biashara haramu ya watu. Kuna ushahidi wa matukio ambayo yanaonyesha kuna wahanga wa usafirishaji na biashara haramu kutoka India na Pakistan kuletwa Tanzania.

Watoto wahanga wa usafirishaji na biashara haramu ya watu waliosaidiwa na Shirika la Kimataifa la Uhamiaji/International Organization for Migration (IOM) wengi wao hutokea sana mikoa ya Iringa, Morogoro, Mbeya, Mwanza Singida na Dodoma. Zipo dalili kubwa kwamba Dar es Salaam na Zanzibar ndio vituo vikubwa wanaopelekwa wahanga hao. Watoto hao kawaida hutolewa vijijini kwa kuahidiwa maisha bora na elimu mjini na ndugu zao wa karibu au watu wanaoaminiwa na wazazi wao. Wakati mwingine watoto hawa hutolewa na wazazi wao kwa ndugu kwa mategemeo watoto wao watapata maisha bora wakiwa mjini.
Lakini wakati mwingine hali huwa sio kama walivyotegemea. Unyonyaji ni pamoja na kumlazimisha muhanga kufanya ukahaba, kazi za ndani, biashara za mitaani, kuosha magari bila kupewa nafasi ya elimu na matibabu, bila chakula au chakula kidogo sana, kunyanyaswa kijinsia, kutukanwa, kupigwa, kutishwa na kufanyishwa kazi bila ya ujira. Wengi wa watoto hawa wakifanikiwa kutoroka, huishia mitaani.

Sababu

Elimu ni moja ya sababu kubwa. Upatikanaji mkubwa wa elimu mjini huvutia vijana wa kike na kiume kutoka vijijini, wahanga wengi waliosaidiwa na IOM ni watoto walioacha shule au hawajawahi kwenda shule kabisa kijijini mwao (watoto wa kike 24 kati ya 34 waliosaidiwa mwaka 2007 hawakuwahi kwenda shule kabisa).
Kupoteza wazazi wote wawili. Hali hii husababisha watoto kulazimika kutegemea walezi.

Tuesday, November 4, 2008

MAISHA +NDOA MKE NA MUME




Kwa mawazo au akili yangu sijui ipi ni kweli au uwongo kwani labda ni kweli kila mtu duniani hapa ameumbika tofauti. Ni mungu peke yake anajua au labda ni wewe peke yako na nafsi yako ndiyo wajuzi.

MAISHA + NDOA YA WANAUME KWA WANAUME




Labda sababu ya kupenda, kazi kweli kweli ila labda kweli sababu ya kupenda semeni ninyi

MAISHA YA NDOA YA MKE KWA MKE





Semeni ninyi. mimi sina la kusema. Labda sababu ya kupenda au?

Monday, November 3, 2008

JE? MATATIZO NI KAWAIDA KATIKA MAISHA?

Matatizo, Matatizo kila kitu ninachofanya ni tatizo. Hata pumzi ninayotoa ni tatizo. Hata yule/wale ninaye/ninaowapenda ni tatizo.

Mwenzenu naumia, ninalia matatizo. Oh, matatizo matatizo. hata wale ninaowajali hawajali. Hata wale ninaowapenda hawanipendi niambieni nielewe ni kwa nini mimi, ninalia. Matatizo, matatizo.

Ni matatizo ya kila siku lakini yangu ni mazito niambieni nifanyeje ili niondoe matatizo haya. Maana kila kukicha ni matatizo, ni matatizo ni matatizo.

Saturday, November 1, 2008

LEO NI SIKUKUU YA MAREHEMU


Leo hapa Sweden ni sikuuu ya marehemu labda sehemu nyingine pia ila sina uhakika. Kwa hiyo napenda kuwakumbuka Marehemu wote kwa sala hii:-

Salamu, Maria, umejaa neema,
Bwana yu nawe,umebarikiwakuliko wanawake wote,
Na Yesu, mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
Maria mtakatifu, Mama wa Mungu,
Utuombee sisi wakosefu,
Sasa na saa ya kufa kwetu,Amina.
Marehemu wote wastarehe kwa amani, Amina.

Na hapa sala yangu:


Bikikira Maria mama wa msaada,
Na uwabariki watu wote wa dunia hii,
Uwaokoe katika dhambi. Amina.